< Torati 1 >

1 Haya ni maneno ambayo Musa aliyasema kwa Israeli wote ng'ambo ya jangwa la Yordani, katika tambarare ya mto wa Yordani juu ya Suph, katikati mwa Paran, Topheli, Laban, Hazeroth, na Di Zahab.
Telles sont les paroles que Moïse adressa à tout Israël, de l'autre côté du Jourdain, dans le désert, dans la plaine qui fait face à Souf, entre Paran, Tophel, Laban, Hatséroth et Dizahab.
2 Ni safari ya siku kumi na moja toka Horabu kupitia njia ya mlima wa Seir kwenda Kadeshi Barnea.
Il y a onze jours de voyage depuis Horeb, par le chemin de la montagne de Séir, jusqu'à Kadesh Barnea.
3 Ilitokea kwenye mwaka wa nne, mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, Musa alizungumza kwa watu wa Israeli, kuambia yote yale Yahwe aliyomwamuru kuhusu wao.
La quarantième année, le onzième mois, le premier jour du mois, Moïse parla aux enfants d'Israël, selon tout ce que Yahvé lui avait commandé,
4 Hii ilikuwa baada ya Yahwe kumvamia Sihoni mfalme wa Amoria, ambaye aliishi huko Heshboni, na Ogi mfalme wa Bashani, ambaye aliishi huko Ashtarothi ya Edrei.
après avoir frappé à Édréi Sihon, roi des Amoréens, qui habitait à Heshbon, et Og, roi de Basan, qui habitait à Ashtaroth.
5 Ng'ambo ya Yordani, katika nchi ya Moabu, Musa alianza kutangaza maelekezo haya, akisema,
Au-delà du Jourdain, dans le pays de Moab, Moïse commença à proclamer cette loi, en disant:
6 “Yahwe Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, akisema, umeishi vya kutosha katika milima ya nchi hii.
« Yahvé notre Dieu nous a parlé à Horeb, en disant: Vous avez assez vécu sur cette montagne.
7 Geuka na uanze safari yako, na uende kwenye nchi ya milima ya Amorites, na kwenye maeneo yote karibu na tambarare ya mto Yordani, katika nchi ya milima, na nyanda za chini, huko Negev, na pwani - nchi ya Wakanani na huko Lebanoni mbali ya mto mkuu wa Euphratesi.
Tournez-vous, partez, et allez dans la montagne des Amoréens et dans tous les lieux voisins: dans la plaine, dans la montagne, dans la plaine, dans le midi, au bord de la mer, dans le pays des Cananéens et au Liban, jusqu'au grand fleuve, le fleuve Euphrate.
8 Tazama, nimetenga nchi kwa ajili yako, nenda ndani na umiliki nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kuwapa na uzao wao baada yao.
Voici, j'ai mis le pays devant toi. Allez-y et prenez possession du pays que Yahvé a juré à vos pères - à Abraham, à Isaac et à Jacob - de leur donner, à eux et à leur descendance après eux.'"
9 Nilisema nawe kwa wakati huo, nikisema, siwezi nikakubeba peke yangu,
Je vous ai parlé en ce temps-là, en disant: « Je ne suis pas capable de vous porter moi-même tout seul.
10 Yahwe Mungu wako amekuzidisha, na tazama, leo umekuwa umati wa nyota angani.
L'Éternel, ton Dieu, t'a multiplié, et voici que tu es aujourd'hui comme les étoiles du ciel pour la multitude.
11 Yahwe aweza, Mungu wa baba zako, kukufanya wewe mara elfu moja zaidi ya ulivyo, na kukubariki, kama alivyokuahidi!
Que Yahvé, le Dieu de tes pères, te rende mille fois plus nombreux que toi et te bénisse, comme il te l'a promis!
12 Lakini inawezekanaje mimi peke yangu kubeba shehena zako, mizigo yako, na migogoro yako?
Comment pourrais-je, à moi seul, supporter vos problèmes, vos fardeaux et vos querelles?
