< Torati 9 >

1 Sikiliza, Israeli; umekaribia kuvuka ng'ambo ya pili ya Yordani leo, kuyafukuza mataifa yenye nguvu na ushujaa kuliko ninyi, na miji ambayo ni mikuu na yenye boma iliyoenda juu,
“Hear, O Israel: You are passing over the Jordan today to go in to possess nations greater and mightier than yourself, cities great and fortified up to the heavens,
2 watu wakuu na warefu, wana wa Anakimu, ambaye mnamjua, na yule mliomsikia watu wakisema, 'Nani atasimama mbele ya wana wa Anak?
a people great and tall, sons of Anakim, whom you have known, and [of whom] you have heard: Who stations himself before sons of Anak?
3 Kwa hiyo tambua leo kwamba, Yahwe Mungu wenu ni yeye ambaye huenda mbele yenu kama moto uwalao; atawaharibu na kuwaangamiza mbele yenu, kwa hiyo mtawaondosha na kuwafanya kuwapoteza kwa haraka, kama Yahwe alivyosema kwenu.
And you have known today that your God YHWH [is] He who is passing over before you [as] a consuming fire; He destroys them, and He humbles them before you, and you have dispossessed them, and destroyed them quickly, as YHWH has spoken to you.
4 Msiseme kwenye mioyo yenu, baada ya Yahwe Mungu wenu kuwatupilia toka mbele yenu, “ilikuwa kwa sababu ya haki yangu kwamba Yahwe amenileta mimi kuimiliki nchi hii; kwa kuwa ilikuwa kwa sababu ya maovu ya mataifa haya kwamba Yahwe anawaondowa toka mbele yenu.
You do not speak in your heart (in your God YHWH’s driving them away from before you), saying, In my righteousness YHWH has brought me in to possess this land; but in YHWH dispossessing these nations from your presence, [it is because of] their being wicked.
5 Si kwa sababu ya uadilifu wenu au unyofu wa mioyo yenu ambayo mnaenda kuingia kumiliki nchi yao, lakini ni kwa sababu ya maovu ya mataifa haya ambayo Mungu anawaondowa kutoka mbele zenu, na kusudi alifanye kuwa kweli neno ambalo aliapa kwa mababu zenu, Ibrahimu, Isaka na Yakabo.
[It is] not in your righteousness and in the uprightness of your heart [that] you are going in to possess their land, but in YHWH dispossessing these nations from your presence, [it is because of] their being wicked, and in order to establish the word which YHWH has sworn to your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob;
6 Kwa hiyo tambua, kwamba Yahwe Mungu wenu awapi ninyi nchi hii nzuri kuimiliki kwa sababu ya uadilifu wenu kwa kuwa ni watu wakaidi.
and you have known that [it is] not in your righteousness [that] your God YHWH is giving this good land to you to possess it, for you [are] a people stiff of neck.
7 Kumbuka na msisahau jinsi mlivyomchochea Yahwe Mungu wenu katika hasira huko jangwani; kutoka siku hiyo ambayo mliacha nchi ya Misri mpaka mlipokuja kwenye eneo hili, mmekuwa waasi dhidi ya Yahwe.
Remember [and] do not forget that [with] which you have made your God YHWH angry in the wilderness; from the day that you have come out of the land of Egypt until your coming to this place, you have been rebellious against YHWH;
8 Pia huko Horebu mlimchochea Yahwe katika hasira, na Yahwe alikasirika vya kutosha kwenu kuwaangamiza.
even in Horeb you have made YHWH angry, and YHWH shows Himself angry against you—to destroy you.
9 Wakati nilipoenda juu ya mlima kupokea mbao za mawe, mbao za agano ambalo Yahwe alifanya nanyi, Nilibaki kwenye mlima kwa siku arobaini na usiku arobaini; Wala sikula mkate wala kunywa maji.
In my going up into the mountain to receive the tablets of stone (tablets of the covenant which YHWH has made with you), then I abide on the mountain forty days and forty nights; I have not eaten bread and I have not drunk water;
10 Yahwe alinipa mbao mbili za mawe zilizoandikwa kwa kidole chake; juu yake kuliandikwa kila kitu kama tu maneno yote ambayo Yahwe alitangaza kwenu juu ya mlima toka katikati mwa moto siku hiyo ya kusanyiko.
and YHWH gives to me the two tablets of stone written with the finger of God, and on them [is] according to all the words which YHWH has spoken with you on the mountain, out of the midst of the fire, in the day of the assembly.
11 Ilitokea mwishoni mwa siku hizo arobaini na usiku arobaini ya kwamba Yahwe alinipa mimi mbao mbili za mawe, mbao za agano.
And it comes to pass, at the end of forty days and forty nights, YHWH has given the two tablets of stone to me—tablets of the covenant.
12 Yahwe alisema nami, 'Inuka, nenda chini haraka kutokea hapa, kwa kuwa watu wako, ambao uliwaleta toka Misri, wamekuwa wafisadi wenyewe. Kwa haraka wamegeuka toka kwenye njia ambayo niliwaamuru. Wamejifanyia wenyewe umbo la kutupwa.
Then YHWH says to me, Rise, go down, hurry from here, for your people whom you have brought out of Egypt have done corruptly; they have quickly turned aside from the way which I have commanded them—they have made a molten thing for themselves!
13 Zaidi ya hayo, Yahwe alizungumza na mimi na kusema, “Nimewaona watu hawa; ni watu wakaidi.
And YHWH speaks to me, saying, I have seen this people, and behold, it [is] a people stiff of neck.
