< Mhubiri 11 >

1 Peleka mkate wako juu ya maji, kwa kuwa utaupata tena baada ya siku nyingi.
Cast your bread over running waters. For, after a long time, you shall find it again.
2 Shiriki mkate na watu saba, hata wanane kwa kuwa haujui ni majanga gani yanayo kuja juu ya nchi.
Give a portion to seven, and indeed even to eight. For you do not know what evil may be upon the earth in the future.
3 Kama mawingu yamejaa mvua, yanajivua yenyewe chini ya nchi. Na kama mti ukianguka kuelekea kusini au kuelekea kaskazini, popote mti unapoangukia papo hapo utabakia.
If the clouds have been filled, they will pour forth rain upon the earth. If a tree falls to the south, or to the north, or to whatever direction it may fall, there it shall remain.
4 Yeyote autazamaye upepo yawezekana asipande, na yeyote atazamaye mawingu yawezekana asivune.
Whoever heeds the wind will not sow. And whoever considers the clouds will never reap.
5 Kama usivyo jua njia ya upepo, wala vile ambavyo mtoto akuavyo tumboni, vivyo hivyo huwezi kuielewa kazi ya Mungu, aliye umba kila kitu.
In the same manner that you do not know the way of the spirit, nor the way that bones are joined together in the womb of a pregnant woman, so you do not know the works of God, who is the Maker of all.
6 Asubuhi panda mbegu yako; hadi jioni, fanya kazi kwa mikono yako kama inavyo hitajika kwa kuwa haujui ni ipi itafanikiwa, jioni au asubuhi, au hii au ile au zote zitakuwa nzuri.
In the morning, sow your seed, and in the evening, do not let your hand cease. For you do not know which of these may rise up, the one or the other. But if both rise up together, so much the better.
7 Kweli nuru ni tamu, na ni kitu cha kufurahisha kwa ajili ya macho kuona jua.
Light is pleasant, and it is delightful for the eyes to see the sun.
8 Kama mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote, lakina na afikiri juu ya siku zijazo za giza, kwa kuwa zitakuwa nyingi. Kila kitu kijacho ni mvuke unaoteketea.
If a man lives for many years, and if he has rejoiced in all of these, he must remember the many days of the dark times, which, when they will have arrived, will accuse the past of vanity.
9 Furahia kijana, katika ujana wako, na moyo wako ufurahie siku za ujana wako. fuatilia yale mema ya moyo wako, chochote kilicho mbele ya macho yako. Ingawa, fahamu kwamba MUngu atakuleta hukumuni kwa ajili ya vitu hivi vyote.
So then, rejoice, O young man, in your youth, and let your heart remain in what is good during the days of your youth. And walk in the ways of your heart, and with the perception of your eyes. And know that, concerning all these things, God will bring you to judgment.
10 Ondoa hasira kutoka moyoni mwako, na usijali maumivu yoyote katika mwili wako, kwa sababu ujana na nguvu zake ni mvuke.
Remove anger from your heart, and set aside evil from your flesh. For youth and pleasure are empty.

< Mhubiri 11 >