< Torati 16 >

1 Angalia mwezi wa Abibu, na uishike pasaka ya Yahwe Mungu wako, kwa kuwa katika mwezi wa Abibu Yahwe Mungu wako alikuleta toka Misri usiku.
Kepe thou the monethe of newe fruytis, and of the bigynnyng of somer, that thou make pask to thi Lord God; for in this monethe thi Lord God ledde thee out of Egipt in the nyyt.
2 Utamtolea dhabibu ya pasaka Yahwe Mungu wako na baadhi ya mifugo na wanyama kwenye eneo ambalo Yahwe atachagua kama patakatifu pake.
And thou schalt offre pask to thi Lord God, of scheep and of oxun, in the place which thi Lord God chees, that his name dwelle there.
3 Hautakula mkate wa chachu pamoja nayo, siku saba utakula mkate usio na chachu, mkate wa mateso; kwa kuwa mlitoka katika nchi ya Misri kwa haraka. Fanya haya katika siku zako zote za maisha yako ili uweze kukumbuka akilini siku mliotoka nchi ya Misri.
Thou schalt not ete `ther ynne breed `diyt with sourdouy; in seuene daies thou schalt ete breed of affliccioun, with out sourdouy, for in drede thou yedist out of Egipt, that thou haue mynde of the dai of thi goyng out of Egipt, in alle the daies of thi lijf.
4 Hakuna chachu inapaswa kuonekana miongoni mwenu ndani ya mipaka yenu wakati wa siku saba; wala nyama yoyote mnayotoa dhabihu jioni kwa siku ya kwanza inabaki mpaka asubuhi.
No thing `diyt with sourdouy schal appere in alle thi termes by seuene daies, and of the fleischis of that that is offrid in the euentid, schal not dwelle in the firste dai in the morewtid.
5 Msitoe dhabihu ya pasaka kati ya malango yenu ya ndani ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa.
Thou schalt not mow offre pask in ech of thi citees whiche thi Lord God schal yyue to thee,
6 Badala yake, toa dhabihu katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kama patakatifu pake. Hapo mtatoa dhabihu ya pasaka jioni wakati jua linazama, kwa wakati huo wa mwaka mlitoka Misri.
but in the place which thi Lord God chees, that his name dwelle there; thou schalt offre pask in the euentid, at the goyng doun of the sunne, whanne thou yedist out of Egipt.
7 Mtapaswa kuichoma na kuila katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua; asubuhi mtageuka na kwenda kwenye mahema yenu.
And thou schalt sethe, and ete, in the place which thi Lord God hath chose, and thou schalt rise in the morewtid of the secunde dai, and thou schalt go in to thi tabernaclis.
8 Kwa siku sita mtakula mkate usiotia chachu; katika siku ya saba kutakuwa na kusanyiko makini kwa ajili ya Yahwe Mungu wenu; katika siku hiyo hamtafanya kazi.
Bi sixe daies thou schalt ete therf breed; and in the seuenthe dai, for it is the gaderyng of thi Lord God, thou schalt not do werk.
9 Mtahesabu wiki saba kwa ajili yenu; tangu wakati mlipoanza kuweka mundu kwenye nafaka iliyosimama mtapaswa kuanza kuhesabu wiki saba.
Thou schalt noumbre to thee seuene woukis, fro that dai in which thou settidist a sikil in to the corn;
10 Mtapaswa kushika wiki za sherehe ya Yahwe Mungu wenu pamoja na mchango wa sadaka ya utayari kutoka mkono wako ambayo utatoa, kulingana na Yahwe alivyokubariki.
and thou schalt halewe the feeste dai of woukis to thi Lord God, a wilful offryng of thyn hond, which thou schalt offre by the blessing of thi Lord God.
11 Utafurahi mbele ya Yahwe Mungu wako- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi aliye katika malango yako, na mgeni, yatima, na mjane alio miongoni mwenu, katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kwa ajili ya patakatifu pake.
