< Torati 6 >
1 Sasa haya ni maagizo, amri, na sheria ambazo Yahwe Mungu wetu ameniamuru mimi kuwafundisha ninyi, ili kwamba muweze kuzishika katika nchi ambayo mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani kumiliki,
(And this *L(P)*) [is] the commandment the statutes and the judgments which he has commanded Yahweh God your to teach you to observe in the land where you [are] about to pass over there towards to take possession of it.
2 ili kwamba mpate kumheshimu Yahwe wenu, ili muzishike amri zake zote na maagizo ninayowaamuru-ninyi, wana wenu na wana wa wana wenu, siku zenu zote za maisha, ili kwamba siku zenu ziongezeke.
So that you may fear Yahweh God your to keep all statutes his and commandments his which I [am] commanding you you and child your and [the] child of child your all [the] days of life your and so that they may grow long! days your.
3 Kwa hiyo wasikilizeni, Israeli, na kuzishika ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu, ili kusudi muweze kuzidi mno kwenye nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Yahwe Mungu wa Baba zenu, amewaahidi atafanya.
And you will hear O Israel and you will take care to observe [them] that it will go well for you and that you will increase! exceedingly just as he spoke Yahweh [the] God of ancestors your to you a land flowing of milk and honey.
4 Sikiliza, Israel: Yahwe Mungu wetu ni mmoja.
Hear O Israel Yahweh God our Yahweh - [is] one.
5 Mtampenda Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote, kwa roho zenu zote, na kwa akili zenu zote.
And you will love Yahweh God your with all heart your and with all being your and with all strength your.
6 Maneno ninayowaamuru ninyi leo yatakuwa katika moyo wenu;
And they will be the words these which I [am] commanding you this day on heart your.
7 na mtayafundisha kwa bidii kwa watoto wenu, mtayazungumza wakati mkaapo katika nyumba zenu, wakati mlalapo, na wakati mwinukapo.
And you will repeat them to children your and you will speak in them when sitting you in house your and when walking you on the road and when lying down you and when rising up you.
8 Utazifunga kama ishara juu ya mkono wako, nayo yatakuwa utepe kati ya macho yako.
And you will tie them for a sign on hand your and they will be for marks between eyes your.
9 Utaziandika kwenye miimo ya mlango ya nyumba yako na kwenye malango.
And you will write them on [the] doorposts of house your and on gates your.
10 Wakati Yahwe Mungu wako akuleta kwenye nchi ambayo aliaapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwamba angekupa, pamoja na miji mikubwa na mizuri ambayo hamkuijenga,
And it will be that he will bring you - Yahweh God your into the land which he swore to ancestors your to Abraham to Isaac and to Jacob to give to you cities large and good which not you built.
11 na nyumba zilizojaa kila aina ya vitu vizuri ambavyo hamkuzifanya, visima ambavyo hamkuvichimba, mashamba na miti ya mizeituni ambayo hamkuipanda, mtakula na kutosheka-
And houses full every good thing which not you filled and wells dug out which not you dug vineyards and olive trees which not you planted and you will eat and you will be satisfied.
12 basi iweni makini ili kwamba msije kumsahau Yahwe, aliyewaleta toka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
Take heed to yourself lest you should forget Yahweh who he brought out you from [the] land of Egypt from a house of slaves.
13 Mtamheshimu Yahwe Mungu wenu, yeye mtamwabudu, na mtaapa kwa jina lake.
Yahweh God your you will fear and him you will serve and in name his you will swear oaths.
14 Hamtawaendea miungu mingine, miungu ya watu wanaowazunguka wote-
Not you will walk! after gods other any of [the] gods of the peoples which [are] around you.
15 kwa kuwa Yahwe Mungu wenu katikati yenu ni Mungu wa wivu- kama mtafanya, hasira ya Yahwe Mungu wenu atawasha dhidi yenu na atawaangamiza kutoka kwenye uso wa dunia.
For [is] a God jealous Yahweh God your in midst your lest it should burn [the] anger of Yahweh God your on you and he will destroy you from on [the] surface of the ground.
16 Hamtamjaribu Yahwe Mungu wenu kama mlivyomjaribu huko Massah.
Not you will put to [the] test Yahweh God your just as you put [him] to [the] test at Massah.
17 Kwa bidii mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, maagizo yake makini, na amri ambazo amewaamuru.
Certainly you will keep! [the] commandments of Yahweh God your and testimonies his and statutes his which he has commanded you.
18 Mtafanya kile kilicho sahihi na kizuri katika macho ya Yahwe, kwamba iwe vizuri kwenu, na kwamba muweze kuingia na kumiliki nchi nzuri ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu,
And you will do the right and the good in [the] eyes of Yahweh so that it may go well for you and you will go and you will take possession of the land good which he swore Yahweh to ancestors your.
19 kuwaondoa maadui zenu wote mbele zenu, kama Yahwe alivyosema.
To drive out all enemies your from before you just as he has spoken Yahweh.
20 Wakati mwana wako auliza kwa wakati unaokuja, kusema,”Ni zipi amri za gano, sheria, na amri zingine ambazo Yahwe Mungu wetu alituamuru?
If he will ask you child your tomorrow saying what? [are] the testimonies and the statutes and the judgments which he commanded Yahweh God our you.
21 Basi utasema kwa mwana wako, tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, Yahwe alitutoa Misri kwa mkono wa uweza,
And you will say to child your slaves we were of Pharaoh in Egypt and he brought out us Yahweh from Egypt by a hand strong.
22 na alionesha ishara na maajabu, makuu na makali, Misri kwa Farao, na kwa nyumba yake yote, mbele ya macho yenu,
And he gave Yahweh signs and wonders great and bad - on Egypt on Pharaoh and on all household his to eyes our.
23 na alitutoa kutoka huko, ili kwamba atulete ndani, kutupa nchi ambayo aliaapa kwa baba zetu.
And us he brought out from there so as to bring us to give to us the land which he swore to ancestors our.
24 Yahwe alituamuru daima kuzishika amri hizi, kumuogopa Yahwe Mungu wetu kwa uzuri wetu, ili kwamba atuweke hai, kama tulivyo leo.
And he commanded us Yahweh to observe all the statutes these to fear Yahweh God our for good of us all the days to preserve alive us as the day this.
25 Kama tutashika maagizo haya yote mbele ya Yahwe Mungu wetu kama alivyotuamuru, hii itakuwa haki yetu.
And righteousness it will belong to us that we will take care to observe all the commandment this before Yahweh God our just as he commanded us.