< Mhubiri 8 >

1 Ni mtu gani mwenye hekima? Ambaye anafahamu matukio yana maana gani katika maisha? Hekima ndani ya mtu husababisha uso wake kung'ara, na ugumu wa uso wake hubadilika.
Qui est comme le sage? Et qui connaît l'interprétation d'une chose? La sagesse d'un homme fait briller son visage, et la dureté de son visage est changée.
2 Ninakushauri kuitii amri ya mfalme kwa sababu ya kiapo cha Mungu cha kumlinda yeye.
Je dis: « Exécutez l'ordre du roi! » à cause du serment fait à Dieu.
3 Usiharakishe kuondoka mbele ya uwepo wake, na usisimame kuunga mkono jambo lisilofaa, kwa kuwa mfalme anafanya chochote anacho tamani.
Ne vous empressez pas de vous soustraire à sa présence. Ne persiste pas dans une mauvaise action, car il fait ce qui lui plaît,
4 Neno la mfalme hutawala, kwa hiyo ni nani atakaye mwambia, 'Unafanya nini?
car la parole du roi est suprême. Qui peut lui dire: « Que fais-tu? »
5 Yeyote ashikaye amri za mfalme hukwepa madhara. Moyo wa mwenye hekima hutambua mwelekeo muafaka na muda wa kuenda.
Celui qui garde le commandement ne risque rien, et son cœur avisé connaîtra le temps et la procédure.
6 Kwa kuwa kila jambo lina jibu sahihi, na wakati wa kujibu, kwa sababu taabu ya mtu ni kubwa.
Car il y a un temps et une procédure pour toute fin, bien que la misère de l'homme soit lourde pour lui.
7 Hakuna anaye fahamu kinacho fuata. Ni nani awezaye kumwambia nini kinacho kuja?
Car il ne sait pas ce qui sera; car qui peut lui dire comment cela se passera?
8 Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa; wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile; wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea.
Il n'y a pas d'homme qui ait pouvoir sur l'esprit pour contenir l'esprit; il n'a pas non plus pouvoir sur le jour de la mort. Il n'y a pas de décharge dans la guerre; et la méchanceté ne délivrera pas ceux qui la pratiquent.
9 Mambo hayo yote nimeyaona, nikatia moyo wangu katika kila kazi iliyofanyika chini ya jua. Kuna wakati ambapo mtu mmoja anayo mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasira yake.
J'ai vu tout cela, et j'ai appliqué mon esprit à toutes les œuvres qui se font sous le soleil. Il y a un temps où un homme a sur un autre un pouvoir qui lui nuit.
10 Hivyo niliwaona wabaya wakizikwa hadharani. Waliondolewa mahali patakatifu na kuzikwa mahali waliposifiwa na watu katika mji walipokuwa wamefanya matendo maovu. Hii nayo haifai.
J'ai donc vu les méchants ensevelis. En effet, ils venaient aussi de la sainteté. Ils sont partis et ont été oubliés dans la ville où ils ont agi. Cela aussi est une vanité.
11 Wakati hukumu dhidi ya tendo ovu haihukumiwi haraka, hushawishi mioyo ya wanadamu kutenda ubaya.
Parce que la sentence contre une œuvre mauvaise ne s'exécute pas promptement, le cœur des fils de l'homme est tout disposé à faire le mal.
12 Hata kama mwenye dhambi afanye uovu mara mia moja na bado aishi kwa muda mrefu, bado ninafahamu itakuwa vyema kwa wale wanao muheshimu Mungu, wanaouheshimu uwepo wake walio nao.
Quand un pécheur commettrait cent fois des crimes, et qu'il vivrait longtemps, je sais cependant qu'il en sera de même pour ceux qui craignent Dieu, qui sont respectueux devant lui.
13 Lakini haitakuwa vyema kwa mtu mwovu; mkewe hatacheleweshwa. Siku zake kama kizuri kitowekacho upesi, kwa sababu hamuheshimu Mungu.
Mais le méchant ne sera pas heureux, et il prolongera ses jours comme une ombre, parce qu'il ne craint pas Dieu.
14 Kuna mvuke mwingine usio faa, jambo jingine linaofanyika juu ya dunia. Mambo hutokea kwa watu wenye haki kama yatokeavyo kwa watu waovu, na mambo hutokea kwa wenye haki kama yatokeavyo kwa waovu. Ninasema hili pia ni mvuke usiofaa.
Il y a une vanité qui se fait sur la terre, c'est qu'il y a des hommes justes à qui il arrive selon l'œuvre des méchants. Encore une fois, il y a des méchants à qui il arrive d'agir selon l'œuvre des justes. J'ai dit que cela aussi est une vanité.
15 Kwa hiyo nikapendekeza furaha, kwa sababu mtu hana jambo bora chini ya jua zaidi ya kula na kunywa na kuwa na furaha. furaha ndiyo itamfuata katika kazi zake kwa siku zote za maisha yake ambayo Mungu amempa chini ya jua.
Puis j'ai fait l'éloge de la joie, parce que l'homme n'a rien de mieux sous le soleil que de manger, de boire et de se réjouir, car cela l'accompagnera dans son travail tous les jours de sa vie que Dieu lui a donnés sous le soleil.
16 Nikauweka moyo wangu kufamu hekima na kufahamu kazi inayofanyika juu ya nchi, kazi ambayo inafanyika mara nyingi pasipo kufumba macho usiku au mchana.
Quand j'ai appliqué mon cœur à connaître la sagesse, et à voir les affaires qui se font sur la terre (bien que les yeux ne voient pas le jour ni la nuit),
17 Kisha nika tafakari matendo yote ya Mungu, na kwamba mtu hawezi kuelewa kazi inayofanyika chini ya jua. Bila kujali mtu anafanya kupata majibu, hatayapata. Ingawa mwenye hekima anaweza kuamini anajua, kitu kweli hajui.
alors j'ai vu toute l'œuvre de Dieu, que l'homme ne peut pas découvrir l'œuvre qui se fait sous le soleil, parce que même si un homme s'efforce de la chercher, il ne la trouvera pas. Oui, même si un homme sage pense pouvoir la comprendre, il ne pourra pas la trouver.

< Mhubiri 8 >