< Mhubiri 1 >

1 Haya ni maneno ya Mwalimu, mwana wa Daudi na mfalme katika Yerusalemu.
The words of the Preacher, the son of David, king in Jerusalem.
2 Mwalimu asema hivi, “Kama mvuke wa ukungu, kama upepo mwanana katika upepo, kila kitu hutoweka na kuacha maswali mengi.
Vanity of vanities, saith the Preacher, vanity of vanities, all is vanity.
3 Ni faida gani wanadamu huipata kutoka katika kazi zote wazifanyazo chini ya jua?
What profit hath a man by all his labor with which he wearieth himself under the sun?
4 Kizazi kimoja huenda, na kizazi kingine huja, lakini nchi yabaki milele.
One generation passeth away, and another generation cometh; while the earth abideth for ever.
5 Jua huchomoza na jua huzama na kwenda kwa kasi, na kurudi mahali linapochomozea tena.
The sun riseth, and the sun goeth down, and hasteneth to the place whence it arose.
6 Upepo huvuma kusini na huzunguka kasikazi, na mara zote ukizunguka katika njia yake na kurudi tena.
The wind goeth toward the south, and turneth about to the north; round and round goeth the wind, and returneth to its circuits.
7 Mito yote hutiririka katika bahari, lakini bahari haijai. Mahali mito inakoenda, ndiko inakoenda tena.
All the rivers run into the sea, yet the sea is not full; to the place whence the rivers come, thither they return.
8 Kila kitu huwa uchovu, na hakuna yeyote awezae kukielezea. Jicho halishibina kile linachokiona, wala sikio halishibi na kile linachosikia.
All words become weary; man cannot express it; the eye is not satisfied with seeing, nor the ear filled with hearing.
9 Chochote kilichopo ndicho kitakachokuwepo, kila kilichofanyika ndicho kitakachofanyika. Hakuna jipya chini ya jua.
The thing that hath been is that which shall be, and that which hath been done is that which shall be done; and there is no new thing under the sun.
10 Je kuna jambo lolote ambalo watu wanaweza kusema, 'Tazama, hili ni jipya'? Chochote kilichopo kimekwisha kuwepo muda mwingi, wakati uliokuwepo kabla yetu.
Is there any thing of which one may say, “Behold, this is new”? It was long ago, in the times which were before us.
11 Hakuna anayeonekana kukumbuka kilichotokea nyakati za zamani. Na mambo yaliyo tokea siku zilizo pita na yale yatakayo tokea siku za mbele nayo hayatakumbukwa.”
There is no remembrance of former things, and of things that are to come there shall be no remembrance to those who live afterwards.
12 Mimi ni mwalimu, na nimekuwa mfalme juu ya Isareli katika Yerusalemu.
I, the Preacher, was king over Israel at Jerusalem.
13 Nilitia akili yangu katika kusoma na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachofanywa chini ya mbingu. Hili nalo ni jukumu zito ambalo Mungu amewapa wana wa watu kujishughulisha nalo.
And I gave my mind to seek and to search out with wisdom concerning all things which are done under heaven; an evil business, which God hath given to the sons of men, in which to employ themselves.
14 Nimeona matendo yote ambayo yanafanyika chini ya jua, na tazama yote ni mvuke ni kujaribu kuuchunga upepo.
I saw all the things which are done under the sun; and, behold, it was all vanity, and striving after wind.
15 Palipopinda hapawezi kunyoshwa! Kisicho kuwepo hakiwezi kuhesabiwa!
That which is crooked cannot be made straight, and that which is wanting cannot be numbered.
16 Nimeuambia moyo wangu nikisema, “Tazama, nimepata hekima kubwa kuliko walioishi Yerusalemu kabla yangu. Akili yangu imeona hekima kubwa na ufahamu.”
I communed with my heart, saying, “Behold, I have gained more and greater wisdom than all who have been before me at Jerusalem; yea, my mind hath seen much wisdom and knowledge.”
17 nimetia moyo wangu kujua hekima na upumbuvu na ujinga. Nikagundua kuwa hili nalo pia lilikuwa ni kujaribu kuuchunga upepo.
And I gave my mind to know wisdom, and to know senselessness and folly; I perceived that this also is striving after wind.
18 Kwa kuwa katika wingi wa hekima kuna masumbufu mengi, naye aongezae ujuzi, aongeza masikitiko.
For in much wisdom is much vexation, and he that increaseth knowledge increaseth sorrow.

< Mhubiri 1 >