< Torati 23 >

1 Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
Да не входит каженик и скопец в сонм Господень.
2 Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
Ниже да внидет блудородный во храм Господень до десятаго рода.
3 Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
Да не внидет Амманитин и Моавитин в храм Господень: и даже до десятаго рода да не входит в храм Господень, и даже до века,
4 Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
понеже не сретоша они вас с хлебы и водою на пути, исходящым вам из земли Египетския, и яко наяша на тя Валаама сына Веорова от Месопотамии, да тя прокленет:
5 Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
и не восхоте Господь Бог твой послушати Валаама, и обрати Господь Бог твой клятвы в благословение, зане возлюби тя Господь Бог твой:
6 Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
да не совещаеши мирная им и полезная им во вся дни твоя во веки.
7 Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
Да не возгнушаешися Идумеанином, яко брат твой есть: да не возгнушаешися Египтянином, яко пришлец был еси в земли его:
8 Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
сынове аще родятся им, в роде третием да внидут в храм Господень.
9 Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
Аще же изыдеши ополчитися на враги твоя, и да сохранишися от всякаго слова зла.
10 Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
Аще будет у тебе человек, иже не будет чист от излияния его нощию, и да изыдет вне полка, и да не внидет в полк:
11 Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
и егда будет к вечеру, да омыет тело свое водою, и зашедшу солнцу да внидет в полк.
12 Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
И место тебе да будет вне полка, и изыдеши тамо вон:
13 na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
и рылец да будет тебе за поясом твоим, и будет егда сядеши вне, и да ископаеши им (яму), и навратив покрыеши стыдение твое в ней:
14 Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
яко Господь Бог твой ходит в полце твоем избавляти тя и предати враги твоя в руце твои пред лицем твоим: и да будет полк твой свят, и да не явится у тебе стыдение вещи, и отвратится от тебе.
15 Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
Да не предаси раба господину его, иже прииде к тебе от господина своего:
16 Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
с тобою да обитает, с вами да живет во всяком месте, идеже угодно будет ему: да не оскорбиши его.
17 Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
Да не будет блудница от дщерей Израилевых, и да не будет блудник от сынов Израилевым.
18 Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
Да не принесеши мзды блудничи, ниже цене песии в дом Господа Бога твоего на всяк обет, яко мерзость суть Господеви Богу твоему и обоя.
19 Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
Да не даси брату твоему в лихву сребра и в лихву пищей и в лихву всякия вещи, емуже аще взаим даси:
20 Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
чуждему да даси в лихву, брату же твоему да не даси в лихву, да благословит тя Господь Бог твой во всех делех твоих на земли, в нюже входиши тамо наследити ю.
21 Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
Аще же обещаеши обет Господеви Богу твоему, да не умедлиши воздати его, яко взыская взыщет Господь Бог твой от тебе, и будет на тебе грех:
22 Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
аще же не восхощеши обещати, несть ти греха.
23 Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
Исходящая на уст твоих сохрани и сотвори, имже образом обещал еси Господеви Богу твоему дар, егоже глаголал еси устами твоими.
24 Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
Аще же внидеши на ниву ближняго своего, и собереши в руце свои класы, а серпа да не возложиши на ниву ближняго.
25 Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.
Аще же внидеши в виноград ближняго своего, да яси гроздие, елико души твоей насытитися, в сосуд же да не вложиши.

< Torati 23 >