< Mhubiri 2 >
1 Nikasema moyoni, “Njoo, na nitakujaribu kwa kwa furaha. Kwa hiyo furahia.” Lakini tazama, huu nao ulikuwa ni upepo wa muda.
I said I in heart my come! please let me put to [the] test you with pleasure and look on good and there! also it [was] futility.
2 Nikasema juu ya kicheko, “Ni wazimu,” na kuhusu furaha, “Yafaa nini?”
Of laughter I said [it is] folly and of pleasure what? this [is it] doing.
3 Nikajipeleleza moyoni mwangu katika jinsi ya kutimiza hamu yangu kwa mvinyo. Nikaruhusu akili yangu iongozwe na hekima ingawa bado nilikuwa nikishikilia ujinga. Nilitaka kutafuta jambo lililo jema kwa wanadamu kufanya chini ya mbingu wakati wa siku za maisha yao.
I searched in heart my to gratify with wine flesh my and heart my [was] guiding with wisdom and to take hold on folly until that I saw where? this [is] good for [the] children of humankind which they will do under the heavens [the] number of [the] days of lives their.
4 Nilitimiza mambo makubwa. Nilijenga nyumba kwa ajili yangu na kupanda miti ya mizabibu.
I made great works my I built for myself houses I planted for myself vineyards.
5 Nilitengeneza bustani na viwanja; nikapanda aina zote za matunda ndani yake.
I made for myself gardens and parks and I planted in them tree[s] of every fruit.
6 Nikatengeneza mabwawa ya maji ili kumwagilia msitu mahali miti ilikuwa imepandwa.
I made for myself pools of water to water from them a forest sprouting of trees.
7 Nilinunua watumwa wa kiume na wa kiume; nilikuwa na watumwa waliozaliwa katika ikulu yangu. Pia nikawa na makundi makubwa na wanyama wa kufugwa, zaidi ya mfalme yeyote aliyetawala kabla yangu katika Yerusalemu.
I acquired [male] slaves and female slaves and sons of house he belonged to me also livestock herd[s] and flock[s] [surely] a multitude belonged to me more than all who were before me in Jerusalem.
8 Pia nilijikusanyia fedha na dhahabu, hazina ya wafalme na majimbo. Nikapata waimbaji wanaume na wanawake kwa ajili yangu, na kufurahia kutoka kwa wana wa wanadamu, masulia na wanawake.
I gathered for myself also silver and gold and treasure of kings and provinces I acquired for myself male singers and female singers and [the] delights of [the] children of humankind breast and breasts.
9 Hivyo nikawa mkuu na tajiri kuliko wote waliokuwa Yerusalemu kabla yangu, na hekima yangu ilikuwa ndani yangu.
And I became great and I increased more than any who was before me in Jerusalem also wisdom my it remained to me.
10 Lolote ambalo macho yangu yalikitamani sikuyazuia. Sikuuzuia moyo wangu katika furaha yeyote, kwa sababu moyo wangu ulifurahi katika katka kazi yangu zote na furaha ilikuwa ni tunu kwa kazi zangu zote.
And all that they asked eyes my not I withheld from them not I restrained heart my from any pleasure for heart my [was] joyful from all toil my and this it was reward my from all toil my.
11 Kisha nikatazama matendo yote ambayo mikono yangu iliyokwisha kuyatimiliza na juu ya kazi niliyokuwa nimeifanya, lakini tena, kila kitu kilikuwa ni mvuke na kujaribu kuuchunga upepo. Hakukuwa na faida chini ya jua.
And I turned I on all works my that had done hands my and on the toil that I had toiled to do and there! everything [was] futility and striving of wind and there not [was] profit under the sun.
12 Kisha nikageuka kuipambanua hekima, na upumbavu na ujinga. Kwa maana ni kitu gani mfalme anayekuja baada yangu afanye, ambacho hakijafanyika?
And I turned I to consider wisdom and madness and folly for - what? [is] the person who will come after the king [that] which already people have done it.
13 Kisha nikaanza kuelewa kwamba hekima ina faida kuliko upumbavu, kama nuru ilivyo bora kuliko giza.
And I saw I that there [is] advantage of wisdom more than folly like [the] advantage of light more than darkness.
14 Mwenye hekima hutumia macho yake katika kichwa chake kuona mahali anakoenda, lakini mpumbavu hutembea katika giza, ingawa ninafahamu kuwa mwisho wa aina moja umetunzwa kwa kila mmoja.
