< Mhubiri 7 >
1 Jina zuri ni bora kuliko manukato ya gharama, na siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.
A good name is betere than preciouse oynementis; and the dai of deth is betere than the dai of birthe.
2 Ni bora kwenda kwenye nyumba ya maombolezo kuliko nyumba ya karamu, kwa kuwa maombolezo huja kwa watu wote wakati wa mwisho wa uhai, kwa hiyo watu wanaoishi ni lazima waweke hili moyoni.
It is betere to go to the hous of morenyng, than to the hous of a feeste; for in that hous `of morenyng the ende of alle men is monestid, and a man lyuynge thenkith, what is to comynge.
3 Huzuni ni bora kuliko kicheko, kwa kuwa baada ya uso wa huzuni huja furaha ya moyo.
Yre is betere than leiyyng; for the soule of a trespassour is amendid bi the heuynesse of cheer.
4 Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya karamu.
The herte of wise men is where sorewe is; and the herte of foolis is where gladnesse is.
5 Ni bora kusikiliza maonyo ya mtu mwenye hekima kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu.
It is betere to be repreued of a wijs man, than to be disseyued bi the flateryng of foolis;
6 Kwa kuwa kama mlio wa miiba chini ya chungu, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu. Huu pia ni mvuke.
for as the sown of thornes brennynge vndur a pot, so is the leiyyng of a fool. But also this is vanyte.
7 kweli jeuri humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu, na rusha huharibu moyo.
Fals chalenge disturblith a wijs man, and it schal leese the strengthe of his herte.
8 Ni heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo; na watu wenye uvumilivu ni bora kuliko wenye majivuno rohoni.
Forsothe the ende of preyer is betere than the bigynnyng. A pacient man is betere than a proud man.
9 Usikasirike haraka rohoni mwako, kwa sababu hasira hukaa katika mioyo ya wapumbavu.
Be thou not swift to be wrooth; for ire restith in the bosum of a fool.
10 Usiseme, “Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko siku hizi?” Kwa kuwa sio kwa sababu ya hekima kwamba unauliza swali hili.
Seie thou not, What gessist thou is of cause, that the formere tymes weren betere than ben now? for whi siche axyng is fonned.
11 Hekima ni njema kama vitu vya thamani tunavyorithi kutoka kwa wazazi wetu. Inatoa faida kwa wale wanaoliona jua.
Forsothe wisdom with richessis is more profitable, and profitith more to men seynge the sunne.
12 Kwa kuwa hekima hutoa ulinzi kama vile fedha inavyoweza kutoa ulinzi, lakini faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai kwa yeyote aliye nayo.
For as wisdom defendith, so money defendith; but lernyng and wisdom hath this more, that tho yyuen lijf to `her weldere.
13 Tafakaria matendo ya Mungu: Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?
Biholde thou the werkis of God, that no man may amende hym, whom God hath dispisid.
14 Wakati nyakati vinakuwa njema, ishi kwa furaha katika hali hiyo, lakini wakati unapokuwa mbaya, tafakari hili: Mungu ameruhusu hali zote ziwepo, Kwa sababu hii, hakuna mwanadamu yeyote atakaye fahamu chochote kinacho kuja baada yake.
In a good day vse thou goodis, and bifore eschewe thou an yuel day; for God made so this dai as that dai, that a man fynde not iust playnyngis ayens hym.
15 Nimeona mambo mengi katika siku zangu za ubatili. Kuna watu wenye haki ambao wanaangamia licha ya kwamba wana haki, na kuna watu waovu wanaoishi maisha marefu licha ya kwamba ni waovu.
Also Y siy these thingis in the daies of my natyuyte; a iust man perischith in his riytfulnesse, and a wickid man lyueth myche tyme in his malice.
16 Usiwe mwenye haki katika macho yako mwenyewe. Kwa nini kujiharibu mwenyewe?
Nyle thou be iust myche, nether vndurstonde thou more than is nedeful; lest thou be astonyed.
17 Usiwe mwovu sana au mpumbavu. Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?
Do thou not wickidli myche, and nyle thou be a fool; lest thou die in a tyme not thin.
18 Ni vyema kwamba ushike hekima hii, na kwamba usiache haki iende zake. Kwa kuwa mtu amchae Mungu atatimiza ahadi zake zote.
It is good, that thou susteyne a iust man; but also withdrawe thou not thin hond from hym; for he that dredith God, is not necligent of ony thing.
19 Hekima ina nguvu ndani ya mwenye hekima, zaidi ya watawala kumi katika mji.
Wisdom hath coumfortid a wise man, ouer ten pryncis of a citee.
20 Hakuna mtu mwenye haki juu ya nchi anayefanya mema na hatendi dhambi.
Forsothe no iust man is in erthe, that doith good, and synneth not.
21 Usisikilize kila neno linaongelewa, kwa sababu unaweza kusikia mtumishi wako anakulaani.
But also yyue thou not thin herte to alle wordis, that ben seid; lest perauenture thou here thi seruaunt cursynge thee;
22 Vivyo hivyo unafahamu mwenyewe ndani ya moyo wako umewalaani wengine mara kadhaa.
for thi conscience woot, that also thou hast cursid ofte othere men.
23 Haya yote nimeyathibitisha kwa hekima. Nikasema, “nitakuwa mwenye hekima,” lakini zaidi ambavyo ningekuwa.
I asayede alle thingis in wisdom; Y seide, I schal be maad wijs, and it yede awei ferthere fro me, myche more than it was;
24 Hekima i mbali na kina sana. Ni nani awezaye kuipata?
and the depthe is hiy, who schal fynde it?
25 Nikageuza moyo wangu kujifunza kuchunguza na kutafuta hekima na ufafanuzi wa ukweli, na kufahamu kwamba ubaya ni ujinga na kwamba upumbavu ni wazimu.
I cumpasside alle thingis in my soule, to kunne, and biholde, and seke wisdom and resoun, and to knowe the wickidnesse of a fool, and the errour of vnprudent men.
26 Nikapata kufahamu kwamba uchungu kuliko kifo, ndivo alivyo mwanamke yeyote ambaye moyo wake umejaa mitego, na nyavu, na ambaye mikono yake ni minyororo. Yeyote ampendezaye Mungu ataponyoka kutoka kwake, lakini mwenye dhambi atachukuliwa naye.
And Y foond a womman bitterere than deth, which is the snare of hunteris, and hir herte is a net, and hir hondis ben boondis; he that plesith God schal ascape hir, but he that is a synnere, schal be takun of hir.
27 “Tafakari kile nilichovumbua,” asema Mwalimu. “Nimekuwa nikiongeza uvumbuzi mmoja hadi mwingine ili kwamba nipate ufafanuzi wa ukweli.
Lo! Y foond this, seide Ecclesiastes, oon and other, that Y schulde fynde resoun, which my soule sekith yit;
28 Hii ndiyo bado natafuta, lakini bado sijapata. Sikupata mwanamme mmoja mwenye haki miongoni mwa elfu, lakini sikupata mwanamke miongoni mwa wale wote.
and Y foond not. I foond o man of a thousynde; Y foond not a womman of alle.
29 Nimegundua hili: kwamba Mungu alimuumba binadamu akiwa mnyoofu, lakini wametoka katika hali ya unyofu wakitafuta magumu mengi.
I foond this oonli, that God made a man riytful; and he medlide hym silf with questiouns with out noumbre. Who is siche as a wijs man? and who knowith the expownyng of a word?