< Torati 33 >

1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
This is the blessing that Moses [Drawn out] the man of God blessed the children of Israel [God prevails] before his death.
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
He said, “Adonai came from Sinai [Thorn], and rose from Seir to them. He shone from Mount Paran. He came from the ten thousands of holy ones. At his right hand was a fiery law for them.
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
Yes, he choveiv ·hides in bosom, loves· the people. All his saints are in your hand. They sat down at your feet. Each receives your words.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
The Torah ·Teaching· Moses [Drawn out] enjoined us, an inheritance for the assembly of Jacob [Supplanter].
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
He was king in Jeshurun [Upright one], when the heads of the people were gathered, all the tribes of Israel [God prevails] together.
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
“Let Reuben [See, a son!] live, and not die; Nor let his men be few.”
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
This is for Judah [Praised]. He said, “Sh'ma ·Hear obey·, Adonai, the voice of Judah [Praised]. Bring him in to his people. With his hands he contended for himself. You shall be a help against his adversaries.”
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
About Levi [United with] he said, “Your Thummim ·Perfections· and your 'Urim ·Lights· are with your pious one, whom you proved at Massah [Testing], with whom you contended at the waters of Meribah [Quarreling].
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
He said of his father, and of his mother, ‘I have not seen him.’ He didn’t acknowledge his brothers, nor did he know his own children; for they have observed your word, and keep your covenant.
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
They shall teach Jacob [Supplanter] your judgments, and Israel [God prevails] your Torah ·Teaching·. They shall put incense before you, and whole burnt offering on your altar.
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
Adonai, bless his skills. Accept the work of his hands. Strike through the hips of those who rise up against him, of those who hate him, that they not rise again.”
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
About Benjamin [Son of right hand, Son of south] he said, “The Yadid ·Beloved· of Adonai will dwell in safety by him. He covers him all day long. He dwells between his shoulders.”
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
About Joseph [May he add] he said, “His land is blessed by Adonai, for the precious things of the heavens, for the dew, for the deep that couches beneath,
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
for the precious things of the fruits of the sun, for the precious things that the moon can yield,
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
for the best things of the ancient mountains, for the precious things of the everlasting hills,
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
for the precious things of the earth and its fullness, the good will of him who lived in the bush. Let this come on the head of Joseph [May he add], on the crown of the head of him who was separated from his brothers.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
The firstborn of his herd, majesty is his. His horns are the horns of the wild ox. With them he will push all the peoples, to the ends of the earth. They are the ten thousands of Ephraim [Fruit]. They are the thousands of Manasseh [Causing to forget].”
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
About Zebulun [Living together] he said, “Rejoice, Zebulun [Living together], in your going out; and Issachar [Hire, Reward], in your tents.
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
They will call the peoples to the mountain. There they will offer sacrifices of righteousness, for they will draw out the abundance of the seas, the hidden treasures of the sand.”
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
About Gad [Good fortune] he said, “He who enlarges Gad [Good fortune] is blessed. He dwells as a lioness, and tears the arm, yes, the crown of the head.
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
He provided the first part for himself, for the Torah-giver’s portion reserved was reserved for him. He came with the heads of the people. He executed the righteousness of Adonai, His judgments with Israel [God prevails].”
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
About Dan [He judged] he said, “Dan [He judged] is a lion’s cub that leaps out of Bashan.”
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
About Naphtali [My wrestling] he said, “Naphtali [My wrestling], satisfied with favor, full of Adonai’s blessing, Possess the west and the south.”
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
About Asher [Happy] he said, “Asher [Happy] is blessed with children. Let him be acceptable to his brothers. Let him dip his foot in oil.
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
Your bars will be iron and bronze. As your days, so your strength will be.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
“There is no one like God, Jeshurun [Upright one], who rides on the heavens for your help, in his excellency on the skies.
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
The eternal God is your dwelling place. Underneath are the everlasting arms. He divorce and cast away the enemy from before you, and said, ‘Destroy!’
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
Israel [God prevails] dwells in safety; the fountain of Jacob [Supplanter] alone, In a land of grain and new wine. Yes, his heavens drop down dew.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
You are happy, Israel [God prevails]! Who is like you, a people saved by Adonai, the shield of your help, the sword of your excellency? Your enemies will submit themselves to you. You will tread on their high places.”

< Torati 33 >