13 Chukua wanaume wa hekima, wanaume waelewa, na wanaume walio na sifa nzuri toka kila kabila, nitawafaya kuwa vichwa juu yenu.
Prenez des hommes sages et intelligents, respectés dans vos tribus, et je les établirai à votre tête. »
14 Mlinijibu na kusema, 'Jambo ulilolisema ni zuri kwetu kufanya.'
Tu m'as répondu et tu as dit: « Ce que tu as dit est bon à faire. »
15 Kwa hiyo nilichukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wa hekima, na wanaume wenye sifa nzuri, na nikawafanya kuwa vichwa juu yenu, jemedari kwa elfu, jemedari kwa hamsini, jemedari kwa kumi, na maakida, kabila kwa kabila.
J'ai pris les chefs de vos tribus, des hommes sages et respectés, et je les ai établis chefs sur vous, chefs de milliers, chefs de centaines, chefs de cinquièmes, chefs de dizaines, et officiers, selon vos tribus.
16 Niliwaamuru waamuzi wenu kwa wakati huo, kusema, 'Zikiliza mabishano kati ya ndugu zenu, na muhukumu ya haki kati ya ndugu na ndugu zake, na mgeni aliye pamoja naye.
En ce temps-là, je donnai cet ordre à vos juges: « Entendez les causes entre vos frères et jugez avec équité entre un homme et son frère, et l'étranger qui habite avec lui.
17 Hamtaonesha upendeleo kwa yeyote katika mgogoro, mtasikia madogo na makubwa pia. Hamtaogopa uso wa mtu, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Migogoro iliyo migumu kwenu, mtaniletea mimi, na mimi nitaisikiliza.
Vous ne ferez pas preuve de partialité dans votre jugement; vous entendrez le petit comme le grand. Tu ne craindras pas la face de l'homme, car c'est à Dieu qu'appartient le jugement. Le cas qui est trop difficile pour toi, tu me l'apporteras, et je l'entendrai. »
18 Niliwaamuru kwa wakati huo mambo yote mtakayofanya.
En ce temps-là, je vous commandai toutes les choses que vous deviez faire.
19 Tulisafiri toka Horebu na kwenda kupitia jangwa lile kubwa lote na lenye kutisha lile mliloliona, katika njia yetu kuelekea nchi ya milima huko Amorites, kama Yahwe Mungu wetu alivyotuamuru sisi, na tukaja Kadeshi ya Barnea.
Nous partîmes d'Horeb et traversâmes tout ce grand et terrible désert que tu as vu, en prenant le chemin de la montagne des Amoréens, comme l'avait ordonné l'Éternel, notre Dieu, et nous arrivâmes à Kadès Barnea.
20 Niliwambia, mmekuja kwenye nchi ya milima ya Amorites, ambayo Yahwe Mungu wetu anatupa sisi.
Je vous ai dit: « Vous êtes arrivés à la montagne des Amoréens, que l'Éternel, notre Dieu, nous donne.
21 Tazama, Yahwe Mungu wenu amekwisha weka nchi mbele yenu; nenda juu, muimiliki, kama Yahwe, Mungu wa baba zenu, amekwisha zungumza nanyi, msiogope wala kukata tamaa.
Voici, l'Éternel, votre Dieu, a mis le pays devant vous. Montez, prenez-en possession, comme vous l'a dit Yahvé, le Dieu de vos pères. N'aie pas peur et ne sois pas consterné. »
22 Kila moja wenu alikuja kwangu na kusema, 'Basi tutume watu mbele yetu, ili kwamba waweze kupepeleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea sisi neno kuhusiana na njia ya wapi tuvamie, na kuhusiana na miji tutakayoingia.
Vous vous êtes approchés de moi, chacun d'entre vous, et vous avez dit: « Envoyons des hommes devant nous, afin qu'ils explorent le pays pour nous, et qu'ils nous rapportent le chemin par lequel nous devons monter, et les villes où nous devons arriver. »
23 Shauri hilo lilinibariki mimi, 'Nilichukua watu kumi na mbili kutoka kwenu, mtu moja kwa kila kabila.
La chose m'a plu. Je pris douze de vos hommes, un homme pour chaque tribu.
