< Mhubiri 10 >
1 Kama nzi walio kufa husababisha manukato kutoa harufu ya uozo, hivyo hivyo upumbavu kidogo hushinda hekima na heshima.
Dying flies ruin the sweetness of the ointment. Wisdom and glory is more precious than a brief and limited foolishness.
2 Moyo wa mtu mwenye hekima huelekea kulia, lakini moyo wa mpumbavu huelekea kushoto.
The heart of a wise man is in his right hand, and the heart of a foolish man is in his left hand.
3 Wakati mpumbavu anapotembea barabarani, fikira zake zina upungufu, ikithibitisha kwa kila mtu kwamba ni mpumbavu.
Moreover, as a foolish man is walking along the way, even though he himself is unwise, he considers everyone to be foolish.
4 Kama jaziba za mtawala zikiinuka kinyume na wewe, usiache kazi yako. Utulivu unaweza kutuliza ukatili mkubwa.
If the spirit of one who holds authority rises over you, do not leave your place, because attentiveness will cause the greatest sins to cease.
5 Kuna uovu niliouona chini ya jua, aina ya kosa ambalo huja kutoka kwa mtawala:
There is an evil which I have seen under the sun, proceeding from the presence of a prince, as if by mistake:
6 Wapumbavu wanapewa nafasi za uongozi, wakati watu walio faulu wanapewa nafasi za chini.
a foolish man appointed to a high dignity, and the rich sitting beneath him.
7 Nimewaona watumwa wakipanda farasi, na watu walio faulu wakitembea kama watumwa juu ya ardhi.
I have seen servants on horses, and princes walking on the ground like servants.
8 Yeyote anayechimba shimo anaweza kutumbukia yake, na popote mtu anayevunja ukuja, nyoka anaweza kumuuma.
Whoever digs a pit will fall into it. And whoever tears apart a hedge, a snake will bite him.
9 Yeyote achongaye mwawe, anaweza kuumizwa nayo. Na mtu achongaye mbao, anaweza kujihatarisha kwa hiyo.
Whoever carries away stones will be harmed by them. And whoever cuts down trees will be wounded by them.
10 Kama chuma bapa kisicho na makali, na mtu hainoi, kisha ni lazima atumie nguvu nyingi, lakini hekima hutoa faida kwa ufaulu.
If the iron is dull, and if it was not that way before, but has been made dull by much labor, then it will be sharpened. And wisdom will follow after diligence.
11 Kama nyoka akiuma kabla hajafurahi, hivyo hakuna faida kwa mfurahishaji.
Whoever slanders in secret is nothing less than a snake that bites silently.
12 Maneno ya kinywa cha mtu mwenye hekima yana huruma. Lakini midomo ya mpumbavu humumeza mwenyewe.
Words from the mouth of a wise man are graceful, but the lips of a foolish man will throw him down with violence.
13 Kama maneno yanavyo anza kutiririka mdomoni mwa mpumbavu, ujinga hutoka, na mwisho mdomo wake hutiririka wazimu mbaya.
At the beginning of his words is foolishness, and at the end of his talk is a most grievous error.
14 Mpumbavu huongeza maneno, lakini hakuna ajuaye kinachokuja. Ni nani ajuaye baada yake?
The fool multiplies his words. A man does not know what has been before him, and who is able to reveal to him what will be in the future after him?
15 Jasho la wapumbavu huwavaa wao, hivyo hawajui hata barabara ya kwenda mjini.
The hardship of the foolish will afflict those who do not know to go into the city.
16 Ole wako ardhi kama mfalme wako ni kijana mdogo, na kama viongozi wako huanza karamu ahsubuhi!
Woe to you, the land whose king is a boy, and whose princes consume in the morning.
17 Lakini umebarikiwa ardhi kama mfalme wako ni mwana wa waungwana, na kama vingozi wako hula wakati muafaka, kwa nguvu, na sio kwa ulevi.
Blessed is the land whose king is noble, and whose princes eat at the proper time, for refreshment and not for self-indulgence.
18 Kwa sababu ya uvivu paa huanguka. Na kwa sababu isiyo fanya kazi nyumba hupata ufa.
By laziness, a framework shall be brought down, and by the weakness of hands, a house shall collapse through.
19 Watu huandaa chakula kwa kicheko, divai huleta furaha maishani, na fedha hutimiza hitaji kwa kila kitu.
While laughing, they make bread and wine, so that the living may feast. And all things are obedient to money.
20 Usimlaani mfalme, hata katika akili, na usiwalaani wenye mali katika chumba chako cha kulala. Kwa kuwa ndege wa angani inaweza kuchukua maneno yako. Chochote kilicho na mabawa kinaweza kusambaza jambo.
You should not slander the king, even in your thoughts, and you should not speak evil of a wealthy man, even in your private chamber. For even the birds of the air will carry your voice, and whatever has wings will announce your opinion.