< Torati 22 >
1 Hautakiwi kumtazama ng’ombe au kondoo wa Muisraeli mwenzako akikosea njia na ukajificha kwao; hakika unapaswa kuwarejesha kwake.
Vola svojega brata ali njegovo ovco ne boš gledal zaiti in se skril pred njimi. V vsakem primeru jih boš ponovno privedel k svojemu bratu.
2 Iwapo Muisraeli mwenzako hayupo karibu nawe, au kama haumfahamu, basi unapaswa kumleta mnyama huyo nyumbani kwako, na lazima uwe naye mpaka pale mwenyewe atakapomtafuta, na kisha lazima umrejeshee mwenyewe.
Če tvoj brat ni blizu tebe ali če ga ne poznaš, potem jo boš privedel v svojo lastno hišo in ta bo s teboj, dokler je tvoj brat ne gre iskat in mu jo boš ponovno vrnil.
3 Unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa punda wake; unapaswa kufanya vivyo hivyo na vazi lake; unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa kila kitu alichopoteza Muisraeli mwenzako, kitu chochote alichopoteza na ukakipata; hautakiwi kujificha.
Na podoben način boš storil z njegovim oslom in tako boš storil z njegovim oblačilom in z vsemi izgubljenimi stvarmi svojega brata, ki jih je izgubil in si jih našel, boš podobno storil. Ne smeš se skriti.
4 Haupaswi kumwona punda wa Muisraeli mwenzako au ng’ombe wake kaanguka chini barabarani na kujificha dhidi yao; hakika unapaswa kumsaidia kumwinua tena.
Osla svojega brata ali njegovega vola ne boš gledal pasti dol ob poti in se skril pred njima. Zagotovo mu boš pomagal, da jih ponovno dvigne.
5 Mwanamke hatakiwi kuvaa kinachokusudiwa kwa mwanamume, vilevile mwanamume hapaswi kuvaa mavazi ya mwanamke; kwa maana yeyote afanyaye vitu hivi ni chukizo kwa Yahwe Mungu wako.
Ženska ne bo nosila tega, kar pripada moškemu niti moški ne bo oblekel ženskega oblačila, kajti vsi, ki tako delajo, so ogabnost Gospodu, tvojemu Bogu.
6 Iwapo kiota cha ndege kikaonekana barabarani mbele yako, kwenye mti wowote au juu ya ardhi, kikiwa na makinda ya ndege au mayai ndani mwake, na mama yao akiwa juu yao au juu ya mayai, haupaswi kumchukua mama pamoja na makinda au mayai yake.
Če se ptičje gnezdo znajde pred teboj na poti, na kateremkoli drevesu ali na tleh, bodisi so mladiči ali jajca in mati sedi na mladičih ali na jajcih, ne boš vzel samice z mladiči,
7 Hakika unapaswa kumuacha mama aende zake, ila makinda yake unaweza kuyachukua. Tii amri hii ili uenende vyema, na siku zako ziweze kurefushwa.
temveč boš vsekakor pustil mater oditi in k sebi vzel mlade, da bo lahko dobro s teboj in da lahko podaljšaš svoje dni.
8 Ujengapo nyumba mpya, basi unapaswa kujenga kitalu kwa ajili ya paa yako ili usilete damu juu ya nyumba yako mtu akianguka kutoka pale.
Ko gradiš novo hišo, potem boš naredil obzidek za svojo streho, da nad svojo hišo ne privedeš krvi, če katerikoli mož pade od tam.
9 Haupaswi kupanda shamba lako la mizabibu kwa mbegu mbili, ili kwamba mavuno yote yasichukuliwe na sehemu takatifu, mbegu uliyoipanda pamoja na matunda ya mzabibu.
Svojega vinograda ne boš sejal z različnimi semeni, da ne bi bil sad tvojega semena, ki si ga posejal in sad vinograda omadeževan.
10 Haupaswi kulimia ng’ombe na punda kwa pamoja.
Ne boš oral z volom in oslom skupaj.
11 Haupaswi kuvaa kitambaa kilichotengenezwa kwa sufu na kitani kwa pamoja.
Ne boš nosil obleke različnih vrst, kakor iz volne in lanu, skupaj.
12 Unapaswa kutengeneza pindo katika pembe nne za nguo unayoivaa.
Sebi boš naredil rese na štirih četrtinah svoje suknje, s katero se pokrivaš.
13 Iwapo mwanamume kachukua mke, kisha kalala naye, na baadae kumchukia,
Če katerikoli moški vzame ženo in gre noter k njej in jo zasovraži
14 na kisha kumtuhumu kwa vitu vya aibu na kumharibia sifa yake kwa kusema, “Nilimchukua huyu mwanamke, lakini nilipomkaribia sikukuta ushahidi waubikra kwake”.
in da priložnost za opravljanje zoper njo in nadnjo privede zlo ime ter reče: ›Vzel sem to žensko in ko sem prišel k njej, je nisem našel device, ‹
15 Kisha baba na mama mzazi wa binti wanatakiwa kupeleka ushahidi wa ubikra wake kwa wazee mlangoni mwa mji.
potem bosta oče gospodične in njena mati vzela in k starešinam v mestnih velikih vratih prinesla znamenja devištva gospodične
16 Baba wa binti anapaswa kuwaambia wazee, “nilimpatia binti yangu kwa mwanamume huyu awe mkewe, naye anamchukia.
in oče gospodične bo starešinam rekel: ›Svojo hčer sem dal temu možu za ženo, ta pa jo sovraži
17 Tazama, amemtuhumu na vitu vya aibu na kusema, “Sikukuta ushahidi wa ubikra kwa binti yako”. Lakini ushahidi huu hapa wa ubikra wa binti yangu”. Kisha watatandaza shuka mbele ya wazee wa mji.
in glejte, dal je priložnosti za opravljanje zoper njo, rekoč: ›Tvoje hčere nisem našel device.‹ Vendar so to znamenja devištva moje hčere.‹ In obleko bosta razgrnila pred starešinami mesta.
