< Torati 6 >
1 Sasa haya ni maagizo, amri, na sheria ambazo Yahwe Mungu wetu ameniamuru mimi kuwafundisha ninyi, ili kwamba muweze kuzishika katika nchi ambayo mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani kumiliki,
Now this is the commandment, the statutes, and the ordinances, which the LORD your God commanded to teach you, that ye might do them in the land whither ye go over to possess it —
2 ili kwamba mpate kumheshimu Yahwe wenu, ili muzishike amri zake zote na maagizo ninayowaamuru-ninyi, wana wenu na wana wa wana wenu, siku zenu zote za maisha, ili kwamba siku zenu ziongezeke.
that thou mightest fear the LORD thy God, to keep all His statutes and His commandments, which I command thee, thou, and thy son, and thy son's son, all the days of thy life; and that thy days may be prolonged.
3 Kwa hiyo wasikilizeni, Israeli, na kuzishika ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu, ili kusudi muweze kuzidi mno kwenye nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Yahwe Mungu wa Baba zenu, amewaahidi atafanya.
Hear therefore, O Israel, and observe to do it; that it may be well with thee, and that ye may increase mightily, as the LORD, the God of thy fathers, hath promised unto thee — a land flowing with milk and honey.
4 Sikiliza, Israel: Yahwe Mungu wetu ni mmoja.
HEAR, O ISRAEL: THE LORD OUR GOD, THE LORD IS ONE.
5 Mtampenda Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote, kwa roho zenu zote, na kwa akili zenu zote.
And thou shalt love the LORD thy God with all thy heart, and with all thy soul, and with all thy might.
6 Maneno ninayowaamuru ninyi leo yatakuwa katika moyo wenu;
And these words, which I command thee this day, shall be upon thy heart;
7 na mtayafundisha kwa bidii kwa watoto wenu, mtayazungumza wakati mkaapo katika nyumba zenu, wakati mlalapo, na wakati mwinukapo.
and thou shalt teach them diligently unto thy children, and shalt talk of them when thou sittest in thy house, and when thou walkest by the way, and when thou liest down, and when thou risest up.
8 Utazifunga kama ishara juu ya mkono wako, nayo yatakuwa utepe kati ya macho yako.
And thou shalt bind them for a sign upon thy hand, and they shall be for frontlets between thine eyes.
9 Utaziandika kwenye miimo ya mlango ya nyumba yako na kwenye malango.
And thou shalt write them upon the door-posts of thy house, and upon thy gates.
10 Wakati Yahwe Mungu wako akuleta kwenye nchi ambayo aliaapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwamba angekupa, pamoja na miji mikubwa na mizuri ambayo hamkuijenga,
And it shall be, when the LORD thy God shall bring thee into the land which He swore unto thy fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give thee — great and goodly cities, which thou didst not build,
11 na nyumba zilizojaa kila aina ya vitu vizuri ambavyo hamkuzifanya, visima ambavyo hamkuvichimba, mashamba na miti ya mizeituni ambayo hamkuipanda, mtakula na kutosheka-
and houses full of all good things, which thou didst not fill, and cisterns hewn out, which thou the didst not hew, vineyards and olive-trees, which thou didst not plant, and thou shalt eat and be satisfied —
12 basi iweni makini ili kwamba msije kumsahau Yahwe, aliyewaleta toka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
then beware lest thou forget the LORD, who brought thee forth out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
13 Mtamheshimu Yahwe Mungu wenu, yeye mtamwabudu, na mtaapa kwa jina lake.
Thou shalt fear the LORD thy God; and Him shalt thou serve, and by His name shalt thou swear.
14 Hamtawaendea miungu mingine, miungu ya watu wanaowazunguka wote-
Ye shall not go after other gods, of the gods of the peoples that are round about you;
15 kwa kuwa Yahwe Mungu wenu katikati yenu ni Mungu wa wivu- kama mtafanya, hasira ya Yahwe Mungu wenu atawasha dhidi yenu na atawaangamiza kutoka kwenye uso wa dunia.
for a jealous God, even the LORD thy God, is in the midst of thee; lest the anger of the LORD thy God be kindled against thee, and He destroy thee from off the face of the earth.
16 Hamtamjaribu Yahwe Mungu wenu kama mlivyomjaribu huko Massah.
Ye shall not try the LORD your God, as ye tried Him in Massah.
17 Kwa bidii mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, maagizo yake makini, na amri ambazo amewaamuru.
Ye shall diligently keep the commandments of the LORD your God, and His testimonies, and His statutes, which He hath commanded thee.
18 Mtafanya kile kilicho sahihi na kizuri katika macho ya Yahwe, kwamba iwe vizuri kwenu, na kwamba muweze kuingia na kumiliki nchi nzuri ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu,
And thou shalt do that which is right and good in the sight of the LORD; that it may be well with thee, and that thou mayest go in and possess the good land which the LORD swore unto thy fathers,
19 kuwaondoa maadui zenu wote mbele zenu, kama Yahwe alivyosema.
to thrust out all thine enemies from before thee, as the LORD hath spoken.
20 Wakati mwana wako auliza kwa wakati unaokuja, kusema,”Ni zipi amri za gano, sheria, na amri zingine ambazo Yahwe Mungu wetu alituamuru?
When thy son asketh thee in time to come, saying: 'What mean the testimonies, and the statutes, and the ordinances, which the LORD our God hath commanded you?
21 Basi utasema kwa mwana wako, tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, Yahwe alitutoa Misri kwa mkono wa uweza,
then thou shalt say unto thy son: 'We were Pharaoh's bondmen in Egypt; and the LORD brought us out of Egypt with a mighty hand.
22 na alionesha ishara na maajabu, makuu na makali, Misri kwa Farao, na kwa nyumba yake yote, mbele ya macho yenu,
And the LORD showed signs and wonders, great and sore, upon Egypt, upon Pharaoh, and upon all his house, before our eyes.
23 na alitutoa kutoka huko, ili kwamba atulete ndani, kutupa nchi ambayo aliaapa kwa baba zetu.
And He brought us out from thence, that He might bring us in, to give us the land which He swore unto our fathers.
24 Yahwe alituamuru daima kuzishika amri hizi, kumuogopa Yahwe Mungu wetu kwa uzuri wetu, ili kwamba atuweke hai, kama tulivyo leo.
And the LORD commanded us to do all these statutes, to fear the LORD our God, for our good always, that He might preserve us alive, as it is at this day.
25 Kama tutashika maagizo haya yote mbele ya Yahwe Mungu wetu kama alivyotuamuru, hii itakuwa haki yetu.
And it shall be righteousness unto us, if we observe to do all this commandment before the LORD our God, as He hath commanded us.'