< Torati 29 >

1 Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia watu wa Israeli katika nchi ya Moabu, maneno ambayo yaliongezwa katika agano alilolifanya pamoja nao kule Horebu.
These are the words of the covenant which Jehovah commanded Moses to make with the children of Israel in the land of Moab, besides the covenant which he made with them in Horeb.
2 Musa aliwaita Waisraeli wote na kuwaambia, “Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu katika nchi ya Misri kwa Farao, kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote –
And Moses called unto all Israel, and said unto them, Ye have seen all that Jehovah did before your eyes in the land of Egypt unto Pharaoh, and unto all his servants, and unto all his land;
3 mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona, ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa.
the great trials which thine eyes saw, the signs, and those great wonders:
4 Lakini mpaka leo Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia.
but Jehovah hath not given you a heart to know, and eyes to see, and ears to hear, unto this day.
5 Nimewaongoza kwa miaka arobaini jangwani; mavazi yenu hayakuchakaa juu yenu, na ndala zenu hazikuchakaa miguuni mwenu.
And I have led you forty years in the wilderness: your clothes are not waxed old upon you, and thy shoe is not waxed old upon thy foot.
6 Hamkula mkate wowote, na wala hamkunywa divai yoyote au kinywaji chochote chenye ulevi, ili kwamba muweze kujua kuwa mimi ni Yahwe Mungu wenu.
Ye have not eaten bread, neither have ye drunk wine or strong drink; that ye may know that I am Jehovah your God.
7 Mlipokuja mahali hapa, Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani, walikuja dhidi yetu kutupiga, na tukawapiga.
And when ye came unto this place, Sihon the king of Heshbon, and Og the king of Bashan, came out against us unto battle, and we smote them:
8 Tulichukua ardhi yao na kuwapa kama urithi Wareubeni, kwa Wagadi, na kwa nusu ya kabila ya Manase.
and we took their land, and gave it for an inheritance unto the Reubenites, and to the Gadites, and to the half-tribe of the Manassites.
9 Kwa hiyo shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda, ili ufanikiwe katika kila kitu ufanyacho.
Keep therefore the words of this covenant, and do them, that ye may prosper in all that ye do.
10 Nyie wote, mnasimama leo, mbele ya Yahwe Mungu wenu; machifu wenu, makabila yenu, wazee wenu, na maafisa wenu – wanaume wote wa Israeli,
Ye stand this day all of you before Jehovah your God; your heads, your tribes, your elders, and your officers, even all the men of Israel,
11 watoto wenu, wake zenu, na wageni ambao wamo miongoni wa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye maji.
your little ones, your wives, and thy sojourner that is in the midst of thy camps, from the hewer of thy wood unto the drawer of thy water;
12 Mpo hapa ili kwamba muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo,
that thou mayest enter into the covenant of Jehovah thy God, and into his oath, which Jehovah thy God maketh with thee this day;
13 ili kwamba awafanye leo kuwa watu wake, na kwamba aweze kuwa Mungu kwa ajili yako, kama alivyonena kwako, na kama alivyoapa kwa mababu zako, kwa Abrahamu, kwa Isaka na kwa Yakobo.
that he may establish thee this day unto himself for a people, and that he may be unto thee a God, as he spake unto thee, and as he sware unto thy fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob.
14 Kwa maana ninafanya agano hili na kiapo hiki sio na wewe tu –
Neither with you only do I make this covenant and this oath,
15 pamoja kila mtu aliyesimama hapa pamoja nasi leo mbele ya Yahwe Mungu wetu – bali na wale ambao hawapo pamoja nasi leo pia.
but with him that standeth here with us this day before Jehovah our God, and also with him that is not here with us this day
16 Unajua jinsi tulivyoishi katika nchi ya Misri, na jinsi tulivyopenya miongoni mwa mataifa ambao uliwapita.
(for ye know how we dwelt in the land of Egypt, and how we came through the midst of the nations through which ye passed;
17 Mmeona sanamu zao zinazokera zilizotengenezwa kwa mbao na mawe, fedha na dhahabu, ambazo zilikuwa miongoni mwenu.
and ye have seen their abominations, and their idols, wood and stone, silver and gold, which were among them);
18 Hakikisha hakuna kati yenu mwanamume, mwanamke, ukoo, au kabila ambaye moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo, ili kwenda na kuabudu miungu ya mataifa hayo. Hakikisha hakuna kati yenu mzizi utakaozaa nyongo na pakanga.
lest there should be among you man, or woman, or family, or tribe, whose heart turneth away this day from Jehovah our God, to go to serve the gods of those nations; lest there should be among you a root that beareth gall and wormwood;
19 Wakati mtu huyo anaposikia maneno ya laana hii, atajifariji moyoni mwake na kusema, “Nitakuwa na amani, ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu”. Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu.
and it come to pass, when he heareth the words of this curse, that he bless himself in his heart, saying, I shall have peace, though I walk in the stubbornness of my heart, to destroy the moist with the dry.
20 Yahwe hatamsamehe, lakini badala yake, hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika mtu huyo, na laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake, na Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni.
Jehovah will not pardon him, but then the anger of Jehovah and his jealousy will smoke against that man, and all the curse that is written in this book shall lie upon him, and Jehovah will blot out his name from under heaven.
21 Yahwe atamuweka kando kwa ajili ya maafa kutoka katika makabila yote ya Israeli, kwa kuzingatia laana zote za agano ambazo zimeandikwa katika kitabu hiki cha sheria.
And Jehovah will set him apart unto evil out of all the tribes of Israel, according to all the curses of the covenant that is written in this book of the law.
22 Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watazungumza watakapoona mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe –
And the generation to come, your children that shall rise up after you, and the foreigner that shall come from a far land, shall say, when they see the plagues of that land, and the sicknesses wherewith Jehovah hath made it sick;
23 na watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo, ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda, ambapo hapaoti mmea wowote, kama anguko la Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, ambayo Yahwe aliangamiza katika ghadhabu na hasira yake –
[and that] the whole land thereof is brimstone, and salt, [and] a burning, [that] it is not sown, nor beareth, nor any grass groweth therein, like the overthrow of Sodom and Gomorrah, Admah and Zeboiim, which Jehovah overthrew in his anger, and in his wrath:
24 watasema kwa pamoja na mataifa mengine, “Kwa nini Yahwe amefanya hili katika nchi hii? Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?”
even all the nations shall say, Wherefore hath Jehovah done thus unto this land? what meaneth the heat of this great anger?
25 Kisha watu watasema, “Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao, alilofanya nao alipowatoa kutoka Misri,
Then men shall say, Because they forsook the covenant of Jehovah, the God of their fathers, which he made with them when he brought them forth out of the land of Egypt,
26 na kwa sababu waliondoka na kutumikia miungu mingine na kuzisujudu, miungu ambayo hawakujiua na ambayo hakuwapatia.
and went and served other gods, and worshipped them, gods that they knew not, and that he had not given unto them:
27 Kwa hiyo hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii, ili kuleta juu yake laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki.
therefore the anger of Jehovah was kindled against this land, to bring upon it all the curse that is written in this book;
28 Yahwe amewang’oa kutoka nchini kwao kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali, na kuwatupa katika nchi nyingine, leo.
and Jehovah rooted them out of their land in anger, and in wrath, and in great indignation, and cast them into another land, as at this day.
29 Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee; lakini mambo yaliyofichuliwa ni ya kwetu milele pamoja na wazawa wetu, ili tufanye maneno yote ya sheria hii.
The secret things belong unto Jehovah our God; but the things that are revealed belong unto us and to our children for ever, that we may do all the words of this law.

< Torati 29 >