< Waefeso 3 >
1 Kwa sababu ya hii mimi, Paulo, ni mfungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu Mataifa.
For this cause, I Paul am the prisoner of Iesus Christ for you Gentiles,
2 Na amini ya kwamba mmesikia juu ya kazi ya neema ya Mungu aliyo nipa kwa ajili yenu.
If ye haue heard of the dispensation of the grace of God, which is giuen me to you warde,
3 Nawaandikieni kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu. Huu ni ukweli uliyofichika ambao niliandika kwa kifupi kwenye barua nyingine.
That is, that God by reuelation hath shewed this mysterie vnto me (as I wrote aboue in fewe wordes,
4 Usomapo kuhusu haya, utaweza kutambua busara yangu katika ukweli huu uliofichika kuhusu Kristo.
Whereby when ye reade, ye may knowe mine vnderstanding in the mysterie of Christ)
5 Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa wana wa watu. Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho kwa Mitume waliotengwa na Manabii.
Which in other ages was not opened vnto the sonnes of men, as it is nowe reueiled vnto his holy Apostles and Prophets by the Spirit,
6 Ukweli huu uliofichika ni kwamba watu wa Mataifa ni washiriki wenzetu na wajumbe wenzetu wa mwili. Niwashiriki pamoja na ahadi ya Kristo Yesu kupitia injili.
That the Gentiles should be inheriters also, and of the same body, and partakers of his promise in Christ by the Gospel,
7 Na kwa hili nimefanyika mtumishi kwa zawadi ya neema ya Mungu iliyotolewa kwangu kupitia utendaji wa nguvu yake.
Whereof I am made a minister by the gift of the grace of God giuen vnto me through the effectuall working of his power.
8 Mungu alitoa zawadi hii kwangu, japo kuwa mimi ni mtu mdogo wa wote katika wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu. Zawadi hii ni kwamba inanipasa kuwatangazia mataifa injili yenye utajiri usiochunguzika wa Kristo.
Euen vnto me the least of all Saints is this grace giuen, that I should preach among the Gentiles the vnsearchable riches of Christ,
9 inanipasa kuwaangazia watu wote juu ya nini ni mpango wa Mungu wa siri. Huu ni mpango ambao ulikuwa umefichwa kwa miaka mingi iliyopita, na Mungu ambaye aliviumba vitu vyote. (aiōn )
And to make cleare vnto all men what the fellowship of the mysterie is, which from the beginning of the world hath bene hid in God, who hath created all things by Iesus Christ, (aiōn )
10 Hii ilikuwa kwamba, kupitia Kanisa, watawala na mamlaka katika sehemu za mbingu wapate kujua pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu.
To the intent, that nowe vnto principalities and powers in heauenly places, might be knowen by the Church the manifolde wisedome of God,
11 Haya yangetokea kupitia mpango wa milele ambao aliukamilisha ndani ya Kristo Yesu Bwana wetu. (aiōn )
According to the eternall purpose, which he wrought in Christ Iesus our Lord: (aiōn )
12 Kwa kuwa katika Kristo tuna ujasiri na uwezo wa kuingia kwa ujasiri kwa sababu ya imani yetu kwake.
By whom we haue boldenes and entrance with confidence, by faith in him.
13 Kwa hiyo nawaomba msikate tamaa kwasababu ya mateso yangu kwa ajili yenu. Haya ni utukufu wenu.
Wherefore I desire that ye faint not at my tribulations for your sakes, which is your glory.
14 Kwa sababu hii napiga magoti kwa Baba.
For this cause I bowe my knees vnto the Father of our Lord Iesus Christ,
15 ambaye kwa yeye kila familia mbinguni na juu ya nchi imeitwa jina.
(Of whom is named the whole familie in heauen and in earth)
16 Ninaomba kwamba apate kuwanemesha, kutokana na utajiri wa utukufu wake, awafanye imara kwa nguvu kupitia Roho wake, ambaye yu ndani yenu.
That he might graunt you according to the riches of his glorie, that ye may be strengthened by his Spirit in the inner man,
17 Ninaomba kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani.
That Christ may dwell in your heartes by faith:
18 Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Muwe katika pendo lake ili muweze kuelewa, pamoja na wote waaminio, jinsi upana, na urefu na kimo na kina cha upendo wa Kristo.
That ye, being rooted and grounded in loue, may be able to comprehend with al Saints, what is the breadth, and length, and depth, and height:
19 Ninaomba Kwamba mjue ukuu wa upendo wa Kristo, ambao unazidi ufahamu. Mfanye haya ili mjazwe na ukamilifu wote wa Mungu.
And to knowe the loue of Christ, which passeth knowledge, that ye may be filled with all fulnesse of God.
20 Na sasa kwake yeye awezaye kufanya kila jambo, zaidi ya yote tuyaombayo au tuyawazayo, kupitia nguvu yake itendayo kazi ndani yetu,
Vnto him therefore that is able to do exceeding aboundantly aboue all that we aske or thinke, according to the power that worketh in vs,
21 kwake yeye kuwe utukufu ndani ya kanisa na katika Kristo Yesu kwa vizazi vyote milele na milele. Amina. (aiōn )
Be praise in the Church by Christ Iesus, throughout all generations for euer, Amen. (aiōn )