< Torati 15 >

1 Kila mwisho wa kila miaka saba, mnapaswa kufuta madeni.
“At the end of seven years you make a release,
2 Hii ni tabia ya ukombozi. Kila mkopeshaji atafuta kile alichompa jirani yake, hata dai kutoka kwa jirani yake au ndugu yake kwa sababu ufutaji wa madeni wa Yahwe umetangazwa.
and this [is] the matter of the release: every owner of a loan [is] to release his hand which he lifts up against his neighbor, he does not exact of his neighbor and of his brother, but has proclaimed a release to YHWH;
3 Kutoka kwa mgeni mnaweza kudai; lakini kwa chochote chenu kilicho na ndugu yenu mnapaswa mkitoe.
of the stranger you may exact, but that which is yours with your brother your hand releases,
4 Hata hivyo, pasiwepo maskini miongoni mwenu (kwa kuwa Yahwe kwa hakika atawabariki kwenye nchi ambayo anawapa kama urithi kumiliki)
except there is an end [when] no poor [are] with you; for YHWH greatly blesses you in the land which your God YHWH is giving to you [for] an inheritance to possess it,
5 kama peke yenu mnasikiliza kwa bidii sauti ya Yahwe Mungu wenu, kuzishika amri zote ambazo anawaamuru leo.
only if you listen diligently to the voice of your God YHWH, to observe to do all this command which I am commanding you today.
6 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu atawabariki, kama alivyowaahidia; mtakopesha mataifa mengi, lakini hamtaazima; mtaongoza juu ya mataifa mengi, lakini hayatawaongoza ninyi.
For your God YHWH has blessed you as He has spoken to you; and you have lent [to] many nations, but you have not borrowed; and you have ruled over many nations, but they do not rule over you.
7 Kama kuna mtu maskini miongoni mwenu, moja wa ndugu zenu, ndani ya malango yenu yoyote kwenye nchi yenu ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa, msifanye migumu mioyo yenu wala kufunga mkono wenu toka kwa ndugu yenu,
When there is with you any poor of one of your brothers, in one of your cities, in your land which your God YHWH is giving to you, you do not harden your heart, nor shut your hand from your needy brother;
8 Lakini mnapaswa hakika kufungua mkono wenu kwake na hakika mkopeshe yeye vya kutosha hitaji lake.
for you certainly open your hand to him, and certainly lend him sufficiency for his lack which he lacks.
9 Muwe makini kutokuwa na wazo ovu au potovu katika moyo wenu, kusema, “Mwaka wa saba, mwaka wa ukombozi u karibu; ili kwamba msiwe wachoyo kuhusiana na ndugu zenu maskini na haumpi chochote; anaweza kumlilia Yahwe kuhusu nyie, na itakuwa dhambi yenu.
Take heed to yourself lest there be a worthless word in your heart, saying, The seventh year [is] near, the year of release; and your eye is evil against your needy brother, and you do not give to him, and he has called to YHWH concerning you, and it has been sin in you;
10 Mnapaswa kwa hakika mmpe, na moyo wenu hampaswi kuhuzunika wakati mnampa, kwa sababu kurudishiwa kwa Yahwe huyu Mungu wenu atawabariki katika kazi zenu zote na katika chochote mnaweka mkono wenu.
you certainly give to him, and your heart is not sad in your giving to him, for because of this thing your God YHWH blesses you in all your works and in every putting forth of your hand;
11 Kwa kuwa maskini kamwe hatakoma kuishi katika nchi, kwa hiyo nakuamuru wewe na kusema, “Unapaswa kwa hakika ufungue mkono wako kwa ndugu yako, kwa mhitaji wako, na kwa maskini wako katika nchi yako.
because the poor does not cease out of the land, therefore I am commanding you, saying, You certainly open your hand to your brother, to your poor and to your needy one in your land.
12 Kama ndugu yako, ni mwebrania wa kiume au mwebrania wa kike, ameuzwa kwako na anakutumikia kwa miaka saba, basi katika mwaka wa saba unapaswa umwache aende zake huru.
When your brother is sold to you, a Hebrew or a Hebrewess, and he has served you [for] six years, then in the seventh year you send him away free from you.
13 Unapomwacha aende zake huru, usimwache aende mkono mtupu.
And when you send him away free from you, you do not send him away empty;
14 Unapaswa kwa ukarimu hutoe kwake kutoka mifugo yako, kutoka pura iliyo chini, na kinu chako cha mvinyo. Kama Yahwe Mungu wako alivyokubariki, unapaswa umpe yeye.
you certainly adorn him from your flock, and from your threshing-floor, and from your wine-vat; you give to him [from] that which your God YHWH has blessed you [with],
15 Unapaswa kukumbuka kwamba ulikuwa mtumwa kwenye nchi ya Misri, na kwamba Yahwe Mungu wako alikukomboa; kwa hiyo ninakuamuru leo kufanya hivi.
and you have remembered that you have been a servant in the land of Egypt, and your God YHWH ransoms you; therefore I am commanding you this thing today.
16 Itakuwa kwamba kama atasema kwako, “Sitaenda mbali yako; kwa sababu anakupenda na nyumba yako, na kwa sababu ni mzuri kwako,
And it has been, when he says to you, I do not go out from you, because he has loved you and your house, because [it is] good for him with you,
17 basi unapaswa kuchukua uma na msukumo kupitia sikio lake kwenye mlango, na atakuwa mtumwa wako milele. Na pia kwa mtumwa wako wa kike utafanya vilevile.
then you have taken the awl, and have put [it] through his ear, and through the door, and he has been a perpetual servant to you; and you also do so to your handmaid.
18 Isionekane kuwa vigumu kwako kumwachia aende zake huru, kwa sababu amekutumikia kwa miaka sita na amekupa mara mbili udhamani wa mtu aliyeajiriwa. Yahwe Mungu wako atakubariki katika yote unayofanya.
It is not hard in your eyes in your sending him away free from you; for [his worth has been] double the hire of a hired worker [when] he has served you six years; and your God YHWH has blessed you in all that you do.
19 Wazao wote wa kwanza wa kiume katika wanyama na mifugo wako unapaswa uwatenge kwa Yahwe Mungu wako. Hautafanya kazi na mzao wa kwanza wa wanyama wako wala kumnyoa mzao wa kwanza wa mfugo wako.
Every firstling that is born in your herd and in your flock—you sanctify the male to your God YHWH; you do not work with the firstling of your ox, nor shear the firstling of your flock;
20 Unapaswa umle mzaliwa wa kwanza mbele ya Yahwe Mungu wako kila mwaka katika eneo ambalo Yahwe atachagua, wewe na nyumba yako.
you eat it before your God YHWH year by year, in the place which YHWH chooses, you and your house.
21 Kama ina kasoro yoyote- kwa mfano, kama ni kilema au kipofu, au ana kasoro yoyote- haupaswi kumtoa dhabihu kwa Yahwe Mungu wako.
And when there is a blemish in it, [or it is] lame or blind, [or has] any evil blemish, you do not sacrifice it to your God YHWH;
22 Utamla ndani ya malango yako; mtu asiye najisi na aliye najisi ni sawa unapaswa kula, kama ungekula paa au kulungu.
you eat it within your gates, the unclean and the clean alike, as the roe and as the deer.
23 Pekee haupaswi kunywa damu yake; unapaswa kuimwanga damu yake juu ya ardhi kama maji.
Only, you do not eat its blood—you pour it on the earth as water.”

< Torati 15 >