< Torati 34 >

1 Musa aliondoka kutoka nyanda za Moabu mpaka mlima wa Nebo, hadi kilele cha Pisga, kilicho mkabala na Yericho. Huko Yahwe alimwonyesha nchi yote ya Gileadi kutoka umbali wa Dani,
Therfor Moyses stiede fro the feeldi places of Moab on the hil of Nebo, in to the cop of Fasga, ayens Gerico. And the Lord schewide to hym al the lond of Galaad `til to Dan,
2 na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi,
and al Neptalym, and the lond of Effraym and of Manasses, and al the lond of Juda, `til to the laste see; and the south part,
3 na Negevi, na uwanda wa bonde la Yericho, mji wa mitende, mpaka umbali wa Soari.
and the breede of the feeld of Jerico, of the citee of Palmes `til to Segor.
4 Yahwe alimwambia, “Hii ni nchi niliyoapa kwa Abrahamu, kwa Isaka, na kwa Yakobo, na kusema, “Nitawapatia uzao wako.” Nimekuruhusu uitazame kwa macho yako, lakini hautakwenda kule.”
And the Lord seide to hym, This is the lond for which Y swoor to Abraham, Isaac, and Jacob; and Y seide, Y schal yyue it to thi seed; thou hast seyn it with thin iyen, and thou schalt not passe `to it.
5 Basi Musa mtumishi wa Yahwe, alikufa pale katika nchi ya Moabu, kama neno la Yahwe lilivyoahidi.
And Moyses, the seruaunt of the Lord, was deed there, in the lond of Moab, `for the Lord comaundide.
6 Yahwe alimzika katika bonde katika nchi ya Moabu mkabala na Beth-peori, lakini hakuna ajuaye kaburi lake lilipo hadi leo hii.
And the Lord biriede hym in a valey of the lond of Moab, ayens Fegor, and no man knewe his sepulcre `til in to present day.
7 Musa alikuwa na umri wa miaka mia moja na ishirini alipokufa; macho yake hayakufifia, wala nguvu asili zake hazikupungua.
Moises was of an hundrid and twenti yeer whanne he diede; his iye dasewide not, nethir hise teeth weren stirid.
8 Watu wa Israeli walimuomboleza Musa katika nyanda za Moabu kwa siku thelathini, hapo ndipo siku za maombolezo ya Musa zilipotimia.
And the sones of Israel biwepten hym thretti daies in the feeldi places of Moab; and the daies of weilyng of men `bymorenynge Moises weren fillid.
9 Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejawa na roho ya hekima, kwa maana Musa alimwekea mkono juu yake. Watu wa Israeli walimsikiliza na kufanya yale ambayo Yahwe alimuamuru Musa.
Forsothe Josue, the sone of Nun, was fillid with `the spyrit of wisdom, for Moises settide hise hondis on hym; and the sones of Israel obeieden to Josue, and diden as the Lord comaundide to Moises.
10 Tangu hapo hakujatokea nabii katika Israeli kama Musa, ambaye Yahwe alimjua uso kwa uso.
And `a profete roos no more in Israel `as Moises, whom the Lord knewe face to face,
11 Hakujawahi kuwa na nabii yeyote kama yeye kwa ishara na miujiza ambayo Yahwe alimtuma kufanya katika nchi ya Misri, kwa Farao, na kwa watumishi wake, na kwa nchi yake yote.
in alle myraclis, and grete wondris, whiche the Lord sente bi hym, that he schulde do in the lond of Egipt to Farao, and alle hise seruauntis, and to al the lond `of hym,
12 Hakujawahi kuwa na nabii yeyote kama yeye kwa mambo yote makubwa, ya kutisha ambayo Musa aliyafanya machoni pa Israeli yote.
and al strong hond, and the `grete merueylis, whiche Moyses dide bifor al Israel.

< Torati 34 >