< Torati 33 >
1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
И сие благословение, имже благослови Моисей человек Божий сыны Израилевы прежде скончания своего,
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
и рече: Господь от Синаи прииде, и явися от Сиира нам, и приспе от горы Фарани, и прииде со тмами святых, одесную Его ангели с ним,
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
и пощаде люди Своя: и вси освященнии под руками Твоими, и сии под Тобою суть.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
И прия от словес Его закон, егоже заповеда нам Моисей, наследие сонму Иаковлю:
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
и будет в Возлюбленнем князь, собравшымся князем людским купно с племены Израилевыми.
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
Да живет Рувим, и да не умрет, и Симеон да будет мног числом.
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
И сие Иуде: услыши, Господи, глас Иудин и в люди его вниди: руце его поборют по нем, и помощник на враги его да будеши.
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
И Левию рече: дадите Левию явленная Его, и истину Его мужу преподобну, егоже искусиша Искушением, укориша его у воды Пререкания:
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
глаголяй отцу своему и матери своей: не видех тебе: и братии своея не позна, и сынов своих не уведе: сохрани словеса Твоя и завет Твой соблюде:
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
явят оправдания Твоя Иакову и закон Твой Израилю: возложат фимиам во гневе Твоем всегда на олтарь Твой:
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
благослови, Господи, крепость его и дела руку его приими: порази чресла воставших на него врагов его, и ненавидящии его да не востанут.
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
И Вениамину рече: возлюбленный Господем уповаяй вселится (в Нем), и Бог осеняет его во вся дни, и посреде рамен Его почи.
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
И Иосифови рече: от благословения Господня земля его, от красот небесных и росы, и от бездн источников низу,
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
и во время плодов солнечных обращений, и от схождений месячных,
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
и от верха гор начала, и от верха холмов вечных,
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
и по времени земли исполнения: и приятная Явившемуся в купине, да приидут на главу Иосифу, и на версе прославивыйся в братии.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
Первородный юнца доброта его, рози единорога рози его: ими языки избодет вкупе даже до края земли: сия тмы Ефремовы, и сия тысящи Манассиины.
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
И Завулону рече: возвеселися, Завулоне, во исходе твоем, и Иссахаре в селениих твоих:
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
языки потребят: и призовете тамо, и пожрете тамо жертву правды: яко богатство морское воздоит тя, и купли от язык при мори живущих.
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
И Гаду рече: благословен разширяяй Гада: яко лев почи, сокрушивый мышцу и князя:
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
и виде начатки своя, яко тамо разделися земля, князей собранных вкупе с началники людскими: правду Господь сотвори и суд Свой со Израилем.
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
И Дану рече: Дан, скимен львов, и изскочит от Васана.
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
И Неффалиму рече: Неффалиму насыщение приятных, и да насытится благословением от Господа: море и юг наследит.
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
И Асиру рече: благословен от чад Асир, и будет приятен братии своей: омочит в елей ногу свою:
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
железо и медь сапог его будет, и аки дни твоя крепость твоя.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
Несть якоже Бог Возлюбленнаго: восходяй на небо помощник твой, и великолепый в тверди:
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
и покрыет тя Божие начало, и под крепостию мышцей вечных: и отженет от лица твоего врага, глаголя: да погибнеши:
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
и вселится Израиль уповая един на земли Иаковли в вине и пшенице: и небо ему облачно росою.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
Блажен еси, Израилю: кто подобен тебе, людие спасаемии от Господа? Защитит помощник твой, и мечь хвала твоя: и солжут тебе врази твои, и ты на выю их наступиши.