< Torati 7 >

1 Wakati Yahwe Mungu wenu atuleta katika nchi ambayo mnaenda kuimiliki na kuwaondoa mataifa mengi mbele zenu- Mhiti, Mgirgashi na Mwamori, na Mkanaani, na Mperizi, Mhivi, Myebusi- mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko wewe.
If he will bring you Yahweh God your into the land where you [are] about to go there towards to take possession of it and he will clear away nations many - from before you the Hittite[s] and the Girgashite[s] and the Amorite[s] and the Canaanite[s] and the Perizzite[s] and the Hivite[s] and the Jebusite[s] seven nations great and mighty more than you.
2 Na wakati Yahwe Mungu wenu awapa ninyi ushindi juu yao pindi mnakutana nao katika vita, mtawashambulia, basi mnapaswa kuwateketeza kabisa. Hamtafanya agano nao, wala kuonesha huruma kwao.
And he will deliver up them Yahweh God your before you and you will strike down them certainly you will totally destroy them not you will make to them a covenant and not you will show favor to them.
3 Wala hamtapanga ndoa zozote pamoja nao, hamtawatoa binti zenu kwa vijana wao, na hamtawachukua binti zao kwa vijana wenu.
And not you will intermarry with them daughter your not you will give to son his and daughter his not you will take for son your.
4 Kwa kuwa watawabadilisha vijana wenu kutonifuata mimi, ili kwamba waweze kuabudu miungu yao. Kwa hiyo hasira ya Yahwe itawashwa dhidi yenu na atawaangamiza haraka.
For he will turn aside son your from after me and they will serve gods other and it will burn [the] anger of Yahweh on you and he will destroy you quickly.
5 Hivi ndivyo mtakavyo washughulikia nao; mtavunja madhabahu zao, vunja nguzo zao za mawe katika vipande, kata chini ncha za Asherahi, na kuzichoma sanamu za kutupwa.
That except thus you will do to them altars their you will break down and sacred pillars their you will shatter and Asherah poles their you will cut down! and images their you will burn! with fire.
6 Kwa kuwa wewe ni taifa uliyetengwa kwa Yahwe Mungu wako. Amekuchagua wewe kuwa watu kwa ajili yake kumiliki, zaidi ya watu wengine wote ambao wako katika uso wa dunia.
For [are] a people holy you to Yahweh God your you he has chosen - Yahweh God your to become for him a people of possession from all the peoples which [are] on [the] surface of the ground.
7 Yahwe hakuweka upendo wake juu yenu au kuwachagua kwa sababu mlikuwa zaidi katika idadi kuliko watu wowote, kwa kuwa mlikuwa wachache kuliko watu wote-
Not because were numerous you more than all the peoples he loved Yahweh you and he chose you for you [were] the few from all the peoples.
8 Lakini kwa sababu anawapenda ninyi, anataka kushika kiapo alichoapa kwa baba zenu. Huyu ni Yahwe aliyewatoa kwa mkono wa uweza na kuwakomboa kutoka nyumba ya utumwa, kutoka mkono wa Farao, mfalme wa Misri.
For from [the] love of Yahweh you (and because kept he *L(abh)*) the oath which he swore to ancestors your he brought out Yahweh you by a hand strong and he redeemed you from a house of slaves from [the] hand of Pharaoh [the] king of Egypt.
9 Kwa hiyo tambua ya kuwa Yahwe Mungu wako-ni Mungu, Mungu mwaminifu, anayetunza maagano na uaminifu kwa vizazi elfu kwa wale wanaompenda na kuyashika maagizo yake,
And you will know that Yahweh God your he [is] God the God faithful [who] keeps the covenant and covenant loyalty to [those who] love him and to [those who] keep (commandments his *Q(K)*) to a thousand generation[s].
10 lakini huwalipa wale wanaomchukia kwa sura zao, kuwaangamiza, hatakuwa na huruma kwa yeyote anayemchukia; atamlipa kwa uso wake.
And [who] repays to [those who] hate him to face his by destroying him not he delays to [the] [one who] hates him to face his he repays to him.
11 Kwa hiyo utashika maagizo, amri, na sheria ninazokuamuru leo, ili kwamba uzifanye.
And you will keep the commandment and the statutes and the judgments which I [am] commanding you this day to observe them.
12 Kama mtasikiliza maagizo haya, kuyashika na kuyafanya, itakuwa Yahwe Mungu wenu atawashika pamoja na agano na uaminifu ambao aliapa kwa baba zenu.
And it will be - consequence you will hear! the judgments these and you will take care and you will observe them and he will keep Yahweh God your to you the covenant and covenant loyalty which he swore to ancestors your.
13 Atawapenda, atawabariki, na kuwazidisha, pia atabariki tunda la miili yenu na tunda la ardhi yenu, nafaka zenu, divai mpya, mafuta yenu, atazidisha mifugo na kundi lako la mifugo michanga, katika nchi ambayo aliapa kwa baba zenu kuwapa.
