< Torati 24 >
1 Mwanamume akimchukua mke na kumuoa, na mke asipokubalika machoni pa mumewe kwa sababu kagundua jambo ambalo si jema kwake, basi anatakiwa amwandikie talaka, aiweke mkononi mwake, na kumfukuza nyumbani kwake.
Kad kāds apņem sievu un ar to iedodas laulībā, un kad tā neatrod žēlastību viņa acīs, tādēļ ka tas to pienācis kādā kauna lietā un viņš raksta šķiršanās grāmatu un to viņai dod rokā un viņu izraida no sava nama,
2 Akishaondoka nyumbani kwake, anaweza kwenda na kuwa mke wa mwanamume mwingine.
Un tā iziet no viņa nama, un paliek citam vīram par sievu,
3 Iwapo mume wa pili akamchukia na kumwandikia talaka, akaiweka mkononi mwake, na kumfukuza nyumbani kwake; au huyu mume wa pili akafariki, mwanamume aliyemchukua kuwa mke wake –
Un kad šis otrs vīrs arīdzan to ienīst un tai raksta šķiršanās grāmatu, un to tai dod rokā un to izraida no sava nama, vai ja tas otrs vīrs mirst, kas to sev par sievu ņēmis,
4 basi mume wa awali, yule aliyemfukuza mara ya kwanza, haruhusiwi kumchukua tena awe mke wake, baada ya yeye kuwa mchafu, kwa maana hiyo itakuwa ni chukizo kwa Yahwe. Hautakiwi kusababisha nchi iwe na hatia, nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupatia kama urithi.
Tad viņas pirmais vīrs, kas to izraidījis, to nevar atkal par sievu ņemt pēc tam, kad tā palikusi netīra; jo tā ir negantība priekš Tā Kunga; tā tev nebūs ar grēkiem apgānīt to zemi, ko Tas Kungs, tavs Dievs, tev dod iemantot.
5 Mwanamume atakapochukua mke mpya, hatakwenda vitani na jeshi, na wala hataamrishwa kwenda kwenye shughuli yoyote ya kulazimishwa; atakuwa huru kuwa nyumbani kwa mwaka mzima na atamfurahisha mke wake aliyemchukua.
Kad kāds apņem jaunu sievu, tam nebūs iet karā un to ne pie kā nebūs piespiest; veselu gadu lai tas ir svabads savā namā un iepriecina savu sievu, ko viņš ir ņēmis. -
6 Mwanamume yeyote hatachukua kinu wala jiwe la kinu kama dhamana, kwa maana hivyo itakuwa kuchukua Maisha ya mtu kama dhamana.
Tev nebūs ķīlā ņemt ne dzirnavas ne dzirnu akmeni, jo tāds apķīlā dzīvību. -
7 Iwapo mwanamume kakutwa kamteka mmoja wa kaka zake miongoni mwa watu wa Israeli, na kumtendea kama mtumwa na kisha kumuuza, huyo mwizi lazima afe; na utakuwa umeondoa uovu miongoni mwenu.
Ja kādu atrod, kas cilvēku zog no saviem brāļiem, no Israēla bērniem un to tur kā vergu un to pārdod, šis zaglis lai mirst, un tev to ļaunumu būs izdeldēt no sava vidus.
8 Kuwa mwangalifu kuhusu kiini chochote cha ukoma, ili kwamba uwe makini katika kuchunguza na kufuata kila agizo linalopewa kwako ambalo makuhani, Walawi, wanakufundisha; kama nilivyowaamuru, ili utekeleze.
Sargies no spitālības, ka tu turi un tikuši(uzmanīgi ikkatru pamācību) dari, kā tie priesteri, tie Leviti, tev mācīs; kā es tiem esmu pavēlējis, tā jums to būs turēt un darīt.
9 Kumbukeni nini Yahwe Mungu wako alichomfanya Miriam ulipokuwa ukitoka Misri.
Piemini, ko Tas Kungs, tavs Dievs, pie Mirjames ir darījis ceļā, kad jūs izgājāt no Ēģiptes zemes. -
10 Utoapo mkopo wa aina yoyote kwa jirani yako, hautakiwi kwenda ndani ya nyumba yake kutafuta dhamana yake.
Kad tu savam tuvākam ko aizdod uz parādu, tad tev nebūs viņa namā iet ķīlas ņemt.
11 Utasimama nje, na mwanamume aliyekopa kwako ataleta dhamana yake nje kwako.
Paliec ārā un lai tas vīrs, kam tu uz parādu esi aizdevis, iznes tās ķīlas pie tevis ārā.
