< Mhubiri 7 >

1 Jina zuri ni bora kuliko manukato ya gharama, na siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.
Dobro ime je boljše kakor dragoceno mazilo in dan smrti [je boljši] kakor dan rojstva nekoga.
2 Ni bora kwenda kwenye nyumba ya maombolezo kuliko nyumba ya karamu, kwa kuwa maombolezo huja kwa watu wote wakati wa mwisho wa uhai, kwa hiyo watu wanaoishi ni lazima waweke hili moyoni.
Bolje je iti v hišo žalujočega, kakor iti v hišo pojedine, kajti to je konec vseh ljudi; in živi si bodo to položili k srcu.
3 Huzuni ni bora kuliko kicheko, kwa kuwa baada ya uso wa huzuni huja furaha ya moyo.
Bridkost je boljša kot smeh, kajti z žalostjo obličja je srce postalo boljše.
4 Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya karamu.
Srce modrega je v hiši žalovanja, toda srce bedakov je v hiši veselja.
5 Ni bora kusikiliza maonyo ya mtu mwenye hekima kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
Bolje je poslušati oštevanje modrega, kakor za človeka poslušati pesem bedakov.
6 Kwa kuwa kama mlio wa miiba chini ya chungu, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Huu pia ni mvuke.
Kajti kakor je prasketanje trnja pod loncem, tak je smeh bedaka. Tudi to je ničevost.
7 kweli jeuri humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, na rusha huharibu moyo.
Zatiranje modrega zagotovo dela besnega in podkupnina uničuje srce.
8 Ni heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo; na watu wenye uvumilivu ni bora kuliko wenye majivuno rohoni.
Boljši je konec stvari kakor njen začetek, in potrpežljivi v duhu je boljši kakor ponosni v duhu.
9 Usikasirike haraka rohoni mwako, kwa sababu hasira hukaa katika mioyo ya wapumbavu.
V svojem duhu ne bodi nagel, da bi bil jezen, kajti jeza počiva v naročju bedakov.
10 Usiseme, “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa kuwa sio kwa sababu ya hekima kwamba unauliza swali hili.
Ne reci: »Kaj je razlog, da so bili prejšnji dnevi boljši kakor tile?« Kajti glede tega nisi modro poizvedel.
11 Hekima ni njema kama vitu vya thamani tunavyorithi kutoka kwa wazazi wetu. Inatoa faida kwa wale wanaoliona jua.
Modrost je dobra z dediščino; in z njo je korist tistim, ki gledajo sonce.
12 Kwa kuwa hekima hutoa ulinzi kama vile fedha inavyoweza kutoa ulinzi, lakini faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai kwa yeyote aliye nayo.
Kajti modrost je obramba in denar je obramba, toda odličnost spoznanja je, da modrost daje življenje tem, ki jo imajo.
13 Tafakaria matendo ya Mungu: Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?
Preudari Gospodovo delo, kajti kdo lahko izravna to, kar je on skrivil?
14 Wakati nyakati vinakuwa njema, ishi kwa furaha katika hali hiyo, lakini wakati unapokuwa mbaya, tafakari hili: Mungu ameruhusu hali zote ziwepo, Kwa sababu hii, hakuna mwanadamu yeyote atakaye fahamu chochote kinacho kuja baada yake.
Na dan uspevanja bodi radosten, toda na dan nadloge preudari; tudi Bog je postavil enega nasproti drugemu, z namenom, da človek ne bi ničesar našel za njim.
15 Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
Vse stvari sem videl v dneh svoje ničevosti. Je pravičen človek, ki propada v svoji pravičnosti in je zloben človek, ki v svoji zlobnosti podaljšuje svoje življenje.
16 Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
Ne bodi preko mere pravičen niti se ne delaj preveč modrega. Zakaj bi samega sebe uničil?
17 Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
Ne bodi preveč zloben niti ne bodi nespameten. Zakaj bi umrl pred svojim časom?
18 Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
Dobro je, da bi to zgrabil, da, tudi pred tem ne umikaj svoje roke, kajti kdor se boji Boga, bo izmed vseh prišel naprej.
19 Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
Modrost krepi modrega bolj kakor deset silnih mož, ki so v mestu.
20 Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
Kajti na zemlji ni pravičnega človeka, ki dela dobro in ne greši.
21 Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
Prav tako se ne oziraj na vse besede, ki so izgovorjene, da ne bi slišal svojega služabnika [kako] te preklinja,
22 Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
kajti pogosto tudi tvoje lastno srce ve, da si ti sam podobno preklinjal druge.
23 Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
Vse to sem preizkusil z modrostjo. Rekel sem: »Moder bom, « toda to je bilo daleč od mene.
24 Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
To, kar je daleč proč in presegajoče globoko, kdo to lahko spozna?
25 Nikageuza moyo wangu kujifunza kuchunguza na kutafuta hekima na ufafanuzi wa ukweli, na kufahamu kwamba ubaya ni ujinga na kwamba upumbavu ni wazimu.
Svoje srce sem posvetil védenju in preiskovanju in iskanju modrosti in razlogu za stvari in da spoznam zlobnost neumnosti, celo nespametnost in norost.
26 Nikapata kufahamu kwamba uchungu kuliko kifo, ndivo alivyo mwanamke yeyote ambaye moyo wake umejaa mitego, na nyavu, na ambaye mikono yake ni minyororo. Yeyote ampendezaye Mungu ataponyoka kutoka kwake, lakini mwenye dhambi atachukuliwa naye.
Našel sem grenkejše kakor smrt, žensko, čigar srce so pasti in mreže in njene roke kakor trakovi. Kdorkoli ugaja Bogu, bo zbežal pred njo, toda grešnik bo vzet po njej.
27 “Tafakari kile nilichovumbua,” asema Mwalimu. “Nimekuwa nikiongeza uvumbuzi mmoja hadi mwingine ili kwamba nipate ufafanuzi wa ukweli.
»Glej, to sem našel, « pravi pridigar, naštevajoč enega za drugim, da spozna razlog.
28 Hii ndiyo bado natafuta, lakini bado sijapata. Sikupata mwanamme mmoja mwenye haki miongoni mwa elfu, lakini sikupata mwanamke miongoni mwa wale wote.
Kar vendar moja duša išče, toda ne najdem. Našel sem enega med tisočimi, toda ženske med vsemi tistimi nisem našel.
29 Nimegundua hili: kwamba Mungu alimuumba binadamu akiwa mnyoofu, lakini wametoka katika hali ya unyofu wakitafuta magumu mengi.
Glej, samo to sem našel, da je Bog človeka naredil poštenega, toda oni so iskali mnoge domiselnosti.

< Mhubiri 7 >