< Torati 11 >
1 Kwa hiyo mtampenda Yahwe Mungu wenu na daima mtashika maelekezo yake, maagizo yake, sheria zake, na amri zake.
Thou shalt therefore love the Lord thy God, and keep his charge, and his statutes, and his ordinances, and his commandments, all the days.
2 Kumbuka kwamba siongei kwa watoto wako, ambao hawajajua wala kuona hukumu ya Yahwe Mungu wako, ukuu wake, mkono wake wa uweza, mkono wake ulionyoshwa,
And ye shall know this day, that [I speak] not with your children who have not known, and who have not seen the chastisement of the Lord your God, his greatness, his strong hand, and his outstretched arm;
3 Ishara na matendo ambayo alifanya katikati ya Misri kwa Farao, mfalme Misri, na nchi yake yote.
And his signs, and his acts, which he displayed in the midst of Egypt, unto Pharaoh the king of Egypt, and unto all his land;
4 Wala hawakuona kile alichofanya kwa jeshi la Misri, kwa farasi wao, au magari yao; namna alivyoyafanya maji ya bahari ya Reeds kuwaelemea kwa sababu ya kuwafuatilia, na namna Yahwe alivyowaangamiza mpaka leo,
And what he did unto the army of Egypt, unto its horses, and to its chariots; over whom he caused the water of the Red Sea to flow, as they pursued after you, and whom the Lord destroyed unto this day;
5 au nini alifanya kwenu kwenye jangwa mpaka mlikuja eneo hili.
And what he did unto you in the wilderness, until ye came unto this place;
6 Hawajaona nini Yahwe alichofanya kwa Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Reubeni; namna dunia ilifungua kinywa chake na kuwameza, nyumba zao, mahema yao, na kila kitu hai kilichowafuata, katikati mwa Israeli yote.
And what he did unto Dathan and Abiram, the sons of Eliab, the son of Reuben; how the earth opened her mouth, and swallowed them up, and their households, and their tents, and all the living substance that followed them, in the midst of all Israel;
7 Lakini macho yenu yameona kazi yote kuu ya Yahwe aliyoifanya.
But it is your own eyes which have seen all the great acts of the Lord which he hath done.
8 Kwa hiyo shikeni amri zote ambazo ninawaamuru leo, kwamba mweze kuwa imara, na kuingia na kuimiliki nchi, ambayo unaenda zaidi kuimiliki;
Ye shall therefore keep all the commandment which I command you this day, that ye may be strong, and go in and take possession of the land, whither ye go over to possess it;
9 na kwamba uweze kuongeza siku zako katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako kuwapa na uzao wao, nchi itiririkayo maziwa na asali.
And in order that ye may live many days in the land, which the Lord hath sworn unto your fathers to give unto them and to their seed, a land flowing with milk and honey.
10 Kwa kuwa nchi, ambayo unaingia kumiliki, siyo kama nchi ya Misri, ambako mlitoka, ambako mlipanda mbegu na kumwagilizia kwa miguu yenu, kama bustani ya mitishamba;
For the land, whither thou goest in to possess it, is not like the land of Egypt, from where ye came out, where thou sowest thy seed, and waterest it with thy foot, as a garden of herbs;
11 Lakini nchi, ambayo unaenda kuimiliki, ni nchi ya milima na mabonde, na kunywa maji ya mvua mbinguni,
But the land, whither ye go over to possess it, is a land of mountains and valleys, from the rain of heaven doth it drink water.
12 nchi ambayo Yahwe Mungu wenu awajali; macho ya Yahwe Mungu wenu daima yako juu yake, kuanzia mwanzo wa mwaka mpaka mwisho wa mwaka.
A land which the Lord thy God careth for; always are the eyes of the Lord thy God upon it, from the beginning of the year even unto the end of the year.
13 Itatokea, kama mtazisikiliza kwa bidii amri zangu ambazo ninawaamuru leo kumpenda Yahwe Mungu wenu, na kumtumikia kwa moyo wenu wote na roho zenu zote,
And it shall come to pass, if ye will hearken diligently unto my commandments which I command you this day, to love the Lord your God, and to serve him with all your heart and with all your soul,
14 kwamba nitawapa mvua nchi yenu kwa majira yake, mvua za awali na mvua za badaye, ili kwamba mweze kukusanya nafaka zenu, mvinyo wenu mpya, na mafuta yenu.
That I will send rain for your land in its due season, the first rain and the latter rain, that thou mayest gather in thy corn, and thy wine, and thy oil.
15 Nitawapa nyasi kwenye mashamba yenu kwa ajili ya mifugo yenu, na mtakula na kushiba.
And I will give grass in thy field for thy cattle; and thou shalt eat and be satisfied,
16 Uwe makini mwenyewe, ili kwamba moyo wako usidanganyike, na kugeuka na kuabudu miungu mingine, na kuisujudia;
Take heed to yourselves, that your heart be not deceived, and ye turn aside, and serve other gods, and worship them;
17 ili kwamba hasira ya Yahwe isiwashiwe dhidi yenu, na ili kwamba asifunge mbingu, kwamba pasiwe na mvua, na nchi haitavuna matunda, na ili kwamba mpotee kwa haraka kutoka nchi nzuri ambayo Yahwe anawapa.