12 Iwapo ni mtu maskini, hautakiwi kulala na dhamana yake ikiwa mikononi mwako.
Bet ja tas ir nabags, tad tev ar viņa ķīlām nebūs iet gulēt,
13 Hakika unapaswa kumrejeshea dhamana yake kabla jua halijazama, ili aweze kulala ndani ya vazi lake na akubariki; itakuwa utakatifu kwako mbele za Yahwe Mungu wako.
Bet atdod viņam tās ķīlas, kad saule noiet, ka tas ar savu apsegu guļ un tevi svētī. Un tas tev būs par taisnību Tā Kunga, tava Dieva, priekšā.
14 Hautakiwi kumuonea mtumishi wa kuajiriwa ambaye ni maskini na mhitaji, hata kama ni jamaa wa Israeli, au ni kati ya wageni mbao wamo katika nchi ndani ya malango ya mji wako;
Neapspiedi bēdīgu nabaga algādzi, lai viņš ir no taviem brāļiem, vai no taviem piedzīvotājiem, kas ir tavā zemē un tavos vārtos.
15 Kila siku unapaswa kumlipa mshahara wake; jua halipaswi kuzama kabla ya suala hili kutatuliwa, kwa maana ni maskini na anautegemea. Fanya hivi ili asilie dhidi yako kwa Yahwe, na kwamba isiwe ikawa dhambi ambayo umeitenda.
Bet to pašu dienu dod tam algu, lai saule pār to nenoiet; jo viņš ir nabags un viņa dvēsele uz to gaida, ka tas par tevi nesauc uz To Kungu un tas tev nav par grēku. -
16 Wazazi hawapaswi kuuwawa kwa niaba ya watoto wao, na wala watoto hawapaswi kuuawa kwa niaba ya wazazi wao. Badala yake, kila mtu anapaswa kuuwawa kwa dhambi yake mwenyewe.
Tēviem nebūs tapt nokautiem dēlu dēļ, un dēliem nebūs tapt nokautiem tēvu dēļ, bet ikvienam būs tapt nokautam savu grēku dēļ.
17 Haupaswi kutumia nguvu kuchukua haki inayomhusu mgeni au yatima, wala kuchukua vazi la mjane kama dhamana.
Nepārgrozi piedzīvotāja un bāriņa tiesu, un neņem ķīlām atraitnes drēbes.
18 Badala yake, unapaswa ukumbuke ya kwamba ulikuwa mtumwa Misri, na kwamba Yahwe Mungu wako alikukomboa kutoka kule. Kwa hiyo ninakuagiza kutii amri hii.
Piemini, ka tu esi bijis kalps Ēģiptes zemē, un ka Tas Kungs, tavs Dievs, tevi no turienes atpestījis; tādēļ es tev pavēlu to darīt.
19 Utakapovuna zao lako shambani mwako, na ukasahau kipande cha mbegu shambani, haupaswi kurudi na kukichukua; kinapaswa kuwa cha mgeni, cha yatima, au cha mjane, ili Yahwe Mungu wako akubariki katika kazi ya mikono yako.
Kad tu savu labību pļausi savā tīrumā, un aizmirsīsi vienu kūlīti tīrumā, tad tev nebūs atgriezties to paņemt, bet lai tas paliek piedzīvotājam, bāriņam un atraitnei, lai Tas Kungs, tavs Dievs, tevi svētī visā tavā rokas darbā.
20 Utakapotikisa mti wako wa mzeituni, haupaswi kupanda juu ya matawi tena; itakuwa kwa ajili ya mgeni, kwa yatima na kwa mjane.
Kad tu savu eļļas koku nokratīsi, tad tev tos zarus nebūs otrreiz pārmeklēt; lai tas paliek piedzīvotājam, bāriņam un atraitnei.
21 Utakapokusanya mizabibu shambani mwako, haupaswi kukusanya masazo yake tena. Kinachobaki kitakuwa cha mgeni, cha yatima na cha mjane.
Kad tu savā vīna dārzā ogas lasīsi, tad tev tās otrreiz nebūs lasīt, bet lai tas paliek piedzīvotājam un bāriņam un atraitnei.
22 Unatakiwa ukumbuke kuwa ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri; kwa hiyo nakuagiza kutii amri hii.
Un piemini, ka tu Ēģiptes zemē esi bijis par kalpu; tāpēc es tev pavēlu to darīt.