18 Wazee wa mji wanapaswa kumchukua mwanamume huyo na kumuadhibu;
In starešine tega mesta bodo vzele tega moškega in ga kaznovale
19 nao wanapaswa kumtoza faini ya shekeli mia moja ya fedha, na kumpatia baba wa binti, kwa sababu mwanamume kasababisha sifa mbaya kwa bikra wa Israeli. Binti huyu anapaswa kuwa mke wake; mwanamume huyu hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote.
in kaznovali ga bodo s sto šekli srebra in jih dali očetu gospodične, ker je nad Izraelovo devico privedel zlo ime in ona bo njegova žena vse svoje dni. Ne sme je odsloviti.
20 Ila kama jambo hili ni la kweli, kwamba ushahidi wa bikra ya binti haukupatikana,
Toda če je ta stvar resnična in simboli devištva za gospodično niso bili najdeni,
21 basi wanapaswa kumpeleka binti mlangoni kwa baba yake, na kisha wanamume wa mji wake wanatakiwa kumpiga kwa mawe hadi afe, kwa sababu amefanya jambo la aibu katika Israeli, kwa kutenda kama kahaba chini ya nyumba ya baba yake, nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu.
potem bo gospodično privedel ven k vratom hiše njenega očeta in ljudje iz njenega mesta jo bodo kamnali s kamni, da ta umre. Ker je storila neumnost v Izraelu, da igra vlačugo v hiši svojega očeta. Tako boš izmed vas odstranil zlo.
22 Iwapo mwanamume kakutwa analala na mwanamke ambaye ni mke wa mtu, basi wote wanapaswa kufa, mwanamume aliyelala na mwanamke pamoja na mwanamke mwenyewe; nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu.
Če je moški najden, da leži z žensko, poročeno s soprogom, potem bosta oba umrla, oba, tako moški, ki je ležal z žensko, in ženska. Tako boš zlo odstranil iz Izraela.
23 Iwapo kuna msichana bikra, ambaye amechumbiwa na mwanamume, kisha mwanamume mwingine kamkuta mjini na kulala naye,
Če je gospodična, ki je devica, zaročena k soprogu in jo moški najde v mestu in leži z njo,
24 wachukueni wote wawili malangoni mwa mji, na kuwapiga mawe. Unapaswa kumpiga msichana mawe, kwa sababu hakupaza sauti kuomba msaada, ingawa alikuwa ndani ya mji. Unapaswa kumpiga mwanamume mawe, kwa sababu amemwingilia mke wa jirani yake; nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu
potem boš oba privedel ven, k velikim vratom tega mesta in kamnali ju boste s kamenjem, da umreta. Gospodično, ker ni kričala, kljub temu, da je bila v mestu in moškega, ker je ponižal ženo svojega bližnjega. Tako boš izmed sebe odstranil zlo.
25 Lakini kama mwanamume amemkuta msichana aliyechumbiwa shambani, na kama akamkamata na kulala naye, basi mwanamume pekee aliyelala naye ndiye lazima afe.
Toda če moški najde zaročeno gospodično na polju in jo moški prisili in leži z njo, potem naj umre samo moški, ki je ležal z njo.
26 Lakini kwake msichana msifanye chochote; hakuna dhambi inayostahili kifo kwake msichana. Kwa maana suala hili ni kama mwanamume amshambuliapo jirani yake na kumuua.
Toda gospodični ne boš ničesar storil. Tam, na gospodični, ni nobenega greha, vrednega smrti, kajti kakor ko se moški vzdiguje zoper svojega bližnjega in ga ubije, celo takšna je ta zadeva,
27 Kwa maana alimkuta shambani; msichana huyu aliyechumbiwa alipaza sauti, lakini hapakuwa na mtu wa kumuokoa.
kajti našel jo je na polju in zaročena gospodična je vpila, pa ni bilo nikogar, da jo reši.
28 Iwapo mwanamume amemkuta msichana ambaye ni bikra lakini hajachumbiwa, na kama akamkamata na kulala naye, na kama wakagundulika,
Če moški najde gospodično, ki je devica, ki ni zaročena in jo prime in leži z njo in ju najdejo,
29 basi mwanamume aliyelala naye lazima atoe shekeli hamsini za fedha kwa baba wa msichana, naye lazima awe mke wake, kwa sababu amemdhalilisha. Hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote.
tedaj naj moški, ki je ležal z njo, očetu od gospodične izroči petdeset šeklov srebra in ona bo njegova žena; ker jo je ponižal, je vse svoje dni ne sme odsloviti.
30 Mwanamume hapaswi kumchukua mke wa baba yake kama wake; hatakiwi kuchukua haki za ndoa za baba yake.
Mož ne bo vzel žene svojega očeta niti odkril krajca očetovega oblačila.