< Torati 9 >

1 Sikiliza, Israeli; umekaribia kuvuka ng'ambo ya pili ya Yordani leo, kuyafukuza mataifa yenye nguvu na ushujaa kuliko ninyi, na miji ambayo ni mikuu na yenye boma iliyoenda juu,
Ecoute, Israël, tu vas passer aujourd'hui le Jourdain, pour entrer chez des nations plus grandes et plus fortes que toi, vers des villes grandes et murées jusqu'au ciel, pour [les] posséder;
2 watu wakuu na warefu, wana wa Anakimu, ambaye mnamjua, na yule mliomsikia watu wakisema, 'Nani atasimama mbele ya wana wa Anak?
Vers un peuple grand et haut; [vers] les enfants des Hanakins, que tu connais, et desquels tu as ouï dire: Qui est-ce qui subsistera devant les enfants de Hanak?
3 Kwa hiyo tambua leo kwamba, Yahwe Mungu wenu ni yeye ambaye huenda mbele yenu kama moto uwalao; atawaharibu na kuwaangamiza mbele yenu, kwa hiyo mtawaondosha na kuwafanya kuwapoteza kwa haraka, kama Yahwe alivyosema kwenu.
Sache donc aujourd'hui que l'Eternel ton Dieu, qui passe devant toi, est un feu consumant. C'est lui qui les détruira, et c'est lui qui les abaissera devant toi; tu les déposséderas, et tu les feras périr subitement comme l'Eternel te l'a dit.
4 Msiseme kwenye mioyo yenu, baada ya Yahwe Mungu wenu kuwatupilia toka mbele yenu, “ilikuwa kwa sababu ya haki yangu kwamba Yahwe amenileta mimi kuimiliki nchi hii; kwa kuwa ilikuwa kwa sababu ya maovu ya mataifa haya kwamba Yahwe anawaondowa toka mbele yenu.
Ne dis point en ton cœur quand l'Eternel ton Dieu les aura chassés de devant toi: C'est à cause de ma justice que l'Eternel m'a fait entrer en ce pays pour le posséder; car c'est à cause de la méchanceté de ces nations-là que l'Eternel les va chasser de devant toi.
5 Si kwa sababu ya uadilifu wenu au unyofu wa mioyo yenu ambayo mnaenda kuingia kumiliki nchi yao, lakini ni kwa sababu ya maovu ya mataifa haya ambayo Mungu anawaondowa kutoka mbele zenu, na kusudi alifanye kuwa kweli neno ambalo aliapa kwa mababu zenu, Ibrahimu, Isaka na Yakabo.
Ce n'est point pour ta justice ni pour la droiture de ton cœur, que tu entres en leur pays pour le posséder; mais c'est pour la méchanceté de ces nations-là, que l'Eternel ton Dieu les va chasser de devant toi; et afin de ratifier la parole que l'Eternel a jurée à tes pères, Abraham, Isaac, et Jacob.
6 Kwa hiyo tambua, kwamba Yahwe Mungu wenu awapi ninyi nchi hii nzuri kuimiliki kwa sababu ya uadilifu wenu kwa kuwa ni watu wakaidi.
Sache donc que ce n'est point pour ta justice, que l'Eternel ton Dieu te donne ce bon pays pour le posséder; car tu [es] un peuple de col roide.
7 Kumbuka na msisahau jinsi mlivyomchochea Yahwe Mungu wenu katika hasira huko jangwani; kutoka siku hiyo ambayo mliacha nchi ya Misri mpaka mlipokuja kwenye eneo hili, mmekuwa waasi dhidi ya Yahwe.
Souviens-toi, [et] n'oublie pas que tu as fort irrité l'Eternel ton Dieu dans ce désert, [et] que depuis le jour que vous êtes sortis du pays d'Egypte, jusqu'à ce que vous êtes arrivés en ce lieu-ci, vous avez été rebelles contre l'Eternel.
8 Pia huko Horebu mlimchochea Yahwe katika hasira, na Yahwe alikasirika vya kutosha kwenu kuwaangamiza.
Même en Horeb vous avez fort irrité l'Eternel; aussi l'Eternel se mit en colère contre vous, pour vous détruire.
