< Waefeso 4 >

1 Kwa hiyo, kama mfungwa kwa ajili ya Bwana, nawasihi mtembee sawasawa na wito ambao Mungu aliwaita.
I therefore, the prisoner in the Lord, call on you to walk worthily of the calling in which ye were called,
2 Muishi kwa unyenyekevu mkuu na upole na uvumilivu. Mkichukuliana katika upendo.
with all humility and meekness, with longsuffering, forbearing each other in love.
3 Fanyeni bidii kuutunza umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
Endeavoring to keep the unity of the Spirit in the bond of peace,
4 Kuna mwili mmoja na Roho moja, kama ambavyo pia mlikuwa mmeitwa katika uhakika wa taraja moja la wito wenu.
one body, and one Spirit. Just as also ye were called in one hope of your calling,
5 Na kuna Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja,
one Lord, one faith, one immersion,
6 na Mungu mmoja na Baba wa wote. Yeye yuko juu ya yote, na katika yote na ndani ya yote.
one God and Father of all. He is over all, and through all, and in us all.
7 Kwa kila mmoja wetu amepewa kipawa kulingana na kipimo cha kipawa cha Kristo.
But the grace was given to each of us, according to the measure of the gift of the Christ.
8 Ni kama maandiko yasemavyo: “Alipopaa juu sana, aliongoza mateka katika utumwa. Akatoa vipawa kwa watu.”
Therefore he says, Having ascended on high, he led captivity captive, and gave gifts to men.
9 Ni nini maana ya, “Alipaa,” isipokuwa kwamba alishuka pia pande za chini za dunia?
And what is the ascended, except that he also first descended into the lower parts of the earth?
10 Yeye ambaye alishuka ni mtu yuleyule ambae pia alipaa mbali juu ya mbingu zote. Alifanya hivi ili uwepo wake uwe katika vitu vyote.
He who descended is also the same man who ascended high above all the heavens, so that he might fill all things.
11 Kristo alitoa vipawa kama hivi: mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji, na waalimu.
And indeed he gave the apostles, and the prophets, and the evangelists, and the shepherds and teachers
12 Alifanya hivi kuwawezesha waumini kwa ajili ya kazi ya huduma, kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo.
for the perfecting of the sanctified, for the work of ministry, for edification of the body of the Christ.
13 Anafanya hivi hadi sisi sote tufikie umoja wa imani na maarifa ya mwana wa Mungu. Anafanya hivi hadi tuweze kukomaa kama wale waliofikia kimo kamili cha Kristo.
Until we all attain to the unity of the faith, and of the knowledge of the Son of God, to a perfect man, to a standard of stature of the fullness of the Christ.
14 Hii ni ili kwamba tusiwe tena kama watoto, tusirushwerushwe huku na huko. Ili kwamba tusichukuliwe na kila aina ya upepo wa fundisho, kwa hila za watu katika ujanja wa udanganyifu uliopotoka.
So that we may no longer be childish, tossed about and carried about by every wind of doctrine by the trickery of men in craftiness with the methodology of error.
15 Badala yake, tutaongea ukweli katika upendo na kukua zaidi katika njia zote ndani yake ambaye ndiye kichwa, Kristo.
But being truthful in love, we may cause all things to grow for him who is the head-the Christ-
16 Kristo ameunganisha, kwa pamoja, mwili wote wa waumini. Umeungamanishwa pamoja na kila kiungo ili kwamba mwili wote ukue na kujijenga wenyewe katika upendo.
from whom the whole body, joined together and united together through every connection of the supply, according to the working of each one part within a standard, makes the growth of the body for the construction of itself by love.
17 Kwa hiyo, nasema hili, na nawasihi katika Bwana: Msitembee tena kama watu wa mataifa wanavyotembea katika ubatili wa akili zao.
This I say therefore, and solemnly declare in the Lord, for you to walk no longer as also the other Gentiles walk, in the vanity of their mind,
18 Wametiwa giza katika mawazo yao. Wamefukuzwa kutoka katika uzima wa Mungu kwa ujinga ulio ndani yao kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao.
darkened in their understanding, alienated from the life of God through the ignorance that is in them, because of the callousness of their heart.
19 Hawajisikii aibu. Wamejikabidhi wenyewe kwa ufisadi katika matendo machafu, katika kila aina ya uchoyo.
Who, having become callous, gave themselves over to licentiousness for the work of all uncleanness in greed.
20 Lakini, hivi sivyo mlivyojifunza kuhusu Kristo.
But ye did not so learn the Christ,
21 Nadhani kwamba mmesikia kuhusu yeye. Nadhani kwamba mmekuwa mkifundishwa katika yeye, kama tu ukweli ulivyo ndani ya Yesu.
if indeed ye heard him, and were taught in him, as truth is in Jesus,
22 Lazima mvue mambo yote yanayoendana na mwenendo wenu wa zamani, utu wa zamani. Ni utu wa zamani unaooza kwa sababu ya tamaa za udanganyifu.
for you to put off the old man according to your former conduct, the man who is corrupt according to the desires of deceitfulness,
23 Vueni utu wenu wa zamani ili kwamba mfanywe upya katika roho ya akili zenu.
and to be renewed in the spirit of your mind,
24 Fanyeni hivi ili muweze kuvaa utu mpya, unaoendana na Mungu. Umeumbwa katika haki na utakatifu wa kweli.
and to put on the new man according to God, the man who was created in righteousness and piety of the truth.
25 Kwa hiyo, weka mbali udanganyifu. “Ongeeni ukweli, kila mmoja na jirani yake,” kwa sababu tu washirika kwa kila mmoja kwa mwenzake.
Therefore having put off falsehood, let each man speak truth with his neighbor, because we are body-parts of each other.
26 Mwe na hasira, lakini msitende dhambi.” Jua lisizame mkiwa katika hasira zenu.
Be ye angry, and sin not. Let not the sun go down upon your wrath,
27 Msimpe Ibilisi nafasi.
neither give a place to the devil.
28 Yeyote aibaye lazima asiibe tena. Badala yake ni lazima afanye kazi. Afanye kazi yenye manufaa kwa mikono yake, ili kwamba aweze kumhudumia mtu aliye na hitaji.
Let the man who steals steal no more, but rather let him labor, working with his hands the good, so that he may have to give to him who has need.
29 Kauli mbaya isitoke kinywani mwenu. Badala yake, maneno lazima yatoke katika vinywa vyenu yafaayo kwa mahitaji, kuwapa faida wale wanaosikiliza.
Let no corrupt speech go out of your mouth, rather if there is any good word for edification of a need, so that it may give grace to those who hear.
30 Na msimhuzunishe Roho Mtakatifu wa Mungu. Ni kwa Yeye kwamba mmewekewa muhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi.
And do not grieve the Holy Spirit of God, in which ye are sealed for a day of redemption.
31 Lazima muweke mbali uchungu wote, ghadhabu, hasira, ugomvi, na matusi, pamoja na kila aina ya uovu. Iweni wema ninyi kwa ninyi.
Let all bitterness, and wrath, and anger, and clamor, and reviling be taken away from you, with all evil.
32 Mwe na huruma. Msameheane ninyi kwa ninyi, kama vile Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
And become good toward each other, compassionate, forgiving each other, even as also God in Christ forgave us.

< Waefeso 4 >