< Mhubiri 1 >
1 Haya ni maneno ya Mwalimu, mwana wa Daudi na mfalme katika Yerusalemu.
The words of the Preacher, the son of David, king in Jerusalem.
2 Mwalimu asema hivi, “Kama mvuke wa ukungu, kama upepo mwanana katika upepo, kila kitu hutoweka na kuacha maswali mengi.
Vanity of vanities, says the Preacher, vanity of vanities; all is vanity.
3 Ni faida gani wanadamu huipata kutoka katika kazi zote wazifanyazo chini ya jua?
What profit has a man of all his labor which he takes under the sun?
4 Kizazi kimoja huenda, na kizazi kingine huja, lakini nchi yabaki milele.
One generation passes away, and another generation comes: but the earth stays for ever.
5 Jua huchomoza na jua huzama na kwenda kwa kasi, na kurudi mahali linapochomozea tena.
The sun also rises, and the sun goes down, and hastens to his place where he arose.
6 Upepo huvuma kusini na huzunguka kasikazi, na mara zote ukizunguka katika njia yake na kurudi tena.
The wind goes toward the south, and turns about to the north; it whirls about continually, and the wind returns again according to his circuits.
7 Mito yote hutiririka katika bahari, lakini bahari haijai. Mahali mito inakoenda, ndiko inakoenda tena.
All the rivers run into the sea; yet the sea is not full; to the place from where the rivers come, thither they return again.
8 Kila kitu huwa uchovu, na hakuna yeyote awezae kukielezea. Jicho halishibina kile linachokiona, wala sikio halishibi na kile linachosikia.
All things are full of labor; man cannot utter it: the eye is not satisfied with seeing, nor the ear filled with hearing.
9 Chochote kilichopo ndicho kitakachokuwepo, kila kilichofanyika ndicho kitakachofanyika. Hakuna jipya chini ya jua.
The thing that has been, it is that which shall be; and that which is done is that which shall be done: and there is no new thing under the sun.
10 Je kuna jambo lolote ambalo watu wanaweza kusema, 'Tazama, hili ni jipya'? Chochote kilichopo kimekwisha kuwepo muda mwingi, wakati uliokuwepo kabla yetu.
Is there any thing whereof it may be said, See, this is new? it has been already of old time, which was before us.
11 Hakuna anayeonekana kukumbuka kilichotokea nyakati za zamani. Na mambo yaliyo tokea siku zilizo pita na yale yatakayo tokea siku za mbele nayo hayatakumbukwa.”
There is no remembrance of former things; neither shall there be any remembrance of things that are to come with those that shall come after.
12 Mimi ni mwalimu, na nimekuwa mfalme juu ya Isareli katika Yerusalemu.
I the Preacher was king over Israel in Jerusalem.
13 Nilitia akili yangu katika kusoma na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachofanywa chini ya mbingu. Hili nalo ni jukumu zito ambalo Mungu amewapa wana wa watu kujishughulisha nalo.
And I gave my heart to seek and search out by wisdom concerning all things that are done under heaven: this sore travail has God given to the sons of man to be exercised therewith.
14 Nimeona matendo yote ambayo yanafanyika chini ya jua, na tazama yote ni mvuke ni kujaribu kuuchunga upepo.
I have seen all the works that are done under the sun; and, behold, all is vanity and vexation of spirit.
15 Palipopinda hapawezi kunyoshwa! Kisicho kuwepo hakiwezi kuhesabiwa!
That which is crooked cannot be made straight: and that which is wanting cannot be numbered.
16 Nimeuambia moyo wangu nikisema, “Tazama, nimepata hekima kubwa kuliko walioishi Yerusalemu kabla yangu. Akili yangu imeona hekima kubwa na ufahamu.”
I communed with my own heart, saying, See, I am come to great estate, and have gotten more wisdom than all they that have been before me in Jerusalem: yes, my heart had great experience of wisdom and knowledge.
17 nimetia moyo wangu kujua hekima na upumbuvu na ujinga. Nikagundua kuwa hili nalo pia lilikuwa ni kujaribu kuuchunga upepo.
And I gave my heart to know wisdom, and to know madness and folly: I perceived that this also is vexation of spirit.
18 Kwa kuwa katika wingi wa hekima kuna masumbufu mengi, naye aongezae ujuzi, aongeza masikitiko.
For in much wisdom is much grief: and he that increases knowledge increases sorrow.