< Torati 8 >
1 Mnapaswa kuyashika maagizo yote ninayowapa leo, ili kwamba mweze kuishi na kuongezeka, na kuingia na kuimiliki nchi ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu.
Take care to keep all the orders which I give you today, so that you may have life and be increased and go in and take as a heritage the land which the Lord, by his oath to your fathers, undertook to give you.
2 Mtakumbuka akilini njia zote ambazo Yahwe Mungu amewaongoza miaka hii arobaini kwenye jangwa, ili kwamba apate kuwanyenyekeza, ili kwamba awajaribu kujua nini kilikuwa ndani ya mioyo yenu, kama mungeweza kuyashika maagizo yake au hapana.
And keep in mind the way by which the Lord your God has taken you through the waste land these forty years, so that he might make low your pride and put you to the test, to see what was in your heart and if you would keep his orders or not.
3 Aliwanyenyekeza, na kuwafanya kuwa na njaa, na kuwalisha manna, ambayo hamkuijua na ambayo baba zenu hawakuijua. Alifanya hivyo kuwafanya nyie kujua si kwa mkate tu watu wanaishi, badala ni kwa chochote hutoka kwenye kinywa cha Yahwe kwamba watu wanaishi.
And he made low your pride and let you be without food and gave you manna for your food, a thing new to you, which your fathers never saw; so that he might make it clear to you that bread is not man's only need, but his life is in every word which comes out of the mouth of the Lord.
4 Mavazi yenu hayakuchanika na kudondoka, na miguu yenu haikuvimba kipindi cha miaka hiyo arobaini.
Through all these forty years your clothing did not get old or your feet become tired.
5 Mtatafakari katika mioyo yenu kuhusu, namna, kama mtu anavyo mwadibisha kijana wake, hivyo Yahwe Mungu wenu anawadibisha ninyi.
Keep in mind this thought, that as a son is trained by his father, so you have been trained by the Lord your God.
6 Mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, ili kwamba mweze kutembea katika njia zake na kumheshimu.
Then keep the orders of the Lord your God, fearing him and walking in his ways.
7 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi ya vijito vya maji, visima na chemchemi, vitiririkavyo kwenda kwenye mabonde na miongoni mwa milima,
For the Lord your God is guiding you into a good land, a land of water-springs, of fountains, and deep streams flowing out from the valleys and the hills;
8 nchi ya ngano na shayiri, mizabibu, mtini, na komamanga; nchi mizeituni na asali.
A land of grain and vines and fig-trees and fair fruits; a land of oil-giving olive-trees and honey;
9 Ni nchi ambayo mtakula mkate bila kupungukiwa, na ambapo mtaenda bila chochote; nchi ambayo mawe yametengenezwa kwa chuma, na kutokana na milima mtaweze kuchimba shaba.
Where there will be bread for you in full measure and you will be in need of nothing; a land where the very stones are iron and from whose hills you may get copper.
10 Mtakula na kushiba, na mtambariki Yahwe Mungu wenu kwa nchi nzuri ambayo amewapa.
And you will have food enough and be full, praising the Lord your God for the good land he has given you.
11 Iweni makini kwamba msimsahau Yahwe Mungu wenu, na kwamba msipuuzie maagizo yake, hukumu zake, na sheria zake ambazo ninakuamuru leo,
Then take care that you are not turned away from the Lord your God and from keeping his orders and decisions and laws which I give you this day:
12 vinginenyo unapokula na ukashiba, na wakati unajenga nyumba nzuri na kuishi ndani zao.
And when you have taken food and are full, and have made fair houses for yourselves and are living in them;
13 Na muwe makini wakati makundi yenu na mifugo yenu ikiongezeka, na wakati wa fedha zenu na dhahabu zenu zikiongezeka, na vyote mlivyonavyo kuongezeka,
And when your herds and your flocks are increased, and your stores of silver and gold, and you have wealth of every sort;
14 basi kwamba mioyo yenu iliniuliza juu ya kumsahau Yahwe Mungu wenu-aliyewaleta kutoka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
Take care that your hearts are not lifted up in pride, giving no thought to the Lord your God who took you out of the land of Egypt, out of the prison-house;
15 Usimsahau yeye aliyewaongoza kupitia jangwa kuu na la kutisha, ambako ndani yake kulikuwa na nyoka wa moto na nge, na pitia nchi yenye kiu ambako hapakuwa na maji, ambaye yeye alileta maji toka kwenye mwamba wa jiwe.
Who was your guide through that great and cruel waste, where there were poison-snakes and scorpions and a dry land without water; who made water come out of the hard rock for you;
16 Ambaye aliwalisha kwenye jangwa kwa manna ambayo mababu zenu hawakuijua, ili kwamba awajaribu, kufanya uzuri kwenu mwishoni-
Who gave you manna for your food in the waste land, a food which your fathers had never seen; so that your pride might be broken and your hearts tested for your good in the end;
17 lakini mnaweza kusema mioyoni mwenu, Nguvu yangu na mkono wangu wa uweza umepata utajiri huu wote.
Say not then, in your hearts, My power and the strength of my hands have got me this wealth.
18 Lakini mtamkumbuka akilini Yahwe Mungu wenu, kwa kuwa ni yeye awapae ninyi nguvu ya kupata utajiri, ili kwamba aweze kuanzisha agano lake aliloapa kwa baba zenu, kama ilivyo leo.
But keep in mind the Lord your God: for it is he who gives you the power to get wealth, so that he may give effect to the agreement which he made by his oath with your fathers, as at this day.
19 Itakuwa kwamba, kama mtamsahau Yahwe Mungu wenu na kuwaendea miungu mingine, kuibudu, na kuiheshimu, nashuhudia kinyume dhidi yenu leo kwamba mtateketea.
And it is certain that if at any time you are turned away from the Lord your God, and go after other gods, to be their servants and to give them worship, destruction will overtake you.
20 Kama mataifa ambayo Yahwe anatengeneza kuyaangamiza mbele yenu, hivyo mtaangamia, kwa sababu hamkusikiliza sauti ya Yahwe Mungu wenu.
Like the nations which the Lord is cutting off before you, so you will be cut off; because you would not give ear to the voice of the Lord your God.