24 Waligeuka na kwenda juu ya nchi ya milima, kufika kwenye bonde la Eshcol na kufanya upepelezi wa kina.
Ils se retournèrent, montèrent dans la montagne, arrivèrent à la vallée d'Eschcol et l'explorèrent.
25 Walichukua baadhi ya mazao ya ardhi mikononi mwao na kuleta kwetu, Pia walileta neno na kusema, 'Ni nchi nzuri ambayo Yahweh Mungu wetu anatupa sisi'
Ils prirent dans leurs mains une partie des fruits du pays et nous les rapportèrent. Ils nous rapportèrent des nouvelles, et dirent: « C'est un bon pays que l'Éternel, notre Dieu, nous donne. »
26 Bado mlikataa kushambulia, lakini mliasi dhidi ya amri ya Yahwe Mungu wenu.
Pourtant, vous n'avez pas voulu monter, mais vous vous êtes rebellés contre le commandement de l'Éternel, votre Dieu.
27 Mlilalamika katika mahema yenu na kusema, “Ni kwa sababu Yahwe alituchukia sisi kwa kuwa ametutoa katika nchi ya Misri, kuteweka katika mikono ya Amorites kutuangamiza.
Vous murmuriez dans vos tentes, et vous disiez: « Parce que l'Éternel nous haïssait, il nous a fait sortir du pays d'Égypte, pour nous livrer entre les mains des Amoréens et nous faire périr.
28 Tuende wapi sasa? Ndugu zetu wamefanya mioyo yetu kuyeyuka, kusema, Hao watu ni wakubwa na warefu zaidi yetu, miji yao ni mikubwa na imeimarishwa kwenda mbinguni; zaidi ya yote, tumewaona wana wa Anakim huko”
Où allons-nous monter? Nos frères nous ont fait fondre le cœur en disant: 'Le peuple est plus grand et plus fort que nous. Les villes sont grandes et fortifiées jusqu'au ciel. Et nous y avons vu les fils des Anakim ».
29 Kisha nikasema nao, msitishwe wala msiwaogope.
Alors je vous ai dit: « Ne soyez pas terrifiés. N'aie pas peur d'eux.
30 Yahwe Mungu wenu, ambaye aenda mbele yenu, atawapigania, kama yote aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu,
Yahvé ton Dieu, qui marche devant toi, combattra pour toi, selon tout ce qu'il a fait pour toi en Égypte sous tes yeux,
31 na pia katika jangwa, ambapo mmekwisha muona Yahwe Mungu wenu jinsi alivyowabeba, kama mtu abebavyo mtoto wake, kokote mlikoenda mpaka kufika hapa.'
et dans le désert où tu as vu comment Yahvé ton Dieu t'a porté, comme un homme porte son fils, dans tout le chemin que tu as parcouru, jusqu'à ce que tu sois arrivé en ce lieu. »
32 Bado licha ya neno hili hakumwamini Yahwe Mungu wenu,
Mais vous n'avez pas cru en cela Yahvé, votre Dieu,
33 aliyeenda mbele yenu kwenye njia kutafuta eneo kwa ajili yenu kuweka kambi, katika moto kwa usiku, katika mawingu kwa mchana.
qui vous a précédés en chemin pour vous chercher un lieu où dresser vos tentes, la nuit dans le feu pour vous montrer le chemin, le jour dans la nuée.
