< Mhubiri 11 >
1 Peleka mkate wako juu ya maji, kwa kuwa utaupata tena baada ya siku nyingi.
Cast thy bread upon the waters, for thou shalt find it after many days.
2 Shiriki mkate na watu saba, hata wanane kwa kuwa haujui ni majanga gani yanayo kuja juu ya nchi.
Divide a portion into seven, yea, even into eight; for thou knowest not what evil shall be upon the earth.
3 Kama mawingu yamejaa mvua, yanajivua yenyewe chini ya nchi. Na kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, popote mti unapoangukia papo hapo utabakia.
If the clouds be full of rain, they empty themselves upon the earth; and if a tree fall in the south, or in the north, in the place where the tree falleth, there shall it be.
4 Yeyote autazamaye upepo yawezekana asipande, na yeyote atazamaye mawingu yawezekana asivune.
He that observeth the wind shall not sow; and he that regardeth the clouds shall not reap.
5 Kama usivyo jua njia ya upepo, wala vile ambavyo mtoto akuavyo tumboni, vivyo hivyo huwezi kuielewa kazi ya Mungu, aliye umba kila kitu.
As thou knowest not what is the way of the wind, nor how the bones do grow in the womb of her that is with child; even so thou knowest not the work of God who doeth all things.
6 Asubuhi panda mbegu yako; hadi jioni, fanya kazi kwa mikono yako kama inavyo hitajika kwa kuwa haujui ni ipi itafanikiwa, jioni au asubuhi, au hii au ile au zote zitakuwa nzuri.
In the morning sow thy seed, and in the evening withhold not thy hand; for thou knowest not which shall prosper, whether this or that, or whether they both shall be alike good.
7 Kweli nuru ni tamu, na ni kitu cha kufurahisha kwa ajili ya macho kuona jua.
And the light is sweet, and a pleasant thing it is for the eyes to behold the sun.
8 Kama mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote, lakina na afikiri juu ya siku zijazo za giza, kwa kuwa zitakuwa nyingi. Kila kitu kijacho ni mvuke unaoteketea.
For if a man live many years, let him rejoice in them all, and remember the days of darkness, for they shall be many. All that cometh is vanity.
9 Furahia kijana, katika ujana wako, na moyo wako ufurahie siku za ujana wako. fuatilia yale mema ya moyo wako, chochote kilicho mbele ya macho yako. Ingawa, fahamu kwamba MUngu atakuleta hukumuni kwa ajili ya vitu hivi vyote.
Rejoice, O young man, in thy youth; and let thy heart cheer thee in the days of thy youth, and walk in the ways of thy heart, and in the sight of thine eyes; but know thou, that for all these things God will bring thee into judgment.
10 Ondoa hasira kutoka moyoni mwako, na usijali maumivu yoyote katika mwili wako, kwa sababu ujana na nguvu zake ni mvuke.
Therefore remove vexation from thy heart, and put away evil from thy flesh; for childhood and youth are vanity.