< Torati 26 >
1 Utakapofika katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia kama urithi, na utakapoimiliki na kuishi ndani yake,
Lorsque ta seras entré dans le pays que l'Éternel, ton Dieu, te donne en propriété et que tu l'auras conquis, et t'y seras établi,
2 basi unatakiwa kuchukua baadhi ya mavuno yote ya kwanza ya ardhi uliyoyaleta kutoka katika nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia. Unatakiwa kuyaweka ndani ya kikapu na kuelekea katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atapachagua kama mahali patakatifu.
tu prendras des prémices de tous les produits du sol, que tu retireras de ton pays à toi donné par l'Éternel, ton Dieu; et tu les mettras dans une corbeille, et te rendras au lieu que choisira l'Éternel, ton Dieu, pour y fixer son nom;
3 Unatakiwa kwenda kwa kuhani ambaye atakuwa akihudumu katika siku hizo na kumwambia, “Siku ya leo ninakiri kwa Yahwe Mungu wako ya kuwa nimekuja katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zetu kutupatia”.
puis tu t'adresseras au Prêtre qui existera à cette époque, et tu lui diras: Je déclare aujourd'hui à l'Éternel, ton Dieu, être entré dans le pays que l'Éternel a juré à nos pères de nous donner.
4 Kuhani anatakiwa kuchukua kikapu mkononi mwako na kukiweka madhabahuni ya Yahwe Mungu wako.
Et le Prêtre recevra la corbeille de ta main et la déposera devant l'Autel de l'Éternel, ton Dieu.
5 Unapaswa kusema mbele ya Yahwe Mungu wako, “Babu yangu alikuwa Mwaremi mzururaji. Alikwenda chini hadi Misri na kukaa kule, na idadi ya watu wake ilikuwa chache. Kule akawa taifa kubwa, lenye nguvu na idadi kubwa.
Alors tu prendras la parole et diras devant l'Éternel, ton Dieu: Mon père était un Araméen nomade, et il descendit en Egypte, et y séjourna n'ayant que peu de gens avec lui, et là il est devenu une grande, puissante et nombreuse nation.
6 Wamisri walitutendea vibaya na kututesa. Walitulazimisha kufanya kazi za watumwa.
Et les Égyptiens nous maltraitèrent et nous opprimèrent, et nous soumirent à un dur esclavage,
7 Tulimlilia Yahwe, Mungu wa baba zetu, naye akasikia sauti yetu na kuona mateso yetu, kazi zetu na mateso yetu.
et nous criâmes à l'Éternel, Dieu de nos pères, et l'Éternel entendit notre voix et vit notre misère et notre peine et notre oppression.
8 Yahwe alituondoa Misri kwa mkono wake mkuu, kwa mkono wake ulionyoshwa, kwa hofu kuu, kwa ishara na miujiza;
Et l'Éternel nous retira de l'Egypte d'une main forte et avec un bras étendu, et au moyen d'une grande terreur et de signes et de prodiges;
9 na ametuleta katika sehemu hii na kutupatia nchi hii, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.
et Il nous a fait arriver en ce lieu, et nous a donné ce pays, pays découlant de lait et de miel.
10 Tazama sasa, nimeleta mavuno ya kwanza kutoka katika nchi ambayo wewe, Yahwe, umenipatia.” Unapaswa kuweka chini mbele ya Yahwe Mungu wako na kuabudu mbele zake;
Et maintenant, voici, j'apporte les prémices des produits du sol que tu m'as donné, Éternel. Puis dépose-les devant l'Éternel, ton Dieu, et adore l'Éternel, ton Dieu,
11 na unapaswa kufurahia katika mema yote ambayo Yahwe Mungu wako amekufanyia, kwa ajili na nyumba yako – wewe, na Mlawi, na mgeni aliye miongoni mwako.
et réjouis-toi de tous les biens que t'a donnés à toi et à ta maison l'Éternel, ton Dieu, toi et le Lévite et l'étranger qui sera chez toi.
