< Torati 16 >
1 Angalia mwezi wa Abibu, na uishike pasaka ya Yahwe Mungu wako, kwa kuwa katika mwezi wa Abibu Yahwe Mungu wako alikuleta toka Misri usiku.
Observe le mois d'Abib et célèbre la Pâque en l'honneur de Yahvé ton Dieu, car c'est au mois d'Abib que Yahvé ton Dieu t'a fait sortir d'Égypte de nuit.
2 Utamtolea dhabibu ya pasaka Yahwe Mungu wako na baadhi ya mifugo na wanyama kwenye eneo ambalo Yahwe atachagua kama patakatifu pake.
Tu sacrifieras la Pâque à l'Éternel, ton Dieu, du menu et du gros bétail, dans le lieu que l'Éternel choisira pour y faire résider son nom.
3 Hautakula mkate wa chachu pamoja nayo, siku saba utakula mkate usio na chachu, mkate wa mateso; kwa kuwa mlitoka katika nchi ya Misri kwa haraka. Fanya haya katika siku zako zote za maisha yako ili uweze kukumbuka akilini siku mliotoka nchi ya Misri.
Tu ne mangeras pas de pain levé avec elle. Tu mangeras avec lui des pains sans levain pendant sept jours, des pains d'affliction (car tu es sorti du pays d'Égypte en hâte), afin de te souvenir du jour où tu es sorti du pays d'Égypte, tous les jours de ta vie.
4 Hakuna chachu inapaswa kuonekana miongoni mwenu ndani ya mipaka yenu wakati wa siku saba; wala nyama yoyote mnayotoa dhabihu jioni kwa siku ya kwanza inabaki mpaka asubuhi.
Il n'y aura pas de levure avec vous dans tout votre territoire pendant sept jours; et aucune des viandes que vous sacrifierez le premier jour, le soir, ne restera toute la nuit jusqu'au matin.
5 Msitoe dhabihu ya pasaka kati ya malango yenu ya ndani ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa.
Tu ne sacrifieras pas la Pâque dans l'une des portes que l'Éternel, ton Dieu, te donne;
6 Badala yake, toa dhabihu katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kama patakatifu pake. Hapo mtatoa dhabihu ya pasaka jioni wakati jua linazama, kwa wakati huo wa mwaka mlitoka Misri.
mais au lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira pour y faire résider son nom, là tu sacrifieras la Pâque le soir, au coucher du soleil, à l'époque où tu es sorti d'Égypte.
7 Mtapaswa kuichoma na kuila katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua; asubuhi mtageuka na kwenda kwenye mahema yenu.
Tu la feras rôtir et tu la mangeras dans le lieu que choisira Yahvé ton Dieu. Le matin, tu retourneras dans tes tentes.
8 Kwa siku sita mtakula mkate usiotia chachu; katika siku ya saba kutakuwa na kusanyiko makini kwa ajili ya Yahwe Mungu wenu; katika siku hiyo hamtafanya kazi.
Pendant six jours, tu mangeras des pains sans levain. Le septième jour, il y aura une assemblée solennelle en l'honneur de Yahvé, ton Dieu. Tu ne feras aucun travail.
9 Mtahesabu wiki saba kwa ajili yenu; tangu wakati mlipoanza kuweka mundu kwenye nafaka iliyosimama mtapaswa kuanza kuhesabu wiki saba.
Vous compterez pour vous-mêmes sept semaines. A partir du moment où vous commencerez à mettre la faucille sur le grain sur pied, vous commencerez à compter sept semaines.
10 Mtapaswa kushika wiki za sherehe ya Yahwe Mungu wenu pamoja na mchango wa sadaka ya utayari kutoka mkono wako ambayo utatoa, kulingana na Yahwe alivyokubariki.
Vous célébrerez la fête des semaines devant l'Éternel, votre Dieu, avec le tribut d'une offrande volontaire de votre main, que vous donnerez selon la manière dont l'Éternel, votre Dieu, vous bénira.
11 Utafurahi mbele ya Yahwe Mungu wako- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi aliye katika malango yako, na mgeni, yatima, na mjane alio miongoni mwenu, katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kwa ajili ya patakatifu pake.
