< Torati 16 >

1 Angalia mwezi wa Abibu, na uishike pasaka ya Yahwe Mungu wako, kwa kuwa katika mwezi wa Abibu Yahwe Mungu wako alikuleta toka Misri usiku.
Observe the month of Abib, and prepare the passover-sacrifice unto the Lord thy God; for in the month of Abib did the Lord thy God bring thee forth out of Egypt by night.
2 Utamtolea dhabibu ya pasaka Yahwe Mungu wako na baadhi ya mifugo na wanyama kwenye eneo ambalo Yahwe atachagua kama patakatifu pake.
And thou shalt sacrifice the passover-offering unto the Lord thy God of sheep and oxen, in the place which the Lord will choose to let his name dwell there.
3 Hautakula mkate wa chachu pamoja nayo, siku saba utakula mkate usio na chachu, mkate wa mateso; kwa kuwa mlitoka katika nchi ya Misri kwa haraka. Fanya haya katika siku zako zote za maisha yako ili uweze kukumbuka akilini siku mliotoka nchi ya Misri.
Thou shalt not eat therewith any leavened bread: seven days shalt thou eat therewith unleavened bread, the bread of affliction; for in haste didst thou go forth out of the land of Egypt; in order that thou mayest remember the day of thy going forth out of the land of Egypt all the days of thy life.
4 Hakuna chachu inapaswa kuonekana miongoni mwenu ndani ya mipaka yenu wakati wa siku saba; wala nyama yoyote mnayotoa dhabihu jioni kwa siku ya kwanza inabaki mpaka asubuhi.
And there shall not be seen with thee any leaven in all thy borders seven days: neither shall there any of the flesh, which thou sacrificedst in the evening, on the first day, remain all night until the morning.
5 Msitoe dhabihu ya pasaka kati ya malango yenu ya ndani ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa.
Thou mayest not slay the passover within any of thy gates, which the Lord thy God giveth thee;
6 Badala yake, toa dhabihu katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kama patakatifu pake. Hapo mtatoa dhabihu ya pasaka jioni wakati jua linazama, kwa wakati huo wa mwaka mlitoka Misri.
But at the place which the Lord thy God will choose to let his name dwell in, there shalt thou slay the passover at evening, at the going down of the sun, at the season that thou camest forth out of Egypt.
7 Mtapaswa kuichoma na kuila katika eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua; asubuhi mtageuka na kwenda kwenye mahema yenu.
And thou shalt roast and eat it in the place which the Lord thy God will choose; and thou shalt turn in the morning, and go unto thy tents.
8 Kwa siku sita mtakula mkate usiotia chachu; katika siku ya saba kutakuwa na kusanyiko makini kwa ajili ya Yahwe Mungu wenu; katika siku hiyo hamtafanya kazi.
Six days shalt thou eat unleavened bread; and on the seventh day shall be a solemn assembly to the Lord thy God: thou shalt do no work.
9 Mtahesabu wiki saba kwa ajili yenu; tangu wakati mlipoanza kuweka mundu kwenye nafaka iliyosimama mtapaswa kuanza kuhesabu wiki saba.
Seven weeks shalt thou number unto thyself: from the time thou beginnest to put the sickle to the corn, shalt thou begin to number seven weeks.
10 Mtapaswa kushika wiki za sherehe ya Yahwe Mungu wenu pamoja na mchango wa sadaka ya utayari kutoka mkono wako ambayo utatoa, kulingana na Yahwe alivyokubariki.
And thou shalt keep the feast of weeks unto the Lord thy God with a tribute of a freewill-offering of thy hand, which thou shalt give: according as the Lord thy God shall have blessed thee.
11 Utafurahi mbele ya Yahwe Mungu wako- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi aliye katika malango yako, na mgeni, yatima, na mjane alio miongoni mwenu, katika eneo ambalo Yahwe Mungu wako atachagua kwa ajili ya patakatifu pake.