12 Utakapomaliza kutoa zaka yote ya mavuno katika mwaka wa tatu, yaani, mwaka wa kutoa zaka, basi unapaswa kuwapatia Mlawi, kwa mgeni, kwa yatima, na kwa mjane, ili kwamba waweze kula ndani ya malango yenu ya mji na kujazilishwa.
Quand tu auras achevé de délivrer toute la dîme de ton revenu, la troisième année, année de cette dîme, et que tu auras donné au Lévite, à l'étranger, à l'orphelin et à la veuve de quoi manger et se rassasier dans tes Portes,
13 Unatakiwa kusema mbele ya Yahwe Mungu wako, “Nimetoa kutoka nyumbani mwangu vitu ambavyo ni mali ya Yahwe, na kumpatia Mlawi, mgeni, yatima, na mjane, kulingana na amri zote ulizonipatia. Sijavunja amri yako yoyote, wala sijazisahau.
tu diras devant l'Éternel ton Dieu: J'ai ôté de ma maison la chose sacrée, et l'ai donnée au Lévite, à l'étranger, à l'orphelin et à la veuve et me conformant en tout point au commandement que tu m'as prescrit, je n'ai ni transgressé, ni oublié tes commandements.
14 Sijala kati yao wakati wa maombolezo yangu, wala sijaziweka mahali pengine nilipokuwa mchafu, wala sijazitoa kati yao kwa heshima ya wafu. Nimesikiliza sauti ya Yahwe Mungu wangu; Nimetii kila kitu ulichoniamuru kukifanya.
Je n'en ai point mangé pendant mon deuil, et n'en ai rien soustrait pour un [usage] immonde, et n'en ai rien donné pour un repas mortuaire; j'ai été docile à la voix de l'Éternel, mon Dieu, j'ai agi en tout comme tu me l'as prescrit.
15 Tazama chini kutoka mahali patakatifu unapoishi, kutoka mbinguni, na ubariki watu wako Israeli, na nchi uliyotupatia, kama ulivyoapa kwa mababu zetu, nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.
Abaisse tes regards de ta demeure sainte, des Cieux, et bénis ton peuple d'Israël et le sol que tu nous as donné à teneur du serment que tu fis à nos pères, pays découlant de lait et de miel.
16 Leo Yahwe Mungu wako anawaamuru kuzitii sheria na amri hizi; basi utazishikilia na kuzitenda kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote.
En ce jour l'Éternel, ton Dieu, te commande de mettre en pratique ces statuts et ces lois: applique-toi donc à les pratiquer de tout ton cœur et de toute ton âme.
17 Umetamka leo ya kuwa Yahwe ni Mungu wako, na kwamba utatembea katika njia zake na kushikilia sheria zake, maagizo yake na amri zake, na kwamba utaisikiliza sauti yake.
Aujourd'hui tu as obtenu de l'Éternel la déclaration qu'il sera ton Dieu, et que tu dois marcher dans ses voies et garder ses statuts, ses commandements et ses lois, et obéir à sa voix;
18 Leo Yahwe ametamka ya kwamba mu watu ambao ni mali yake, kama alivyoahidi kwenu, na kwamba mnapaswa kushikilia amri zake zote.
et aujourd'hui l'Éternel t'a fait promettre que tu seras son peuple particulier, comme Il te l'a promis, et que tu garderas tous ses commandements,
19 Na atawaweka juu zaidi ya mataifa mengine aliyoyaumba nanyi mtapokea sifa, umaarufu na heshima. Mtakuwa watu waliowekwa kando kwa Yahwe Mungu wako, kama alivyosema.”
et qu'il te rendra supérieur à toutes les nations qu'il a faites, en gloire, et en renom et en magnificence, et que tu seras un peuple consacré à l'Éternel, ton Dieu, comme Il l'a promis.