14 Acha mimi peke yangu, ili kwamba niweze kuwaangamiza na kulifuta jina lao kutoka chini ya mbingu, na nitawafanya ninyi taifa lenye nguvu na kuu kuliko wao.”
Desist from Me, and I destroy them, and blot out their name from under the heavens, and I make you become a nation more mighty and numerous than it.
15 Kwa hiyo niligeuka nyuma na kushuka chini ya mlima, na mlima ulikuwa ukiwaka moto. Mbao mbili za agano zilikuwa kwenye mikono yangu.
And I turn and come down from the mountain, and the mountain is burning with fire, and the two tablets of the covenant [are] on my two hands,
16 Nilitazama, na tazama, mlikuwa mmefanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wenu. Mmejitengenezea wenyewe ndama. Kwa haraka mmegeuka toka njia ambayo Yahwe alikuwa amewaamuru.
and I see, and behold, you have sinned against your God YHWH; you have made a molten calf for yourselves; you have quickly turned aside from the way which YHWH has commanded you.
17 Nilizichukua mbao mbili na kuzitupa toka mikononi mwangu. Nilizivunja mbele ya macho yenu.
And I lay hold on the two tablets, and cast them out of my two hands, and break them before your eyes,
18 Tena nilala kifudifudi mbele ya Yahwe kwa siku arobaini na usiku arobaini; wala sikula mkate wala kunywa maji, kwa sababu dhambi zenu zote ambazo mlikuwa mmefanya, kwa kufanya hivyo ambavyo ilikuwa ni mbaya machoni pa Yahwe, ili kwamba kumchochea yeye katika hasira.
and I throw myself before YHWH, as at first, [for] forty days and forty nights; I have not eaten bread and I have not drunk water, because of all your sins which you have sinned by doing evil in the eyes of YHWH, to make Him angry.
19 Kwa kuwa nilikuwa nimeogopa hasira na gadhabu kali ambayo Yahwe alikuwa amekasirika vya kutosha dhidi yenu kuwaangamiza. Lakini Yahwe alinisikiliza mimi kwa wakati huo pia.
For I have been afraid because of the anger and the fury with which YHWH has been angry against you, to destroy you; and YHWH also listens to me at this time.
20 Yahwe alikuwa na hasira nyingi na Aaroni kwa kusudi la kumuangamiza; pia niliomba kwa ajili ya Aaroni kwa wakati huohuo.
And YHWH has showed Himself very angry with Aaron, to destroy him, and I also pray for Aaron at that time.
21 Nilichukua dhambi zenu, ndama mliyekuwa mmentengeza, na kumchoma, kumpiga, kumweka chini kuwa mdogo, mpaka ilipokuwa laini kama vumbi. Nilirusha vumbi lake katika mkondo ambao ulitiririka chini kutoka mlimani.
And I have taken your sin, the calf which you have made, and I burn it with fire, and beat it, grinding well until it [is] small as dust, and I cast its dust into the brook which is going down out of the mountain.
22 Huko Taberah, Massah, na huko Kibrothi Hattaavah, mlimchochea Yahwe kwenye adhabu.
And in Taberah, and in Massah, and in Kibroth-Hattaavah, you have been making YHWH angry;
23 Wakati Yahwe aliwatoa kutoka Kadeshi ya Barnea na kusema, 'Nenda juu na umiliki nchi ambayo nimekupa, 'ndipo mliasi dhidi ya agizo la Yahwe Mungu wenu, na hamkumwamini na kumsikiliza sauti yake.
also in YHWH’s sending you from Kadesh-Barnea, saying, Go up and possess the land which I have given to you; then you provoke the mouth of your God YHWH, and have not given credence to Him, nor listened to His voice.
24 Mmekuwa waasi dhidi ya Yahwe toka siku ile nilipowajua.
You have been rebellious against YHWH from the day of my knowing you.
25 Kwa hiyo nilala kifudifudi mbele ya Yahwe siku zile arobaini na usiku arobaini, kwa sababu alikuwa amesema kwamba angewaangamiza.
And I throw myself before YHWH—the forty days and the forty nights when I had thrown myself—because YHWH has commanded to destroy you;
26 Niliomba kwa Yahwe na kusema, 'Oh Bwana Yahwe, usiwaangamize watu wako au warithi wako ambao uliwaokoa kwa ukuu wako, ambapo uwatoa toka Misri kwa mkono wa uweza.
and I pray to YHWH, and say, Lord YHWH, do not destroy Your people and Your inheritance whom You have ransomed in Your greatness, whom You have brought out of Egypt with a strong hand;
27 Akilini waite watumishi wenu Ibrahimu, Isaka, na Yakobo; msiangalie ukaidi wa watu hawa, wala maovu yao, dhambi zao,
be mindful of Your servants, of Abraham, of Isaac, and of Jacob; do not turn to the stiffness of this people, and to its wickedness, and to its sin,
28 ili kwamba nchi ambayo ulitutoa iseme, “Kwa sababu Yahwe hakuweza kuwaleta katika nchi aliyowaahadia, na kwa sababu aliwachukia, amewaleta nje kuwauwa katika jangwa.
lest the land from which You have brought us out says, Because of YHWH’s want of ability to bring them into the land of which He has spoken to them, and because of His hating them, He brought them out to put them to death in the wilderness.
29 Bado ni watu wa kwenu na urithi wenu, ambao uliwatoa kwa nguvu zako kuu na kwa kuonesha mamlaka yako,
And they [are] Your people and Your inheritance, whom You have brought out by Your great power and by Your outstretched arm!”

< Torati 9 >