And thou shalt rejoice before the Lord thy God, thou, and thy son, and thy daughter, and thy man-servant, and thy maid-servant, and the Levite that is within thy gates, and the stranger, and the fatherless, and the widow, that are in the midst of thee, in the place which the Lord thy God will choose to let his name dwell there.
12 Utakumbuka akilini kwamba ulikuwa mtumwa Misri; unapaswa kuangalia na kuzishika amri hizi.
And thou shalt remember that thou hast been a bond-man in Egypt; and thou shalt observe and do these statutes.
13 Unapaswa kushika sherehe za vibanda kwa siku saba baada ya kuwa mmekusanya mavuno toka kwenye sakafu ya mapura na kutoka kwenye kinu chako cha divai.
The feast of tabernacles shalt thou hold for thyself seven days, when thou hast gathered in the produce of thy threshing-floor and of thy wine-press:
14 Utafurahi wakati wa sherehe- wewe, kijana wako, binti wako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi, na mgeni, na yatima na mjane walio ndani ya malango yako.
And thou shalt rejoice on thy feast, thou, and thy son, and thy daughter, and thy man-servant, and thy maid-servant, and the Levite, and the stranger, and the fatherless, and the widow, that are within thy gates.
15 Kwa siku saba unapaswa kuangalia sherehe ya Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo Yahwe atachagua, kwa sababu Yahwe Mungu wako atakubariki katika mavuno yako yote na kazi ya mikono yako yote, na unapaswa kuwa na furaha kabisa.
Seven days shalt thou keep a solemn feast unto the Lord thy God in the place which the Lord will choose; because the Lord thy God will bless thee in all thy product, and in all the work of thy hands, and thou shalt only rejoice.
16 Mara tatu kwa mwaka wanaume wako wote wanapaswa kuonekana mbele za Yahwe Mungu wako katika eneo ambalo atachagua: katika sherehe ya mkate usiotiwa chachu, katika sherehe za wiki, na sherehe ya vibanda; na hawataonekana mbele za Yahwe mikono mitupu;
Three times in the year shall every one of thy males appear before the Lord thy God in the place which he will choose: on the feast of unleavened bread, and on the feast of weeks, and on the feast of tabernacles; and no one shall appear before the Lord empty;
17 badala yake, kila mtu atatoa kama awezavyo, kwamba mtajua baraka kwamba Yahwe Mungu wako amekupa.
Every man according to what his hand can give, according to the blessing of the Lord thy God which he hath given thee.
18 Unapaswa kufanya waamuzi na maakida ndani ya malango yako ambayo Yahwe Mungu wako anakupa; watachukuliwa toka kila kabila, and watahukumu watu kwa hukumu ya haki.
Judges and officers shalt thou appoint unto thyself in all thy gates, which the Lord thy God giveth thee, throughout thy tribes: and they shall judge the people with a just judgment.
19 Haupaswi kuiondoa haki kwa nguvu; haupaswi kuonesha upendeleo wala kuchukua rushwa, kwa kuwa rushwa upofusha macho ya hekima na kupotosha maneno ya haki.
Thou shalt not wrest judgment; thou shalt not respect persons, and thou shalt not take a bribe; for the bribe blindeth the eyes of the wise, and perverteth the words of the righteous.
20 Unapaswa kufata baada ya haki, baada ya haki peke yake, ili kwamba uishi na kurithi nchi ambayo Yahwe Mungu wako anakupa.
Justice, only justice shalt thou pursue; in order that thou mayest live, and retain possession of the land which the Lord thy God giveth thee.
21 Haupaswi kujitengenezea Asherahi, aina yoyote ya mti, kando ya madhabahu ya Yahwe Mungu wako ambayo utakayojitengenezea.
Thou shalt not plant unto thyself a grove, any tree, near the altar of the Lord thy God, which thou shalt make unto thyself.
22 Wala usijitengenezee jiwe takatifu la nguzo, ambalo Yahwe Mungu wako anachukia.
Neither shalt thou set thee up any statue, which the Lord thy God hateth.

< Torati 16 >