9 Wakati nilipoenda juu ya mlima kupokea mbao za mawe, mbao za agano ambalo Yahwe alifanya nanyi, Nilibaki kwenye mlima kwa siku arobaini na usiku arobaini; Wala sikula mkate wala kunywa maji.
Quand je montai en la montagne pour prendre les Tables de pierre, les Tables de l'alliance que l'Eternel avait traitée avec vous, je demeurai en la montagne quarante jours et quarante nuits, sans manger de pain, et sans boire d'eau.
10 Yahwe alinipa mbao mbili za mawe zilizoandikwa kwa kidole chake; juu yake kuliandikwa kila kitu kama tu maneno yote ambayo Yahwe alitangaza kwenu juu ya mlima toka katikati mwa moto siku hiyo ya kusanyiko.
Et l'Eternel me donna deux Tables de pierre, écrites du doigt de Dieu, et ce qui y était écrit c'étaient les paroles que l'Eternel avait toutes proférées lorsqu'il parlait avec vous sur la montagne, du milieu du feu, au jour de l'assemblée.
11 Ilitokea mwishoni mwa siku hizo arobaini na usiku arobaini ya kwamba Yahwe alinipa mimi mbao mbili za mawe, mbao za agano.
Et il arriva qu'au bout de quarante jours et de quarante nuits, l'Eternel me donna les deux Tables de pierre, qui sont les Tables de l'alliance.
12 Yahwe alisema nami, 'Inuka, nenda chini haraka kutokea hapa, kwa kuwa watu wako, ambao uliwaleta toka Misri, wamekuwa wafisadi wenyewe. Kwa haraka wamegeuka toka kwenye njia ambayo niliwaamuru. Wamejifanyia wenyewe umbo la kutupwa.
Puis l'Eternel me dit: Lève-toi, descends en hâte d'ici; car ton peuple que tu as fait sortir d'Egypte, s'est corrompu; ils se sont bien-tôt détournés de la voie que je leur avais commandée, ils se sont fait une image de fonte.
13 Zaidi ya hayo, Yahwe alizungumza na mimi na kusema, “Nimewaona watu hawa; ni watu wakaidi.
L'Eternel me parla aussi, en disant: J'ai regardé ce peuple, et voici; c'est un peuple de col roide.
14 Acha mimi peke yangu, ili kwamba niweze kuwaangamiza na kulifuta jina lao kutoka chini ya mbingu, na nitawafanya ninyi taifa lenye nguvu na kuu kuliko wao.”
Laisse-moi, et je les détruirai, et j'effacerai leur nom de dessous les cieux, mais je te ferai devenir une nation plus puissante et plus grande que celle-ci.
15 Kwa hiyo niligeuka nyuma na kushuka chini ya mlima, na mlima ulikuwa ukiwaka moto. Mbao mbili za agano zilikuwa kwenye mikono yangu.
Je me retirai donc, et je descendis de la montagne. Or la montagne était toute en feu, et j'avais les deux Tables de l'alliance en mes deux mains.
16 Nilitazama, na tazama, mlikuwa mmefanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wenu. Mmejitengenezea wenyewe ndama. Kwa haraka mmegeuka toka njia ambayo Yahwe alikuwa amewaamuru.
Puis je regardai, et voici, vous aviez péché contre l'Eternel votre Dieu, et vous vous étiez fait un veau de fonte; vous vous étiez bien-tôt détournés de la voie que l'Eternel vous avait commandée.
17 Nilizichukua mbao mbili na kuzitupa toka mikononi mwangu. Nilizivunja mbele ya macho yenu.
Alors je saisis les deux Tables, je les jetai de mes deux mains, et je les rompis devant vos yeux.
18 Tena nilala kifudifudi mbele ya Yahwe kwa siku arobaini na usiku arobaini; wala sikula mkate wala kunywa maji, kwa sababu dhambi zenu zote ambazo mlikuwa mmefanya, kwa kufanya hivyo ambavyo ilikuwa ni mbaya machoni pa Yahwe, ili kwamba kumchochea yeye katika hasira.
Puis je me prosternai devant l'Eternel, durant quarante jours et quarante nuits, comme auparavant, sans manger de pain, et sans boire d'eau, à cause de tout votre péché, que vous aviez commis, en faisant ce qui est déplaisant à l'Eternel, afin de l'irriter.
