< Torati 33 >
1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
Now, this, is the blessing wherewith Moses, the man of God, blessed the sons of Israel, —before his death.
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
And he said—Yahweh from Sinai, came near, —Yea he dawned, out of Seir, upon them, He shone forth out of Mount Paran, Yea he came out of holy myriads, —Out of his right hand [proceeded] fire to guide them.
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
Yea he loved the tribes, All his holy ones, were in thy hand, —Yea, they, were encamped at thy feet, Each one bare away some of thy words.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
A law, did Moses command us, —A possession, for the convocation of Jacob.
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
Thus became he in, Jeshurun, a king, —When the heads of the people gathered them-selves together, As one man, the tribes of Israel. [Reuben] —
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
Let Reuben live and not die, —Nor his men be easily counted.
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
And, this, is for Judah, when he said, Hear, O Yahweh, the voice of Judah, That unto his own people, thou wouldst bring him home, —Let, his own hands, suffice him, And, a helper from his adversaries, do thou become.
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
And of Levi, he said: Let, thy perfections and thy lights, belong unto thy man of lovingkindness, —Whom thou didst put to the proof at Massah, With whom thou didst contend over the waters of Meribah;
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
Who saith of his father and of his mother, I behold them not, And, his own brethren, regardeth he not, And, his own sons, observeth he not, —Because they watch thy speech, That, thy covenant, they may preserve;
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
May teach thy regulations unto Jacob, And thy law unto Israel, —May put incense in thy nostrils, And a whole-offering upon thine altar.
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
Bless, O Yahweh his substance, And with the work of his hands, wilt thou be well pleased, —Crush thou the loins of them who rise up against him, And of them who hate him, that they rise not again.
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
Of Benjamin, he said, The beloved of Yahweh, shall settle down securely, —With one to throw a shade over him all the day long, Yea, between his shoulders, hath he found rest.
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
And of Joseph, he said, Blessed of Yahweh, be his land, —With the precious things of the heavens with the dew, And with the abyss, couching beneath;
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
And with the precious fruits of the sun, —And with the precious yield of the moons;
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
And with the chief of the ancient mountains, —And with the precious things of the age-abiding hills;
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
And with the precious things of the earth and its fulness, And with the goodwill of One who dwelt in a thorn-bush.—Let it come on the head of Joseph, And on the crown of the head of him who was consecrated among his brethren.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
His firstborn ox, be an honour to him. And the horns of a buffalo, be his horns, With them, let him thrust, peoples, All at once, to the ends of the earth, —Yea, [with] these, the myriads of Ephraim, And, [with] those, the thousands of Manasseh.
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
And, of Zebulun, he said, Rejoice, Zebulun in thy going out, —And [thou], Issachar in thy tents:
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
The peoples, unto the mountain, will they call, There, will they offer the sacrifices of righteousness, —For, the abundance of the seas, will they suck, Hidden treasures of the sand.
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
And, of Gad, he said: Blessed, be he that hath made room for Gad, —As a lioness, hath he laid himself down, And hath torn an arm likewise the crown of the head;
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
And hath provided a first part for himself, For, there, a commander’s portion hath been hid, —So he cometh with the heads of the people, The righteousness of Yahweh, he executeth, And his regulations, with Israel.
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
And, of Dan, he said, Dan, is a lion’s whelp, —He leapeth out of Bashan.
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
And, of Naphtali, he said, O Naphtali! satisfied with favour, And full with the blessing of Yahweh, —The west and the sunny south, do thou possess.
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
And, of Asher, he said, Most blessed of sons, be Asher, —Let him have the goodwill of his brethren, And let him dip, in oil, his foot:
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
Iron and bronze, be thy sandals, And, as thy days, be thy strength.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
There is none like GOD, O Jeshurun, —Riding upon the heavens to thy help, —And for his own majesty, on the skies;
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
Above, is the God of aforetime, And, beneath, are the Arms of the ages, —So he driveth before thee the foe, And doth say—Destroy!
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
Thus hath Israel settled down securely, Alone, the fountain of Jacob, Within a land both of corn and new wine, —His heaven also droppeth down dew.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
How happy art thou, O Israel! Who is like unto thee, O people victorious in Yahweh? Thy helpful shield, who also is thy majestic sword, —So that thy foes come cringing unto thee, And, thou, upon their heights, dost march along.