< Torati 27 >
1 Musa na wazee wa Israeli waliwaamuru watu na kusema, “Zishikeni amri zote ninazowaamuru leo.
And Moses and the elders of Israel commanded the people, saying, Keep all the commandment which I command you this day.
2 Katika siku mtakapopita juu ya Yordani kwenye nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia, mnapaswa kutengeneza mawe kiasi makubwa na kuyachapa kwa lipu.
And it shall be on the day when ye shall pass over the Jordan to the land which Jehovah thy God gives thee, that thou shall set up for thee great stones, and plaster them with plaster.
3 Mnatakiwa kuyaandika juu yake maneno yote ya sheria hii pale mtakapovuka; ili muweze kwenda katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anawapatia, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali, kama Yahwe, Mungu wa mababu zenu, alivyowaahidi.
And thou shall write upon them all the words of this law when thou have passed over, that thou may go in to the land which Jehovah thy God gives thee, a land flowing with milk and honey, as Jehovah, the God of thy fathers, has promised thee.
4 Mtakapovuka juu ya Yordani, yapangane haya mawe ninayowaamuru leo, juu ya mlima wa Ebali, na myapige kwa lipu.
And it shall be, when ye have passed over the Jordan, that ye shall set up these stones, which I command you this day, in mount Ebal, and thou shall plaster them with plaster.
5 Hapo mnapaswa kujenga dhabahu kwa Yahwe Mungu wako, dhabahu la mawe; lakini hautakiwi kuinua chombo cha chuma kujenga mawe.
And there thou shall build an altar to Jehovah thy God, an altar of stones. Thou shall lift up no iron upon them.
6 Unatakiwa kujenga dhabahu ya Yahwe Mungu wako kwa mawe yasiyokuwa na kazi; unatakiwa kutoa dhabihu ya kuteketeza juu yake kwa Yahwe Mungu wako,
Thou shall build the altar of Jehovah thy God of unhewn stones. And thou shall offer burnt offerings on it to Jehovah thy God.
7 na utatoa sadaka ya pamoja na utakula pale; utafurahia mbele ya Yahwe Mungu wako.
And thou shall sacrifice peace offerings, and shall eat there, and thou shall rejoice before Jehovah thy God.
8 Utaandika juu ya mawe maneno yote ya sheria hii kwa wazi.
And thou shall write upon the stones all the words of this law very plainly.
9 Musa na makuhani, Walawi, waliongea na Waisraeli wote na kusema, “Nyamazeni na sikilizeni Israel: Leo mmekuwa watu wa Yahwe Mungu wenu.
And Moses and the priests the Levites spoke to all Israel, saying, Keep silence, and hearken, O Israel. This day thou have become the people of Jehovah thy God.
10 Mnapaswa basi kutii sauti ya Yahwe Mungu wenu na kutii amri na sheria zake ambazo ninawaamuru leo.”
Thou shall therefore obey the voice of Jehovah thy God, and do his commandments and his statutes, which I command thee this day.
11 Musa aliwaamuru watu siku hiyo hiyo na kusema,
And Moses charged the people the same day, saying,
12 “Makabila haya yanapaswa kusimama katika mlima Gerizimu kuwabariki watu baada ya nyinyi kuvuka Yordani; Simeoni, Lawi, Judah, Isakari, Yusufu na Benyamini.
These shall stand upon mount Gerizim to bless the people, when ye have passed over the Jordan: Simeon, and Levi, and Judah, and Issachar, and Joseph, and Benjamin.
13 Haya ni makabila ambayo lazima yasimame juu yam lima Ebali kutamka laana: Rubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dan na Naftali.
And these shall stand upon mount Ebal for the curse: Reuben, Gad, and Asher, and Zebulun, Dan, and Naphtali.
14 Walawi watajibu na kusema kwa wanamume wote wa Israeli kwa sauti kubwa:
And the Levites shall answer, and say to all the men of Israel with a loud voice,
15 “Alaaniwe mwanamume atakayechonga sanamu au kinyago, chukizo kwa Yahwe, kazi ya mikono ya fundi, ambayo ataifanya sirini”. Kisha watu wote wanapaswa kujibu na kusema, ‘Amina’.
Cursed be the man who makes a graven or molten image, an abomination to Jehovah, the work of the hands of the craftsman, and sets it up in secret. And all the people shall answer and say, Truly.
16 Alaaniwe mwanamume atakayemuaibisha baba yake au mama yake. Kisha watu wote waseme, 'Amina'.
Cursed be he who dishonors his father or his mother. And all the people shall say, Truly.
17 Alaaniwe mwanamume anayetoa alama ya ardhi.' Kisha watu wote na waseme, 'Amina'.
Cursed be he who removes his neighbor's landmark. And all the people shall say, Truly.
18 Alaaniwe mwanamume asababishae kipofu kutoka nje ya barabara. Kisha watu wote waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who makes the blind to wander out of the way. And all the people shall say, Truly.
19 Alaaniwe mwanamume atumiaye nguvu kupokonya haki inayomstahili mgeni, yatima, au mjane. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who distorts the justice to the sojourner, fatherless, and widow. And all the people shall say, Truly.
20 Alaaniwe mwanamume atakayelala na mke wa baba yake, kwa sababu atakuwa amechukua haki za baba yake’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who lies with his father's wife, because he has uncovered his father's skirt. And all the people shall say, Truly.
21 Alaaniwe mwanamume atakayelala na aina yoyote ya mnyama’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who lies with any manner of beast. And all the people shall say, Truly.
22 Alaaniwe mwanamume atakayelala na dada yake, binti wa baba yake, au binti wa mama yake. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who lies with his sister, the daughter of his father, or the daughter of his mother. And all the people shall say, Truly.
23 Alaaniwe mwanamume atakayelala na mama mkwe’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who lies with his mother-in-law. And all the people shall say, Truly.
24 Alaaniwe mwanamume atakayemuua jirani yake kwa siri’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who smites his neighbor in secret. And all the people shall say, Truly.
25 Alaaniwe mwanamume apokeaye rushwa kumuua mtu asiye na hatia’. Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed be he who takes a bribe to kill an innocent man. And all the people shall say, Truly.
26 Alaaniwe mwanamume asiyethibitisha maneno ya sheria hii, ili kwamba ayatii.’ Kisha watu wote lazima waseme, ‘Amina’.
Cursed is every man who does not continue in all the words of this law to do them. And all the people shall say, Truly.