< Torati 14 >

1 Ninyi ni watu wa Yahwe Mungu wenu. Msijikate wenyewe, wala kunyoa sehemu za nyuso zenu kwa ajili ya wafu.
You are sons of the LORD your God; do not cut yourselves or shave your foreheads on behalf of the dead,
2 Kwa kuwa mu taifa lilowekwa wakfu kwa Yahwe Mungu wenu, na Yahwe amewachagua kuwa watu kwa ajili ya urithi wake, zaidi kuliko watu wote walio juu ya uso wa dunia.
for you are a people holy to the LORD your God. The LORD has chosen you to be a people for His prized possession out of all the peoples on the face of the earth.
3 Hampaswi kula kitu chochote kilicho chukizo.
You must not eat any detestable thing.
4 Hawa ni wanyama ambao mnaweza kula: ng'ombe, kondoo, mbuzi,
These are the animals that you may eat: The ox, the sheep, the goat,
5 kulungu, paa, kulungu wa kiume, mbuzi wa mwituni, paa mweupe na pofu na kondoo wa mlimani
the deer, the gazelle, the roe deer, the wild goat, the ibex, the antelope, and the mountain sheep.
6 Mnaweza kula wanyama wowote ambao wamegawanyika kwato, ambaye ana kwato zilizogawanyika mara mbili, na utafuna macheuo.
You may eat any animal that has a split hoof divided in two and that chews the cud.
7 Hata hivyo, hampaswi kula baadhi ya wanyama ambao utafuna macheuo au ambao wana kwato zilizogawanyika mara mbili: ngamia, sungura, pomono, kwa sababu watafuna macheuo lakini hawajagawanyika kwato, ni najisi kwenu.
But of those that chew the cud or have a completely divided hoof, you are not to eat the following: the camel, the rabbit, or the rock badger. Although they chew the cud, they do not have a divided hoof. They are unclean for you,
8 Nguruwe ni najisi kwenu pia kwa sababu amegawanyika kwato lakini hatafuni macheuo; ni najisi kwenu. Msile nyama ya nguruwe, na msiguse mizoga yao.
as well as the pig; though it has a divided hoof, it does not chew the cud. It is unclean for you. You must not eat its meat or touch its carcass.
9 Haya yaliyo ndani ya maji mnaweza kula: chochote kilicho na mapesi na magamba;
Of all the creatures that live in the water, you may eat anything with fins and scales,
10 lakini chochote kisichokuwa na mapesi na magamba msile; ni najisi kwenu.
but you may not eat anything that does not have fins and scales; it is unclean for you.
11 Ndege wote safi mnaweza kula.
You may eat any clean bird,
12 Lakini hawa ni ndege ambao hampaswi kula: tai, tumbusi, kipungu,
but these you may not eat: the eagle, the bearded vulture, the black vulture,
13 mwewe mwekundu na mweusi, aina yoyote ya kipanga.
the red kite, the falcon, any kind of kite,
14 Hampaswi kula aina yoyote ya kunguru,
any kind of raven,
15 na mbuzi na mwewe wa usiku, Lanes ndege wa baharini, aina yoyote ya mwewe,
the ostrich, the screech owl, the gull, any kind of hawk,
16 bundi mdogo, bundi mkubwa, na bundi mweupe,
the little owl, the great owl, the white owl,
17 Mwari, nyamafu ya tai, mnandio.
the desert owl, the osprey, the cormorant,
18 Hampaswi kula korongo, aina yoyote ya kongoti, hudihudi, na popo.
the stork, any kind of heron, the hoopoe, or the bat.
19 Wote wenye mabawa; vitu vya utando ni najisi kwenu; havipaswi kuliwa.
All flying insects are unclean for you; they may not be eaten.
20 Mnaweza kula vitu vyote virukavyo.
But you may eat any clean bird.
21 Hampaswi kula chochote kinachokufa chenyewe; mnaweza kumpa mgeni ambaye yuko katika mji wenu, kwamba anaweza kula au mnaweza kuuza kwa mgeni. Kwa kuwa mu taifa lilolowekwa wakfu kwa ajili ya Yahwe Mungu wenu. Hampaswi kumchemusha mbuzi kijana katika maziwa ya mama yake.
You are not to eat any carcass; you may give it to the foreigner residing within your gates, and he may eat it, or you may sell it to a foreigner. For you are a holy people belonging to the LORD your God. You must not cook a young goat in its mother’s milk.
22 Hakika mnapaswa kutoa fungu la kumi la mavuno ya mbegu zenu zote, ambazo huja kutoka kwenye shamba kila mwaka.
You must be sure to set aside a tenth of all the produce brought forth each year from your fields.
23 Mnapaswa kula mbele ya Yahwe Mungu wenu, katika eneo ambalo atachagua kama patakatifu pake, fungu la kumi la nafaka zenu, za mvinyo mpya, na mafuta yenu, na mzaliwa wa kwanza wa wanyama na mifugo, kwamba mnaweza kujifunza daima kumheshimu Yahwe Mungu wenu.
And you are to eat a tenth of your grain, new wine, and oil, and the firstborn of your herds and flocks, in the presence of the LORD your God at the place He will choose as a dwelling for His Name, so that you may learn to fear the LORD your God always.
24 Kama safari ni ndefu kwenu na kwamba hamwezi kuibeba, kwa sababu eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kama patakatifu pake ni mbali kwenu, basi, wakati Yahwe Mngu anawabariki,
But if the distance is too great for you to carry that with which the LORD your God has blessed you, because the place where the LORD your God will choose to put His Name is too far away,
25 mtabadilisha sadaka katika pesa. Fungeni pesa kwenye mkono, na nendeni kwenye eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua.
then exchange it for money, take the money in your hand, and go to the place the LORD your God will choose.
26 Huko mtatumia pesa kwa chochote mnatamani kwa ng'ombe au kondoo, au kwa mvinyo, au kwa kinywaji imara, au kwa chochote mnatamani; mtakula hapo mbele ya Yahwe Mungu wenu, na mtafurahi, nyie na nyumba zenu.
Then you may spend the money on anything you desire: cattle, sheep, wine, strong drink, or anything you wish. You are to feast there in the presence of the LORD your God and rejoice with your household.
27 Mlawi ambaye yuko malangoni mwenu- msimsahau, kwa kuwa hana sehemu wala urithi pamoja nanyi.
And do not neglect the Levite within your gates, since he has no portion or inheritance among you.
28 Mwisho mwa kila miaka mitatu mtawasilisha mafungu yote ya kumi ya mazao kwa mwaka huo huo, na mtatunza katika malango yenu;
At the end of every three years, bring a tenth of all your produce for that year and lay it up within your gates.
29 na Mlawi, kwa sababu hana sehemu wala urithi pamoja nanyi, na mgeni, na yatima, na wajane walio ndani ya malango yenu, watakuja na kula na kurithika. Fanya hivyo kwa Yahwe Mungu wenu aweze kuwabariki katika kazi zote za mikono yenuo mnazofanya.
Then the Levite (because he has no portion or inheritance among you), the foreigner, the fatherless, and the widow within your gates may come and eat and be satisfied. And the LORD your God will bless you in all the work of your hands.

< Torati 14 >