< Waefeso 3 >

1 Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
For this reason I, Paul, the prisoner of Christ Jesus on behalf of you Gentiles -
2 Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
for surely you have heard of the stewardship of the grace of God entrusted to me for you?
3 Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
You have heard how by direct revelation the secret truth was made known to me, as I have already briefly written you.
4 Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
By reading what I have written, you can judge of my insight into that secret truth of Christ
5 Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
which was not disclosed to the sons of men in former generations, as it has now been revealed by the Spirit to his holy apostles and prophets,
6 Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
namely, that in Christ Jesus the Gentiles form one body with us the Jews, and are coheirs and copartners in the promise, through the gospel.
7 Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
It is of this gospel I became a minister according to the gift of the power of the grace of God, bestowed on me by the energy of his power.
8 Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
To me, who am less than the least of all saints, has this grace been given, that I should proclaim among the Gentiles the gospel of the unsearchable riches of Christ;
9 inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn g165)
and should make all men see the new dispensation of that secret purpose, hidden from eternity in the God who founded the universe, (aiōn g165)
10 Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
in order that now his manifold wisdom should, through the church, be made known to the principalities and powers in the heavenly sphere,
11 Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn g165)
according to his eternal purpose which he purposed in Christ Jesus our Lord. (aiōn g165)
12 Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
In him we have this fearless confidence and boldness of access through our faith in him.
13 Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
So I beg you not to lose heart over my tribulations in your behalf; they are your glory.
14 Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
For this cause I bend my knees before the Father,
15 ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
from whom every fatherhood in heaven and earth is named,
16 Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
praying him to grant you according to the riches of his glory to be strengthened with might by his Spirit in your inmost being;
17 Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
that Christ may make his home in your hearts through your faith; that you may be so deeply rooted and so firmly grounded in love,
18 Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
that you may be able to comprehend with all the saints what is "the breadth," "the length," "the depth," and "the height,"
19 Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
and may know the love of Christ which transcends all knowing, so that you may be filled with all the "plenitude" of God.
20 Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
Now unto him who, according to his might that is at work within us, is able to do infinitely more than all we ask or even think,
21 kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn g165)
to him be the glory in the church and in Christ Jesus, to all generations, world without end, Amen. (aiōn g165)

< Waefeso 3 >