[For] then the Lord's wrath will be kindled against you, and he will shut up the heavens that there be no rain, and the land will not yield her products; and ye shall perish quickly from off the good land which the Lord giveth unto you.
18 Kwa hiyo yaweke haya maneno ndani ya moyo wako na roho; yafunge kama ishara kwenye mkono wako, na yawe utepe katikati ya macho yako.
Therefore shall ye lay up these my words in your heart and in your soul; and ye shall bind them for a sign upon your hand, and they shall be as frontlets between your eyes.
19 Utayafundisha kwa watoto na kuongea juu yake wakati uketipo ndani ya nyumba yako, wakati utembeapo barabarani, wakati ulalapo, na wakati uinukapo.
And ye shall teach them to your children, to speak of them when thou sittest in thy house, and when thou walkest by the way, and when thou liest down, and when thou risest up.
20 Utayaandika kwenye miimo ya milango ya nyumba zenu na kwenye malango yenu,
And thou shalt write them upon the door-posts of thy house, and upon thy gates.
21 kwamba siku zenu na siku za watoto wenu ziweze kuongezeka katika nchi ambayo Yahwe aliapa kwa mababu zenu kuwapa, maadamu mbingu ziko juu ya ardhi.
In order that your days may be multiplied, and the days of your children, in the land which the Lord swore unto your fathers to give unto them, as the days of the heavens over the earth.
22 Kama mtayashika kwa bidii maagizo haya yote ambayo ninawaamuru nyinyi, ili kwamba myafanye, mpende Yahwe Mungu wenu, tembea katika njia zake zote, na kushikamana naye,
For if ye will diligently keep all this commandment which I command you, in order to do it, to love the Lord your God, to walk in all his ways, and to cleave unto him:
23 basi Yahwe atawaondosha mataifa haya yote kutoka mbele yenu, na mtayafukuza mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko nyie.
Then will the Lord drive out all these nations from before you, and ye shall supplant nations greater and mightier than yourselves.
24 Kila eneo ambalo unyao wa miguu utatembea litakuwa lenu; kutoka jangwani hadi Lebanoni, toka mto wa Euphratesi, hadi magharibi mwa bahari itakuwa mpaka wenu.
Every place whereon the sole of your foot may tread shall be yours: from the wilderness and the Lebanon, from the river, the river Euphrates, even unto the Western Sea shall be your boundary.
25 Hakuna mtu ataweza kusimama mbele yenu; Yahwe Mungu wenu ataweka hofu yenu na ugaidi wenu juu ya nchi yote mnayotembea juu yake kama alivyosema na ninyi.
There shall no man be able to stand up before you; the dread of you and the fear of you will the Lord your God lay upon all the land which ye may tread upon, as he hath spoken unto you.
26 Tazama, naweka mbele yenu baraka na laana;
Behold, I lay before you this day a blessing and a curse:
27 baraka, kama mtasikiliza amri za Yahwe ambazo ninakuamuru leo,
The blessing, if ye will hearken unto the commandments of the Lord your God, which I command you this day;
28 na laana, kama hamtasikiliza amri za Yahwe Mungu wenu, lakini mkaicha njia ninayokuamuru leo, kuendea miungu mingine ambayo hamjaijua.
And the curse, if ye will not hearken unto the commandments of the Lord your God, and ye turn aside out of the way which I command you this day, to go after other gods, which ye know not.
29 Itakuwa wakati Yahwe Mungu wenu anawaleta ninyi katika nchi ambayo mnaenda kumiliki, kwamba mtaweka baraka juu ya mlima Gerizimu na laana juu ya mlima Ebali.
And it shall come to pass, when the Lord thy God shall have brought thee in unto the land whither thou goest to possess it, that thou shalt put the blessing upon mount Gerizzim, and the curse upon mount 'Ebal.
30 Hawako ng'ambo ya pili zaidi ya Yordani, magharibi mwa barabara la magharibi, katika nchi ya Wakanani wanaoishi Arabah, juu dhidi ya Gilgali, kando ya mialo ya Moreh?
Behold, they are on the other side of the Jordan, far away in the direction of the going down of the sun, in the land of the Canaanites, who dwell in the plain, opposite Gilgal, near the grove of Moreh.
31 Kwa maana mtavuka ng'ambo ya pili ya Yordani kuingia kumiliki nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa, na mtamiliki na kuishi ndani yake.
For ye are about to pass over the Jordan to go in to take possession of the land which the Lord your God giveth you; and ye will possess it, and dwell therein.
32 Mtashika sheria zote na amri ninazoweka mbele yenu leo.
And ye shall then observe to do all the statutes and ordinances which I set before you this day.