< Torati 23 >

1 Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa haruhusiwi kuingia katika kusanyiko la Yahwe.
He that is wounded in the stones, or has his privy member cut off, shall not enter into the congregation of the LORD.
2 Mwana haramu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
A bastard shall not enter into the congregation of the LORD; even to his tenth generation shall he not enter into the congregation of the LORD.
3 Muamori au Mmoabu haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe; kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake, hakuna kati yao anatakiwa kuwa kwenye kusanyiko la Yahwe.
An Ammonite or Moabite shall not enter into the congregation of the LORD; even to their tenth generation shall they not enter into the congregation of the LORD for ever:
4 Hii ni kwa sababu hawakukutana nanyi kwa mkate na maji barabarani mlipokuwa mmetoka nje ya Misri, na kwa sababu walimkodisha Balaamu mwana wa Beoro kutoka Pethoro kule Aramu Naharaimu, awalaani.
Because they met you not with bread and with water in the way, when you came forth out of Egypt; and because they hired against you Balaam the son of Beor of Pethor of Mesopotamia, to curse you.
5 Lakini Yahwe Mungu wako hakumsikiliza Balaamu; badala yake, Yahwe Mungu wako aligeuza laana kuwa baraka kwenu, kwa sababu Yahwe Mungu wako aliwapenda.
Nevertheless the LORD your God would not listen to Balaam; but the LORD your God turned the curse into a blessing to you, because the LORD your God loved you.
6 Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao, katika siku zenu zote.
You shall not seek their peace nor their prosperity all your days for ever.
7 Hutakiwi kumchukia Muedomi, kwa maana ni kaka yako; hutakiwi kumchukia Mmisri, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi yake.
You shall not abhor an Edomite; for he is your brother: you shall not abhor an Egyptian; because you were a stranger in his land.
8 Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe.
The children that are begotten of them shall enter into the congregation of the LORD in their third generation.
9 Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga na kila aina ya uovu.
When the host goes forth against your enemies, then keep you from every wicked thing.
10 Iwapo miongoni mwenu kuna mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku, basi anatakiwa atoke nje ya kambi ya jeshi; hatakiwi kurudi kambini.
If there be among you any man, that is not clean by reason of uncleanness that chances him by night, then shall he go abroad out of the camp, he shall not come within the camp:
11 Jioni ikifika, anatakiwa ajiogeshe kwa maji; na jua likizama atarudi ndani kambini.
But it shall be, when evening comes on, he shall wash himself with water: and when the sun is down, he shall come into the camp again.
12 Pia unatakiwa kuwa na eneo nje ya kambi ambayo utakwenda;
You shall have a place also without the camp, where you shall go forth abroad:
13 na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia; utakapochuchumaa kujisaidia, unapaswa kuchimbia nacho na kisha kurudishia udongo na kufunika kile kilichotoka kwako.
And you shall have a paddle on your weapon; and it shall be, when you will ease yourself abroad, you shall dig therewith, and shall turn back and cover that which comes from you:
14 Kwa maana Yahwe Mungu wako anatembea miongoni mwa kambi yenu kuwapa ushindi na kuwapa maadui zenu mkononi mwenu. Kwa hiyo kambi yenu lazima iwe takatifu, ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu na kuwaacha.
For the LORD your God walks in the middle of your camp, to deliver you, and to give up your enemies before you; therefore shall your camp be holy: that he see no unclean thing in you, and turn away from you.
15 Hutakiwi kumrudishia bwana mtumwa aliyetoroka kwake.
You shall not deliver to his master the servant which is escaped from his master to you:
16 Mruhusu aishi pamoja nawe, katika mji wowote atakaochagua. Usimuonee.
He shall dwell with you, even among you, in that place which he shall choose in one of your gates, where it likes him best: you shall not oppress him.
17 Hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa mabinti wa Israeli, na wala hapatakiwi kuwa na kahaba wa kidhehebu miongoni mwa wana wa kiume wa Israeli.
There shall be no whore of the daughters of Israel, nor a sodomite of the sons of Israel.
18 Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba au mshahara wa mbwa katika nyumba ya Yahwe Mungu wako kwa kiapo chochote; kwa maana vyote hivi na machukizo mbele ya Yahwe Mungu wako.
You shall not bring the hire of a whore, or the price of a dog, into the house of the LORD your God for any vow: for even both these are abomination to the LORD your God.
19 Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba – riba ya fedha, riba ya chakula, au riba ya kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba.
You shall not lend on usury to your brother; usury of money, usury of victuals, usury of any thing that is lent on usury:
20 Kwa mgeni unaweza kukopesha kwa riba; lakini kwa Muisraeli mwenzako haupaswi kukopesha kwa riba, ili kwamba Yahwe Mungu wako aweze kukubariki katika kila jambo uwekalo mkono wako, katika nchi ambayo mnaenda kumiliki.
To a stranger you may lend on usury; but to your brother you shall not lend on usury: that the LORD your God may bless you in all that you set your hand to in the land where you go to possess it.
21 Unapofanya kiapo kwa Yahwe Mungu wako, haupaswi kukawia kuikamilsha, kwa maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho; itakuwa dhambi kako usipokamilisha.
When you shall vow a vow to the LORD your God, you shall not slack to pay it: for the LORD your God will surely require it of you; and it would be sin in you.
22 Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako.
But if you shall forbear to vow, it shall be no sin in you.
23 Kile ambacho kimetoka kinywani mwako unapaswa kukifuata na kukitekeleza; kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako, chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako.
That which is gone out of your lips you shall keep and perform; even a freewill offering, according as you have vowed to the LORD your God, which you have promised with your mouth.
24 Utakapokwenda katika shamba la mizabibu la jirani yako, unatakiwa kula mizabibu idadi yoyote unayotaka, lakini hautakiwi kuhifadhi yoyote katika kikapu chako.
When you come into your neighbor’s vineyard, then you may eat grapes your fill at your own pleasure; but you shall not put any in your vessel.
25 Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako, unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako, lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako.
When you come into the standing corn of your neighbor, then you may pluck the ears with your hand; but you shall not move a sickle to your neighbor’s standing corn.

< Torati 23 >