< Waefeso 1 >
1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, kwa waliotengwa kwa ajili ya Mungu walioko Efeso na ambao ni waaminifu katika Kristo Yesu.
This letter comes from Paul, an apostle of Christ Jesus according to God's will, to the Christians in Ephesus and those who trust in Christ Jesus.
2 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.
Grace and peace to you from God our Father and the Lord Jesus Christ.
3 Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo apewe sifa. Ni yeye aliyetubariki kwa kila baraka za kiroho, katika mahali pa mbingu ndani ya Kristo.
Praise God the Father of our Lord Jesus Christ, who has blessed us in Christ with all that's spiritually good in the heavenly world,
4 Kabla ya kuumbwa ulimwengu, Mungu alituchagua sisi ambao tunaamini katika Kristo. Alituchagua sisi ili tuweze kuwa watakatifu na tusiolaumika mbele yake.
just as he chose us to be in him before the beginning of this world, so that in love we could be holy and without fault before him.
5 Katika pendo Mungu alituchagua mwanzo kwa kututwaa kama watoto wake kwa njia ya Yesu Kristo. Alifanya hivi kwa sababu alipendezwa kufanya kile alichotamani.
He decided in advance to adopt us as his children, working through Jesus Christ to bring us to himself. He was happy to do this because this is what he wanted.
6 Matokeo yake ni kwamba Mungu anatukuzwa kwa neema ya utukufu wake. Hiki ndicho alichotupatia bure kwa njia ya mpendwa wake.
So we praise him for his glorious grace that he so kindly gave us in his beloved Son.
7 Kwa kuwa katika mpendwa wake, tunaukombozi kupitia damu yake, msamaha wa dhambi. Tunalo hili kwa sababu ya utajiri wa neema yake.
Through him we gain salvation through his blood, the forgiveness of our sins as a result of his priceless grace
8 Alifanya neema hii kuwa nyingi kwa ajili yetu katika hekima na ufahamu.
that he so generously provided for us, together with all wisdom and understanding.
9 Mungu alifanya ijulikane kwetu ile kweli iliyofichika ya mpango, kutokana na hamu iliyodhihirishwa ndani ya Kristo.
He revealed to us his previously-hidden will through which he was happy to pursue his plan
10 Wakati nyakati zimetimia kwa utimilifu wa mpango wake, Mungu ataviweka pamoja kila kitu cha mbinguni na cha juu ya nchi ndani ya Kristo.
at the appropriate time to bring everyone together in Christ—those in heaven and those on the earth.
11 Katika Kristo tulikuwa tumechaguliwa na kukusudiwa kabla ya wakati. Hii ilikuwa ni kutokana na mpango wa anayefanya vitu vyote kwa kusudi la mapenzi yake.
In him—we were chosen beforehand, according to the plan of the one who is working everything out according to his will,
12 Mungu alifanya hivyo ili kwamba tuweze kuwapo kwa sifa ya utukufu wake. Tulikuwa wa kwanza kuwa na ujasiri ndani ya Kristo.
for the purpose that we who were the first to hope in Christ could praise his glory.
13 Ilikuwa kwa njia ya Kristo kwamba mlisikia neno la kweli, injili ya wokovu wenu kwa njia ya Kristo. Ilikuwa katika yeye pia kwamba mmeamini na kutiwa mhuri na Roho Mtakatifu aliye ahidiwa.
In him—you too have heard the word of truth, the good news of your salvation. In him—because you trusted in him you were stamped with the seal of the Holy Spirit's promise,
14 Roho ndiyo dhamana ya urithi wetu mpaka umiliki utakapopatikana. Hii ilikuwa ni kwa sifa ya utukufu wake.
which is a down-payment on our inheritance when God redeems what he's kept safe for himself—us, who will praise and give him glory!
15 Kwa sababu hii, tangu wakati niliposikia kuhusu imani yenu ndani ya Bwana Yesu na kuhusu pendo lenu kwa wale wote ambao wametengwa kwa ajili yake.
That's the reason, because I've heard of your trust in the Lord Jesus and the love that you have for all Christians,
16 Sijaacha kumshukuru Mungu kwa ajili yenu na kuwataja katika maombi yangu.
why I never stop thanking God for you and remember you in my prayers.
17 Ninaomba kwamba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, baba wa utukufu, atawapeni roho ya hekima, mafunuo ya ufahamu wake.
I pray that the God of our Lord Jesus Christ, the glorious Father, may give you a spirit of wisdom to see and know him as he really is.
18 Ninaomba kwamba macho yenu ya moyoni yatiwe nuru kwa ninyi kujua ni upi ujasiri wa kuitwa kwenu. Naomba kwamba mjue utajiri wa utukufu wa urithi wake miongoni mwa wale waliotengwa kwa ajili yake.
May your minds be enlightened so you can understand the hope he's called you to— the glorious riches he promises as an inheritance to his holy people.
19 Naomba kwamba ujue ukuu uzidio wa nguvu yake ndani yetu ambao tunaamini. Huu ukuu ni kutokana na kufanya kazi katika nguvu zake.
May you also understand God's amazing power
20 Hii ni nguvu iliyofanya kazi ndani ya Kristo wakati Mungu alipomfufua kutoka kwa wafu na kumketisha katika mkono wake wa kuume katika mahali pa mbingu.
that he demonstrated in raising Christ from the dead. God seated Christ at his right hand in heaven,
21 Alimketisha Kristo juu mbali na utawala, mamlaka, nguvu, enzi, na kila jina litajwalo. Alimketisha Yesu si tu kwa wakati huu lakini kwa wakati ujao pia. (aiōn )
far above any other ruler, authority, power, or lord, or any leader with all their titles—not only in this world, but also in the coming world too. (aiōn )
22 Mungu amevitiisha vitu vyote chini ya miguu ya Kristo. Amemfanya yeye kichwa juu ya vitu vyote katika kanisa.
God has made everything subject to the authority of Christ, and has given him the responsibility as head over everything for the church,
23 Ni kanisa kwamba ndilo mwili wake, ukamilifu wake ambaye hujaza vitu vyote katika njia zote.
which is his body, filled full and made complete by Christ, who fills and brings everything to completion.