< Torati 33 >
1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
Voici la bénédiction par laquelle Moïse, homme de Dieu, a béni les enfants d'Israël avant sa mort.
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
Il dit, « Yahvé est venu du Sinaï, et s'est élevé de Seir jusqu'à eux. Il brillait du mont Paran. Il est issu des dix mille saints. A sa droite, il y avait une loi ardente pour eux.
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
Oui, il aime le peuple. Tous ses saints sont dans votre main. Ils se sont assis à vos pieds. Chacun reçoit vos paroles.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
Moïse nous a donné une loi, un héritage pour l'assemblée de Jacob.
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
Il était roi à Jeshurun, quand les chefs du peuple étaient réunis, toutes les tribus d'Israël réunies.
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
« Que Ruben vive et ne meure pas; Et que ses hommes ne soient pas trop nombreux. »
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
Ceci est pour Juda. Il a dit, « Écoute, Yahvé, la voix de Juda. Amenez-le à son peuple. Avec ses mains, il s'est battu pour lui-même. Tu seras un secours contre ses adversaires. »
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
À propos de Lévi, il a dit, « Ton Thummim et ton Urim sont avec ton pieux, que vous avez prouvé à Massah, avec qui tu t'es disputé aux eaux de Meribah.
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
Il dit de son père et de sa mère: « Je ne l'ai pas vu ». Il n'a pas reconnu ses frères, et il ne connaissait pas non plus ses propres enfants; car ils ont observé ta parole, et garde ton alliance.
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
Ils enseigneront à Jacob tes ordonnances, et Israël ta loi. Ils mettront de l'encens devant toi, et un holocauste entier sur ton autel.
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
Yahvé, bénis ses compétences. Acceptez l'œuvre de ses mains. Frappez les hanches de ceux qui se dressent contre lui, de ceux qui le haïssent, afin qu'ils ne ressuscitent pas. »
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
A propos de Benjamin, il dit, « Le bien-aimé de Yahvé habitera en sécurité auprès de lui. Il le couvre toute la journée. Il habite entre ses épaules. »
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
A propos de Joseph, il dit, « Son pays est béni par Yahvé, pour les choses précieuses des cieux, pour la rosée, pour le profond qui s'étend en dessous,
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
pour les choses précieuses des fruits du soleil, pour les choses précieuses que la lune peut rapporter,
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
pour les meilleures choses des anciennes montagnes, pour les choses précieuses des collines éternelles,
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
pour les biens précieux de la terre et sa plénitude, la bonne volonté de celui qui vivait dans la brousse. Que cela tombe sur la tête de Joseph, sur la couronne de la tête de celui qui a été séparé de ses frères.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
La majesté appartient au premier-né de son troupeau. Ses cornes sont les cornes du bœuf sauvage. Avec eux, il poussera tous les peuples jusqu'aux extrémités de la terre. Ce sont les dix mille d'Ephraïm. Ce sont les milliers de Manassé. »
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
Sur Zabulon, il dit, « Réjouis-toi, Zabulon, de ta sortie; et Issachar, dans vos tentes.
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
Ils appelleront les peuples sur la montagne. Ils y offriront des sacrifices de justice, car ils puiseront dans l'abondance des mers, les trésors cachés du sable. »
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
A propos de Gad, il dit, « Celui qui élargit Gad est béni. Il habite comme une lionne, et déchire le bras et la couronne de la tête.
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
Il a fourni la première partie pour lui-même, car la part du législateur lui était réservée. Il est venu avec les têtes du peuple. Il a exécuté la justice de Yahvé, Ses ordonnances avec Israël. »
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
A propos de Dan, il dit, « Dan est un lionceau qui bondit hors de Bashan. »
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
A propos de Nephtali, il dit, « Naphtali, satisfait de la faveur, plein de la bénédiction de Yahvé, Posséder l'ouest et le sud. »
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
A propos d'Asher, il a dit, « Asher a la chance d'avoir des enfants. Qu'il soit accepté par ses frères. Qu'il trempe son pied dans l'huile.
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
Tes barres seront en fer et en bronze. Ta force sera à la mesure de tes jours.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
« Il n'y a personne comme Dieu, Jeshurun, qui chevauche les cieux pour vous aider, dans son excellence sur les cieux.
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
Le Dieu éternel est ta demeure. En dessous, il y a les bras éternels. Il a chassé l'ennemi de devant vous, et a dit: « Détruisez!
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
Israël habite en sécurité, la seule fontaine de Jacob, Au pays du grain et du vin nouveau. Oui, ses cieux laissent tomber la rosée.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
Tu es heureux, Israël! Qui est comme vous, un peuple sauvé par Yahvé, le bouclier de ton aide, l'épée de votre excellence? Vos ennemis se soumettront à vous. Tu fouleras leurs hauts lieux. »