34 Yahwe alisikia sauti ya maneno yenu na alikasirika; aliapa na kusema,
L'Éternel a entendu la voix de vos paroles, il s'est mis en colère et il a juré, en disant:
35 Hakika hakuna mmoja ya hawa watu wa kizazi hiki kiovu wataona nchi nzuri ambayo niliapa kuwapa babu zao,
Aucun de ces hommes de cette génération mauvaise ne verra le bon pays que j'ai juré de donner à vos pères,
36 kasoro Kalebu mwana wa Jephuneeh; yeye ataiona. Yeye nitampa nchi ambayo amekwisha kuikanyanga, na watoto wake, kwa sababu alimfuata Yahwe kwa ukamilifu.'
excepté Caleb, fils de Jephunné. Il le verra. Je donnerai le pays qu'il a foulé à lui et à ses enfants, parce qu'il a entièrement suivi Yahvé. »
37 Pia Yahweh alinikasirikia mimi kwa sababu yenu, kusema, 'Wewe pia hautaingia huko,
Yahvé s'est mis en colère contre moi à cause de vous, en disant: « Toi non plus, tu n'y entreras pas.
38 Yoshua mwana wa Nuh, ambaye amesimama mbele yako, yeye ataingia, mtie moyo, kwani yeye atawaongoza Israeli kuimiliki.
C'est Josué, fils de Nun, qui se tient devant vous, qui y entrera. Encouragez-le, car c'est lui qui fera hériter Israël.
39 Zaidi ya yote, watoto wenu wadogo, ambao mlisema watakuwa waathirika, ambao leo hawana elimu ya uzuri au ubaya-wataenda ndani huko. Wao nitawapa nchi hiyo, na wataimiliki.
Tes petits enfants, dont tu disais qu'ils seraient capturés ou tués, tes enfants qui aujourd'hui ne savent ni le bien ni le mal, y entreront. Je la leur donnerai, et ils la posséderont.
40 Lakini ninyi, geuka na muuanza safari kwenda jangwani kwa kuambaa njia ya bahari ya mianzi'.
Mais vous, tournez-vous, et partez pour le désert, sur le chemin de la mer Rouge. »
41 Kisha mlinijibu na kusema kwangu, 'Tumetenda dhambi dhidi ya Yahwe, tutaenda juu na kupigana, tutafuata yote ambayo Yahwe Mungu wetu ametuamuru sisi kufanya'. Kila mtu miongoni mwenu aliweka silaha za vita, na mlikuwa tayari kuvamia nchi ya milima.
Alors vous avez répondu et vous m'avez dit: « Nous avons péché contre Yahvé. Nous monterons et nous combattrons, selon tout ce que Yahvé notre Dieu nous a ordonné. » Chacun de vous revêtit ses armes de guerre et se mit à monter dans la montagne.
42 Yahwe alisema nami, 'Waambie, msivamie na kupigana, kwa kuwa sitakuwa pamoja nanyi, na mtashindwa na adui zenu'.
Yahvé me dit: « Dis-leur: « Ne montez pas et ne combattez pas, car je ne suis pas au milieu de vous, de peur que vous ne soyez frappés devant vos ennemis. »"
43 Nilizungumza nanyi kwa njia hii, lakini hamkunisikiliza, Mliasi dhidi ya amri ya Yahwe, mlikuwa wenye kiburi na mlivamia nchi ya milima.
Je vous ai donc parlé, et vous n'avez pas écouté; vous vous êtes rebellés contre le commandement de l'Éternel, vous avez été présomptueux, et vous êtes montés dans la montagne.
44 Lakini Amorites, ambayo waliishi katika nchi hiyo ya milima, walitoka dhidi yenu na kuwafukuza kama nyuki, na kuwapiga chini huko Seir, mbali kama Hormah.
Les Amoréens, qui habitaient cette montagne, sortirent contre vous, vous poursuivirent comme les abeilles, et vous battirent en Séir, jusqu'à Horma.
45 Mlirudi na kulia mbele ya Yahwe; lakini Yahwe hakusikiliza sauti zenu, wala hakuwa makini kwenu.
Vous êtes revenus et vous avez pleuré devant l'Éternel, mais l'Éternel n'a pas écouté votre voix et ne vous a pas prêté l'oreille.
46 Kwa hiyo mlibaki Kadeshi siku nyingi, siku zote mlibaki huko.
Vous restâtes donc à Kadès de nombreux jours, selon les jours où vous êtes restés.

< Torati 1 >