< Torati 14 >
1 Ninyi ni watu wa Yahwe Mungu wenu. Msijikate wenyewe, wala kunyoa sehemu za nyuso zenu kwa ajili ya wafu.
All of you are the children of the LORD your God: all of you shall not cut yourselves, nor make any baldness between your eyes for the dead.
2 Kwa kuwa mu taifa lilowekwa wakfu kwa Yahwe Mungu wenu, na Yahwe amewachagua kuwa watu kwa ajili ya urithi wake, zaidi kuliko watu wote walio juu ya uso wa dunia.
For you are an holy people unto the LORD your God, and the LORD has chosen you to be an exclusive people unto himself, above all the nations that are upon the earth.
3 Hampaswi kula kitu chochote kilicho chukizo.
You shall not eat any abominable thing.
4 Hawa ni wanyama ambao mnaweza kula: ng'ombe, kondoo, mbuzi,
These are the beasts which all of you shall eat: the ox, the sheep, and the goat,
5 kulungu, paa, kulungu wa kiume, mbuzi wa mwituni, paa mweupe na pofu na kondoo wa mlimani
The hart, and the roebuck, and the fallow deer, and the wild goat, and the pygarg, and the wild ox, and the chamois.
6 Mnaweza kula wanyama wowote ambao wamegawanyika kwato, ambaye ana kwato zilizogawanyika mara mbili, na utafuna macheuo.
And every beast that parts the hoof, and cleaves the cleft into two claws, and chews the cud among the beasts, that all of you shall eat.
7 Hata hivyo, hampaswi kula baadhi ya wanyama ambao utafuna macheuo au ambao wana kwato zilizogawanyika mara mbili: ngamia, sungura, pomono, kwa sababu watafuna macheuo lakini hawajagawanyika kwato, ni najisi kwenu.
Nevertheless these all of you shall not eat of them that chew the cud, or of them that divide the cloven hoof; as the camel, and the hare, and the coney: for they chew the cud, but divide not the hoof; therefore they are unclean unto you.
8 Nguruwe ni najisi kwenu pia kwa sababu amegawanyika kwato lakini hatafuni macheuo; ni najisi kwenu. Msile nyama ya nguruwe, na msiguse mizoga yao.
And the swine, because it divides the hoof, yet chews not the cud, it is unclean unto you: all of you shall not eat of their flesh, nor touch their dead carcass.
9 Haya yaliyo ndani ya maji mnaweza kula: chochote kilicho na mapesi na magamba;
These all of you shall eat of all that are in the waters: all that have fins and scales shall all of you eat:
10 lakini chochote kisichokuwa na mapesi na magamba msile; ni najisi kwenu.
And whatsoever has not fins and scales all of you may not eat; it is unclean unto you.
11 Ndege wote safi mnaweza kula.
Of all clean birds all of you shall eat.
12 Lakini hawa ni ndege ambao hampaswi kula: tai, tumbusi, kipungu,
But these are they of which all of you shall not eat: the eagle, and the vulture, and the buzzard,
13 mwewe mwekundu na mweusi, aina yoyote ya kipanga.
And the vulture, and the kite, and the vulture after his kind,
14 Hampaswi kula aina yoyote ya kunguru,
And every raven after his kind,
15 na mbuzi na mwewe wa usiku, Lanes ndege wa baharini, aina yoyote ya mwewe,
And the owl, and the night hawk, and the cuckoo, and the hawk after his kind,
16 bundi mdogo, bundi mkubwa, na bundi mweupe,
The little owl, and the great owl, and the swan,
17 Mwari, nyamafu ya tai, mnandio.
And the pelican, and the carrion vulture, and the cormorant,
18 Hampaswi kula korongo, aina yoyote ya kongoti, hudihudi, na popo.
And the stork, and the heron after her kind, and the lapwing, and the bat.
19 Wote wenye mabawa; vitu vya utando ni najisi kwenu; havipaswi kuliwa.
And every creeping thing that flies is unclean unto you: they shall not be eaten.
20 Mnaweza kula vitu vyote virukavyo.
But of all clean fowls all of you may eat.
21 Hampaswi kula chochote kinachokufa chenyewe; mnaweza kumpa mgeni ambaye yuko katika mji wenu, kwamba anaweza kula au mnaweza kuuza kwa mgeni. Kwa kuwa mu taifa lilolowekwa wakfu kwa ajili ya Yahwe Mungu wenu. Hampaswi kumchemusha mbuzi kijana katika maziwa ya mama yake.
All of you shall not eat of anything that dies of itself: you shall give it unto the stranger that is in your gates, that he may eat it; or you may sell it unto an foreigner: for you are an holy people unto the LORD your God. You shall not seethe a kid in his mother's milk.
22 Hakika mnapaswa kutoa fungu la kumi la mavuno ya mbegu zenu zote, ambazo huja kutoka kwenye shamba kila mwaka.
You shall truly tithe all the increase of your seed, that the field brings forth year by year.
23 Mnapaswa kula mbele ya Yahwe Mungu wenu, katika eneo ambalo atachagua kama patakatifu pake, fungu la kumi la nafaka zenu, za mvinyo mpya, na mafuta yenu, na mzaliwa wa kwanza wa wanyama na mifugo, kwamba mnaweza kujifunza daima kumheshimu Yahwe Mungu wenu.
And you shall eat before the LORD your God, in the place which he shall choose to place his name there, the tithe of your corn, of your wine, and of your oil, and the firstlings of your herds and of your flocks; that you may learn to fear the LORD your God always.
24 Kama safari ni ndefu kwenu na kwamba hamwezi kuibeba, kwa sababu eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kama patakatifu pake ni mbali kwenu, basi, wakati Yahwe Mngu anawabariki,
And if the way be too long for you, so that you are not able to carry it; or if the place be too far from you, which the LORD your God shall choose to set his name there, when the LORD your God has blessed you:
25 mtabadilisha sadaka katika pesa. Fungeni pesa kwenye mkono, na nendeni kwenye eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua.
Then shall you turn it into money, and bind up the money in your hand, and shall go unto the place which the LORD your God shall choose:
26 Huko mtatumia pesa kwa chochote mnatamani kwa ng'ombe au kondoo, au kwa mvinyo, au kwa kinywaji imara, au kwa chochote mnatamani; mtakula hapo mbele ya Yahwe Mungu wenu, na mtafurahi, nyie na nyumba zenu.
And you shall bestow that money for whatsoever your soul lusts after, for oxen, or for sheep, or for wine, or for strong drink, or for whatsoever your soul desires: and you shall eat there before the LORD your God, and you shall rejoice, you, and your household,
27 Mlawi ambaye yuko malangoni mwenu- msimsahau, kwa kuwa hana sehemu wala urithi pamoja nanyi.
And the Levite that is within your gates; you shall not forsake him; for he has no part nor inheritance with you.
28 Mwisho mwa kila miaka mitatu mtawasilisha mafungu yote ya kumi ya mazao kwa mwaka huo huo, na mtatunza katika malango yenu;
At the end of three years you shall bring forth all the tithe of your increase the same year, and shall lay it up within your gates:
29 na Mlawi, kwa sababu hana sehemu wala urithi pamoja nanyi, na mgeni, na yatima, na wajane walio ndani ya malango yenu, watakuja na kula na kurithika. Fanya hivyo kwa Yahwe Mungu wenu aweze kuwabariki katika kazi zote za mikono yenuo mnazofanya.
And the Levite, (because he has no part nor inheritance with you, ) and the stranger, and the fatherless, and the widow, which are within your gates, shall come, and shall eat and be satisfied; that the LORD your God may bless you in all the work of your hand which you do.