Tu te réjouiras devant l'Éternel, ton Dieu, toi, ton fils, ta fille, ton serviteur, ta servante, le Lévite qui est dans tes portes, l'étranger, l'orphelin et la veuve qui sont parmi toi, dans le lieu que l'Éternel, ton Dieu, choisira pour y faire résider son nom.
12 Utakumbuka akilini kwamba ulikuwa mtumwa Misri; unapaswa kuangalia na kuzishika amri hizi.
Tu te souviendras que tu as été esclave en Égypte. Tu observeras et tu mettras en pratique ces lois.
13 Unapaswa kushika sherehe za vibanda kwa siku saba baada ya kuwa mmekusanya mavuno toka kwenye sakafu ya mapura na kutoka kwenye kinu chako cha divai.
Tu célébreras la fête des cabanes pendant sept jours, après avoir ramassé ce qui vient de ton aire et de ta cuve.
14 Utafurahi wakati wa sherehe- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi, na mgeni, na yatima na mjane walio ndani ya malango yako.
Tu te réjouiras de ta fête, toi, ton fils, ta fille, ton serviteur, ta servante, le lévite, l'étranger, l'orphelin et la veuve qui sont dans tes portes.
15 Kwa siku saba unapaswa kuangalia sherehe ya Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo Yahwe atachagua, kwa sababu Yahwe Mungu wako atakubariki katika mavuno yako yote na kazi ya mikono yako yote, na unapaswa kuwa na furaha kabisa.
Tu feras une fête à l'Éternel, ton Dieu, pendant sept jours, dans le lieu que l'Éternel choisira, car l'Éternel, ton Dieu, te bénira dans tout ton produit et dans tout le travail de tes mains, et tu seras tout entier dans la joie.
16 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele za Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo atachagua: katika sherehe ya mkate usiotiwa chachu, katika sherehe za wiki, na sherehe ya vibanda; na hawataonekana mbele za Yahwe mikono mitupu;
Trois fois par an, tous tes mâles se présenteront devant l'Éternel, ton Dieu, dans le lieu qu'il choisira: à la fête des pains sans levain, à la fête des semaines et à la fête des kiosques. Ils ne se présenteront pas devant l'Éternel à vide.
17 badala yake, kila mtu atatoa kama awezavyo, kwamba mtajua baraka kwamba Yahwe Mungu wako amekupa.
Chacun donnera selon ses moyens, en fonction de la bénédiction que l'Éternel, ton Dieu, t'a accordée.
18 Unapaswa kufanya waamuzi na maakida ndani ya malango yako ambayo Yahwe Mungu wako anakupa; watachukuliwa toka kila kabila, and watahukumu watu kwa hukumu ya haki.
Tu établiras des juges et des officiers dans toutes tes portes, celles que l'Éternel, ton Dieu, te donne, selon tes tribus, et ils jugeront le peuple avec droiture.
19 Haupaswi kuiondoa haki kwa nguvu; haupaswi kuonesha upendeleo wala kuchukua rushwa, kwa kuwa rushwa upofusha macho ya hekima na kupotosha maneno ya haki.
Tu ne pervertiras pas la justice. Tu ne feras pas preuve de partialité. Tu ne prendras pas de pot-de-vin, car le pot-de-vin aveugle les yeux des sages et pervertit les paroles des justes.
20 Unapaswa kufata baada ya haki, baada ya haki peke yake, ili kwamba uishi na kurithi nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupa.
Tu suivras ce qui est tout à fait juste, afin de vivre et d'hériter du pays que l'Éternel, ton Dieu, te donne.
21 Haupaswi kujitengenezea Asherahi, aina yoyote ya mti, kando ya madhabahu ya Yahwe Mungu wako ambayo utakayojitengenezea.
Tu ne planteras pas d'ashère d'un arbre quelconque à côté de l'autel de Yahvé ton Dieu, que tu te feras toi-même.
22 Wala usijitengenezee jiwe takatifu la nguzo, ambalo Yahwe Mungu wako anachukia.
Tu ne te dresseras pas non plus une pierre sacrée que Yahvé ton Dieu déteste.