And he will love you and he will bless you and he will increase you and he will bless [the] fruit of womb your and [the] fruit of ground your grain your and new wine your and fresh oil your [the] young of cattle your and [the] young ones of flock your on the land which he swore to ancestors your to give to you.
14 Mtabarikiwa zaidi kuliko watu wengine wote; hapatakuwa na mwanaume asiyekuwa na mtoto au mwanamke tasa miongoni mwenu au miongoni mwa mifugo.
Blessed you will be more than all the peoples not he will be among you a sterile [male] and a barren [female] and among livestock your.
15 Yahwe atawaondolea magonjwa yote; hakuna magonjwa mabaya ya Misri ambayo mnayajua yatawekwa juu yenu, Lakini atayaweka kwa wote wanaowachukia ninyi.
And he will remove Yahweh from you every sickness and all [the] diseases of Egypt harmful which you experienced not he will put them on you and he will set them on all [those who] hate you.
16 Mtayaondoa makundi ya watu wote ambayo Yahwe Mungu wenu awapa ushindi, na jicho lenu halitawaonea huruma. Na hamtaabudu miungu yao, kwa kuwa huo utakuwa mtego kwenu.
And you will consume all the peoples which Yahweh God your [is] about to deliver up to you not it will look with pity eye your on them and not you will serve gods their for [will be] a snare it to you.
17 Kama mtasema kwenye mioyo, Haya mataifa ni mengi zaidi kuliko mimi; nitawezaje kuwafukuza?
For you will say in heart your [are] great the nations these more than I how? will I be able to dispossess them.
18 Usiwaogope; utakumbuka akilini Yahwe nini Mungu wenu alifanya kwa Farao na Misri yote?
Not you must be afraid from them carefully you will remember [that] which he did Yahweh God your to Pharaoh and to all Egypt.
19 Mateso makuu ambayo macho yenu yaliona, ishara, maajabu, mkono wa uweza, mkono ulionyoshwa ambao Yahwe Mungu wenu alivyowatoa. Yahwe Mungu wenu atafanya kile kile kwa watu wote ambao mnawaogopa.
The trials great which they saw eyes your and the signs and the wonders and the hand mighty and the arm outstretched which he brought out you Yahweh God your thus he will do Yahweh God your to all the peoples which you [are] afraid of them.
20 Zaidi ya yote, Yahwe Mungu wenu atatuma nyigu miongoni mwao, mpaka wale waliobaki na wale wanaojificha wenyewe mbele yenu waangamizwa mbele ya uwepo wenu.
And also the hornet he will send Yahweh God your among them until perish [those] who remain and [those] who hide themselves from before you.
21 Hamtatishikeni nao, kwa kuwa Yahwe Mungu wenu yuko miongoni mwenu, Mungu mkuu na wa kuogofya.
Not you must be terrified of them for Yahweh God your [is] in midst your a God great and awesome.
22 Yahwe Mungu wenu atayaondoa mataifa mbele zenu kidogo kidogo. Hamtayashinda yote kwa wakati mmoja, au wanyama wa mwitu watakuwa wengi karibu yenu.
And he will clear away Yahweh God your the nations these from before you little little not you will be able to make an end of them quickly lest it should increase with you [the] animal[s] of the field.
23 Lakini Yahwe Mungu wenu atawapa ninyi ushindi dhidi yao wakati mkutanapo vitani; atawachanganya kwa kiasi kikubwa mpaka wameangamizwa.
And he will deliver up them Yahweh God your before you and he will confuse them confusion great until are destroyed they.
24 Atawaweka wafalme wao chini ya utawala wenu, na mtafanya jina lao kuangamia toka chini ya mbingu. Hakuna atakayeweza kusimama mbele yenu, mpaka muwaangamize.
And he will give kings their in hand your and you will destroy name their from under the heavens not he will stand anyone in face your until destroying you them.
25 Utazichoma sanamu za kuchonga za miungu yao- usitamani madini ya fedha au dhahabu yanayofunika na kuichukua kwa ajili yenu, kwa sababu mkifanya, mtanaswa nayo-kwa kuwa ni chukizo kwa Yahwe Mungu wenu.
[the] images of Gods their you will burn! with fire not you will covet silver and gold on them and you will take [it] for yourself lest you should be ensnared by it for [is] [the] abomination of Yahweh God your that.
26 Hamtaleta chukizo lolote ndani ya nyumba zenu na kuanza kuiabudu. Mtachukizwa kabisa na kuchukia kwa kuwa imetengwa kwa ajili ya uharibifu.
And not you will bring an abomination into house your and you will be an object for destruction like it utterly - you will detest it and utterly - you will abhor it for [is] an object for destruction it.

< Torati 7 >