19 Kwa kuwa nilikuwa nimeogopa hasira na gadhabu kali ambayo Yahwe alikuwa amekasirika vya kutosha dhidi yenu kuwaangamiza. Lakini Yahwe alinisikiliza mimi kwa wakati huo pia.
Car je craignais la colère et la fureur dont l'Eternel était enflammé contre vous pour vous détruire; et l'Eternel m'exauça encore cette fois-là.
20 Yahwe alikuwa na hasira nyingi na Aaroni kwa kusudi la kumuangamiza; pia niliomba kwa ajili ya Aaroni kwa wakati huohuo.
L'Eternel fut aussi fort irrité contre Aaron pour le détruire, mais je priai en ce même temps-là aussi pour Aaron.
21 Nilichukua dhambi zenu, ndama mliyekuwa mmentengeza, na kumchoma, kumpiga, kumweka chini kuwa mdogo, mpaka ilipokuwa laini kama vumbi. Nilirusha vumbi lake katika mkondo ambao ulitiririka chini kutoka mlimani.
Puis je pris votre péché que vous aviez fait, [savoir] le veau, et je le brûlai au feu, je le pilai en le broyant bien, jusqu'à ce qu'il fût réduit en poudre, et j'en jetai la poudre au torrent qui descendait de la montagne.
22 Huko Taberah, Massah, na huko Kibrothi Hattaavah, mlimchochea Yahwe kwenye adhabu.
Vous avez aussi fort irrité l'Eternel en Tabhéra et en Massa, et en Kibrothtaava.
23 Wakati Yahwe aliwatoa kutoka Kadeshi ya Barnea na kusema, 'Nenda juu na umiliki nchi ambayo nimekupa, 'ndipo mliasi dhidi ya agizo la Yahwe Mungu wenu, na hamkumwamini na kumsikiliza sauti yake.
Et quand l'Eternel vous envoya de Kadès-barné, en disant: Montez, et possédez le pays que je vous ai donné, alors vous vous rebellâtes contre le commandement de l'Eternel votre Dieu, vous ne le crûtes point, et vous n'obéîtes point à sa voix.
24 Mmekuwa waasi dhidi ya Yahwe toka siku ile nilipowajua.
Vous avez été rebelles à l'Eternel dès le jour que je vous ai connus.
25 Kwa hiyo nilala kifudifudi mbele ya Yahwe siku zile arobaini na usiku arobaini, kwa sababu alikuwa amesema kwamba angewaangamiza.
Je me prosternai donc devant l'Eternel durant quarante jours et quarante nuits, durant lesquels je me prosternai, parce que l'Eternel avait dit qu'il vous détruirait.
26 Niliomba kwa Yahwe na kusema, 'Oh Bwana Yahwe, usiwaangamize watu wako au warithi wako ambao uliwaokoa kwa ukuu wako, ambapo uwatoa toka Misri kwa mkono wa uweza.
Et je priai l'Eternel, et je lui dis: Ô Seigneur Eternel! ne détruis point ton peuple, et ton héritage que tu as racheté par ta grandeur, [et] que tu as retiré d'Egypte, à main forte.
27 Akilini waite watumishi wenu Ibrahimu, Isaka, na Yakobo; msiangalie ukaidi wa watu hawa, wala maovu yao, dhambi zao,
Souviens-toi de tes serviteurs Abraham, Isaac, et Jacob; ne regarde point à la dureté de ce peuple, ni a sa méchanceté, ni à son péché;
28 ili kwamba nchi ambayo ulitutoa iseme, “Kwa sababu Yahwe hakuweza kuwaleta katika nchi aliyowaahadia, na kwa sababu aliwachukia, amewaleta nje kuwauwa katika jangwa.
De peur que les habitants du pays, dont tu nous as fait sortir, ne disent: Parce que l'Eternel ne les pouvait pas faire entrer au pays dont il leur avait parlé, et parce qu'il les haïssait, il les a fait sortir [d'Egypte] pour les faire mourir en ce désert.
29 Bado ni watu wa kwenu na urithi wenu, ambao uliwatoa kwa nguvu zako kuu na kwa kuonesha mamlaka yako,
Cependant ils sont ton peuple et ton héritage, que tu as tirés [d'Egypte] par ta grande puissance, et à bras étendu.

< Torati 9 >