< Torati 6 >
1 Sasa haya ni maagizo, amri, na sheria ambazo Yahwe Mungu wetu ameniamuru mimi kuwafundisha ninyi, ili kwamba muweze kuzishika katika nchi ambayo mnaenda ng'ambo ya pili ya Yordani kumiliki,
These now are the commandements, ordinances, and lawes, which the Lord your God commanded me to teach you, that ye might doe them in the land whither ye go to possesse it:
2 ili kwamba mpate kumheshimu Yahwe wenu, ili muzishike amri zake zote na maagizo ninayowaamuru-ninyi, wana wenu na wana wa wana wenu, siku zenu zote za maisha, ili kwamba siku zenu ziongezeke.
That thou mightest feare the Lord thy God, and keepe all his ordinances, and his commandements which I commaund thee, thou, and thy sonne, and thy sonnes sonne all the dayes of thy life, euen that thy dayes may be prolonged.
3 Kwa hiyo wasikilizeni, Israeli, na kuzishika ili kwamba iweze kuwa vizuri kwenu, ili kusudi muweze kuzidi mno kwenye nchi itiririkayo maziwa na asali, kama Yahwe Mungu wa Baba zenu, amewaahidi atafanya.
Heare therefore, O Israel, and take heede to doe it, that it may go well with thee, and that ye may increase mightily in the land that floweth with milke and hony, as the Lord God of thy fathers hath promised thee.
4 Sikiliza, Israel: Yahwe Mungu wetu ni mmoja.
Heare, O Israel, The Lord our God is Lord onely,
5 Mtampenda Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote, kwa roho zenu zote, na kwa akili zenu zote.
And thou shalt loue the Lord thy God with all thine heart, and with all thy soule, and with all thy might.
6 Maneno ninayowaamuru ninyi leo yatakuwa katika moyo wenu;
And these wordes which I commaund thee this day, shalbe in thine heart.
7 na mtayafundisha kwa bidii kwa watoto wenu, mtayazungumza wakati mkaapo katika nyumba zenu, wakati mlalapo, na wakati mwinukapo.
And thou shalt rehearse them continually vnto thy children, and shalt talke of them when thou tariest in thine house, and as thou walkest by the way, and when thou liest downe, and when thou risest vp:
8 Utazifunga kama ishara juu ya mkono wako, nayo yatakuwa utepe kati ya macho yako.
And thou shalt binde them for a signe vpon thine hand, and they shalbe as frontlets betweene thine eyes.
9 Utaziandika kwenye miimo ya mlango ya nyumba yako na kwenye malango.
Also thou shalt write them vpon ye postes of thine house, and vpon thy gates.
10 Wakati Yahwe Mungu wako akuleta kwenye nchi ambayo aliaapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka, na Yakobo, kwamba angekupa, pamoja na miji mikubwa na mizuri ambayo hamkuijenga,
And when the Lord thy God hath brought thee into the land, which he sware vnto thy fathers, Abraham, Izhak, and Iaakob, to giue to thee, with great and goodly cities which thou buildedst not,
11 na nyumba zilizojaa kila aina ya vitu vizuri ambavyo hamkuzifanya, visima ambavyo hamkuvichimba, mashamba na miti ya mizeituni ambayo hamkuipanda, mtakula na kutosheka-
And houses full of all maner of goods which thou filledst not, and welles digged which thou diggedst not, vineyards and oliue trees which thou plantedst not, and when thou hast eaten and art full,
12 basi iweni makini ili kwamba msije kumsahau Yahwe, aliyewaleta toka nchi ya Misri, toka nyumba ya utumwa.
Beware least thou forget the Lord, which brought thee out of the land of Egypt, from the house of bondage.
13 Mtamheshimu Yahwe Mungu wenu, yeye mtamwabudu, na mtaapa kwa jina lake.
Thou shalt feare the Lord thy God, and serue him, and shalt sweare by his Name.
14 Hamtawaendea miungu mingine, miungu ya watu wanaowazunguka wote-
Ye shall not walke after other gods, after any of the gods of the people which are round about you,
15 kwa kuwa Yahwe Mungu wenu katikati yenu ni Mungu wa wivu- kama mtafanya, hasira ya Yahwe Mungu wenu atawasha dhidi yenu na atawaangamiza kutoka kwenye uso wa dunia.
(For the Lord thy God is a ielous God among you: ) least the wrath of the Lord thy God be kindled against thee, and destroy thee from the face of the earth.
16 Hamtamjaribu Yahwe Mungu wenu kama mlivyomjaribu huko Massah.
Ye shall not tempt the Lord your God, as ye did tempt him in Massah:
17 Kwa bidii mtayashika maagizo ya Yahwe Mungu wenu, maagizo yake makini, na amri ambazo amewaamuru.
But ye shall keepe diligently the commandements of the Lord your God, and his testimonies, and his ordinances which he hath commanded thee,
18 Mtafanya kile kilicho sahihi na kizuri katika macho ya Yahwe, kwamba iwe vizuri kwenu, na kwamba muweze kuingia na kumiliki nchi nzuri ambayo Yahwe aliaapa kwa baba zenu,
And thou shalt doe that which is right and good in the sight of the Lord: that thou mayest prosper, and that thou mayest go in, and possesse that good land which the Lord sware vnto thy fathers,
19 kuwaondoa maadui zenu wote mbele zenu, kama Yahwe alivyosema.
To cast out all thine enemies before thee, as the Lord hath sayd.
20 Wakati mwana wako auliza kwa wakati unaokuja, kusema,”Ni zipi amri za gano, sheria, na amri zingine ambazo Yahwe Mungu wetu alituamuru?
When thy sonne shall aske thee in time to come, saying, What meane these testimonies, and ordinances, and Lawes, which the Lord our God hath commanded you?
21 Basi utasema kwa mwana wako, tulikuwa watumwa wa Farao huko Misri, Yahwe alitutoa Misri kwa mkono wa uweza,
Then shalt thou say vnto thy sonne, We were Pharaohs bondmen in Egypt: but the Lord brought vs out of Egypt with a mightie hand.
22 na alionesha ishara na maajabu, makuu na makali, Misri kwa Farao, na kwa nyumba yake yote, mbele ya macho yenu,
And the Lord shewed signes and wonders great and euill vpon Egypt, vpon Pharaoh, and vpon all his housholde, before our eyes,
23 na alitutoa kutoka huko, ili kwamba atulete ndani, kutupa nchi ambayo aliaapa kwa baba zetu.
And brought vs out from thence, to bring vs in, and to giue vs the land which he sware vnto our fathers.
24 Yahwe alituamuru daima kuzishika amri hizi, kumuogopa Yahwe Mungu wetu kwa uzuri wetu, ili kwamba atuweke hai, kama tulivyo leo.
Therefore the Lord hath commanded vs, to doe all these ordinances, and to feare the Lord our God, that it may goe euer well with vs, and that he may preserue vs aliue as at this present.
25 Kama tutashika maagizo haya yote mbele ya Yahwe Mungu wetu kama alivyotuamuru, hii itakuwa haki yetu.
Moreouer, this shall be our righteousnes before the Lord our God, if we take heede to keepe all these commandements, as he hath commanded vs.