And thou schalt ete bifore thi Lord God, thou, and thi sone, and thi douytir, and thi seruaunt, and thin handmayde, and the dekene which is with ynne thi yatis, and the comelynge, and the fadirles ethir modirles child, and the widue, that dwellen with you, in the place `which thi Lord God chees that his name dwelle there.
12 Utakumbuka akilini kwamba ulikuwa mtumwa Misri; unapaswa kuangalia na kuzishika amri hizi.
And thou schalt haue mynde for thou were seruaunt in Egipt, and thou schalt kepe and do tho thingis that ben comaundid.
13 Unapaswa kushika sherehe za vibanda kwa siku saba baada ya kuwa mmekusanya mavuno toka kwenye sakafu ya mapura na kutoka kwenye kinu chako cha divai.
And thou schalt halewe the solempnytee of tabernaclis bi seuene daies, whanne thou hast gaderid thi fruytis of the cornfloor, and pressour.
14 Utafurahi wakati wa sherehe- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi, na mgeni, na yatima na mjane walio ndani ya malango yako.
And thou schalt ete in thi feeste dai, thou, and thi sone, and douytir, and thi seruaunt, and handmayde, also the dekene, and comelyng, and the fadirles ether modirles child, and the widewe, that ben with ynne thi yatis, `schulen ete.
15 Kwa siku saba unapaswa kuangalia sherehe ya Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo Yahwe atachagua, kwa sababu Yahwe Mungu wako atakubariki katika mavuno yako yote na kazi ya mikono yako yote, na unapaswa kuwa na furaha kabisa.
Bi seuene daies thou schalt halewe feestis to thi Lord God, in the place which the Lord chees; and thi Lord God schal blesse thee, in alle thi fruytis, and in al the werk of thin hondis, and thou schalt be in gladnesse.
16 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele za Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo atachagua: katika sherehe ya mkate usiotiwa chachu, katika sherehe za wiki, na sherehe ya vibanda; na hawataonekana mbele za Yahwe mikono mitupu;
In thre tymes bi the yeer al thi male kynde schal appere in the siyt of thi Lord, in the place which he chees, in the solempnyte of therf looues, and in the solempnyte of woukis, and in the solempnyte of tabernaclis. A man schal not appere voide bifor the Lord;
17 badala yake, kila mtu atatoa kama awezavyo, kwamba mtajua baraka kwamba Yahwe Mungu wako amekupa.
but ech man schal offre vpe this that he hath, bi the blessyng of his Lord God, which he yaf to `that man.
18 Unapaswa kufanya waamuzi na maakida ndani ya malango yako ambayo Yahwe Mungu wako anakupa; watachukuliwa toka kila kabila, and watahukumu watu kwa hukumu ya haki.
Thou schalt ordeyne `iugis, and maystris, in alle thi yatis whiche thi Lord God schal yyue to thee, bi ech of thi lynagis, that thei deme the puple bi iust doom,
19 Haupaswi kuiondoa haki kwa nguvu; haupaswi kuonesha upendeleo wala kuchukua rushwa, kwa kuwa rushwa upofusha macho ya hekima na kupotosha maneno ya haki.
and bowe not in `to the tother part for fauour, ethir yifte `ayens equete. Thou schalt not take persoone nether yiftis, for whi yiftis blynden the iyen of wise men, `and chaungen the wordis of iust men.
20 Unapaswa kufata baada ya haki, baada ya haki peke yake, ili kwamba uishi na kurithi nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupa.
Thou schalt pursue iustli that that is iust, that thou lyue and welde the lond which thi Lord God schal yyue to thee.
21 Haupaswi kujitengenezea Asherahi, aina yoyote ya mti, kando ya madhabahu ya Yahwe Mungu wako ambayo utakayojitengenezea.
Thou schalt not plaunte a wode, and ech tre bi the auter of thi Lord God;
22 Wala usijitengenezee jiwe takatifu la nguzo, ambalo Yahwe Mungu wako anachukia.
nether thou schalt make to thee, and ordeyne an ymage; whiche thingis thi Lord God hatith.

< Torati 16 >