< Waefeso 2 >

1 Kama vile mlivyo kuwa mmekufa katika makosa na dhambi zenu.
and also you, he filleth, who were dead in your sins, and in your offences,
2 Ilikuwa katika haya kwamba kwanza mlienenda kulingana na nyakati za ulimwengu huu. Mlikuwa mkienenda kwa kufuata mtawala wa mamlaka ya anga. Hii ndiyo roho yake yule afanyaye kazi katika wana wa kuasi. (aiōn g165)
in the which ye before walked, according to the worldliness of this world, and according to the pleasure of the prince potentate of the air, that spirit which is active in the children of disobedience: (aiōn g165)
3 Sisi wote hapo mwanzo tulikuwa miongoni mwa hawa wasioamini. Tulikuwa tukitenda kwa namna ya tamaa mbaya za miili yetu. Tulikuwa tukifanya mapenzi ya mwili na ufahamu wetu. Tulikuwa kwa asili wana wa ghadhabu kama wengine.
in which deeds we also, formerly, were conversant, in the cravings of our flesh; and we did the pleasure of our flesh, and of our mind, and were altogether the children of wrath, like the rest.
4 Lakini Mungu ni mwingi wa rehema kwa sababu ya pendo lake kubwa alilotupenda sisi.
But God who is rich in his mercies, because of the great love with which he loved us,
5 Wakati tulipokuwa wafu katika makosa yetu, alituleta pamoja katika maisha mapya ndani ya Kristo. Ni kwa neema kwamba mmeokolewa.
when we were dead in our sins, quickened us with the Messiah, and rescued us by his grace;
6 Mungu alitufufua pamoja na kutufanya kukaa pamoja katika mahali pa mbingu ndani ya Kristo Yesu.
and resuscitated us with him, and seated us with him in heaven, in Jesus the Messiah:
7 Alifanya hivi ili katika nyakati zijazo aweze kutuonesha utajiri mkuu wa neema yake. Hutuonesha sisi hili kwa njia ya wema wake ndani ya Kristo Yesu. (aiōn g165)
that he might show to the coming ages the magnitude of the riches of his grace, and his benignity towards us in Jesus the Messiah. (aiōn g165)
8 Kwa neema mmeokolewa kwa njia ya imani. Na hii haikutoka kwetu. Ni zawadi ya Mungu.
For it is by his grace we are rescued, through faith; and this is not of yourselves, but it is the gift of God:
9 Haitokani na matendo. Matokeo yake, asiwepo mmoja wapo wa kujisifu.
not of works, lest any one glory.
10 Kwa sababu sisi tu kazi ya Mungu, tumeumbwa katika Kristo Yesu kutenda matendo mema. Ni matendo haya ambayo Mungu aliyapanga tangu zamani za kale kwa ajili yetu, ili tutembee katika hayo.
For we are his creation; who are created in Jesus the Messiah, for good works, which God hath before prepared for us to walk in.
11 Kwa hiyo kumbukeni kwamba hapo zamani mlikuwa watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili. Mnaitwa “msio na tohara” kwa kile kinachoitwa tohara ya mwili inayofanywa kwa mikono ya binadamu.
Wherefore be mindful, that ye formerly were carnal Gentiles; and ye were called the uncircumcision, by that which is called the circumcision, and which is the work of the hands in the flesh.
12 Kwa wakati huo mlikuwa mmetengwa na Kristo. Mlikuwa wageni kwa watu wa Israel. Mlikuwa wageni kwa agano la ahadi. Hamkuwa na uhakika wa wakati ujao. Mlikuwa bila Mungu katika ulimwengiu.
And ye were, at that time, without the Messiah; and were aliens from the regulations of Israel; and strangers to the covenant of the promise; and were without hope, and without God, in the world.
13 Lakini sasa katika Kristo Yesu ninyi ambao hapo mwanzo mlikuwa mbali na Mungu mmeletwa karibu na Mungu kwa damu ya Kristo.
But now, by Jesus the Messiah, ye who before were afar off, have been brought near by the blood of the Messiah.
14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu. Alifanya wawili kuwa mmoja. Kwa mwili wake aliuharibu ukuta wa utengano ambao ulikuwa umetutenganisha, huo uadui.
For he is himself our peace, who hath made the two become one, and hath demolished the wall which stood in the midst, and the enmity, by his flesh;
15 Kwamba alikomesha sheria ya amri na kanuni ili kwamba aumbe mtu mmoja mpya ndani yake. Akafanya amani.
and by his prescriptions he hath abolished the law of ordinances; that, in himself, he might make the two to be one new man; and he hath made peace,
16 Alifanya hivi ili kuwapatanisha makundi mawili ya watu kuwa mwili mmoja kwa Mungu kupitia msalaba. Kwa njia ya msalaba aliufisha uadui.
and hath reconciled both with God, in one body, and hath slain the enmity by his cross.
17 Yesu alikuja na kutangaza amani kwenu ninyi mliokuwa mbali na amani kwao wale waliokuwa karibu.
And he came, and proclaimed peace to you afar off, and to those near:
18 Kwa maana kwa njia ya Yesu sisi wote wawili tuna nafasi kwa yule Roho mmoja kuingia kwa Baba.
because, by him there is access for us both, by one Spirit, unto the Father.
19 Hivyo basi, ninyi watu wa mataifa si wasafiri na wageni tena. Bali ni wenyeji pamoja na wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu na wajumbe katika nyumba ya Mungu.
Wherefore, ye are not strangers, nor sojourners, but ye are fellow-citizens with the saints, and of the household of God.
20 Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii. Kristo Yesu mwenyewe alikuwa jiwe kuu la pembeni.
And ye are built upon the foundations of the legates and the prophets; and Jesus the Messiah hath become the head of the corner in the edifice.
21 Katika yeye jengo lote limeungamanishwa pamoja na kukua kama hekalu ndani ya Bwana.
And in him all the edifice is framed together, and groweth into a holy temple in the Lord;
22 Ni ndani yake ninyi nanyi mnajengwa pamoja kama mahali pa kuishi pa Mungu katika Roho.
while ye also are builded in him, for a habitation of God through the Spirit.

< Waefeso 2 >