The wise [person] eyes his [are] in head his and the fool in darkness [is] walking and I knew also I that fate one it will happen to all of them.
15 Kisha nikasema moyoni mwangu, “Kinachotokea kwa mpumbavu, ndicho kitachotokea na kwangu. Hivyo kuna utofauti gani kama mimi ni mwenye hekima sana?” Nikahitimisha moyoni mwangu, “Huu pia ni mvuke tu.”
And I said I in heart my like [the] fate of the fool also me it will happen to me and why? have I become wise I then excessively and I said in heart my that also this [is] futility.
16 Kwa kuwa mwenye hekima, kama mpumbavu, hakumbukwi kwa muda mrefu. Katika siku zijazo, kila kitu kitakuwa kimesahauliwa. Mwenye hekima hufa kama navyokufa mpumbavu.
For there not [is] remembrance of the wise man with the fool for a long time in that already the days coming everything it has been forgotten and how! he will die the wise [person] with the fool.
17 Hivyo nikauchukia uhai kwa sababu kazi zote zilizofanyika chini ya jua zilikuwa mbaya kwangu. Hii ni kwa sababu kila kitu ni mvuke na kujaribu kuuchunga upepo.
And I hated life for [was] evil on me the work that was done under the sun for everything [is] futility and striving of wind.
18 Nikachukia yote niliyoyatimiza, ambayo nilikuwa nimekwisha yafanya chini ya jua kwa sababu ni lazima niyaache kwa mtu anaye kuja baada yangu.
And I hated I all toil my that I [was] a laborer under the sun that I will leave it to the person who will be after me.
19 Na ni nani ajuaye kama atakuwa mwenye hekima au mpumbavu? Ila atakuwa msimamizi juu ya kila kitu chini ya jua ambayo kazi yangu na hekima yangu imeyajenga. Huu pia ni mvuke.
And who? [is] knowing ¿ a wise [person] will he be or? a fool so he may have power over all toil my that I have toiled and that I worked skillfully under the sun also this [is] futility.
20 Kwa hiyo moyo wangu ukaanza kukata tamaa juu ya kazi zote nilizozifanya chini ya jua.
And I turned I to make despair heart my on all the toil that I have toiled under the sun.
21 Kwa kuwa kunaweza kuwa na mtu anayefanya kazi kwa hekima, ufahamu, na umahili, lakini ataacha kila kitu alichonacho kwa mtu ambaye hajafanya chochote. Huu nao ni mvuke na hatari kubwa.
If there [was] a person who toil his [was] with wisdom and with knowledge and with skill and to a person who not he toiled in it he will give it portion his also this [is] futility and an evil great.
22 Kwa maana ni faida gani mtu hupata ambaye hufanya kazi kwa juhudi na kujaribu moyoni mwake kutimiza kazi zake chini ya jua?
For what? [is] becoming to the person in all toil his and in [the] striving of heart his that he [was] a laborer under the sun.
23 Kila siku kazi yake ni maumivu na masikitiko, hivyo wakati wa usiku roho yake haipumziki. Huu pia ni mvuke.
For all days his [are] pains and [is] vexation task his also in the night not it rests heart his also this [is] futility it.
24 Hakuna jambo jema kwa mtu yeyote zaidi ya kula na kunywa na kuridhika na kile kilichochema katika kazi yake. Nikaona kwamba ukweli huu unatoka kutoka mkononi mwa Mungu.
There not [is] good for person that he will eat and he will drink and he will show self his good in toil his also this I have seen I that [is] from [the] hand of God it.
25 Kwa kuwa ni nani anaweza kula au anaweza kupata furaha yoyote tofauti na Mungu?
For who? will he eat and who? will he enjoy outside from me.
26 Kwa kuwa kwa kila anayemfurahisha yeye, Mungu humpa hekimana ufahamu ba furaha. Ingawa, kwa mwenye dhambi humpa kazi ya kukusanya na kutunza ili kwamba ampe mtu anayempendeza Mungu. Huu pia ni sawa na mvuke na kujaribu kuuchunga upepo.
For to anyone who [is] good before him he gives wisdom and knowledge and joy and to the sinner he gives a task to gather and to collect to give [it] to a [person] good before God also this [is] futility and striving of wind.