< Torati 10 >
1 Kwa wakati ule Yahwe alisema kwangu, 'Chonga mbao mbili za mawe kama zile za kwanza, na njoo kwangu huku juu ya mlima, na utengeneze sanduku la mbao.
At that time the LORD said unto me: 'Hew thee two tables of stone like unto the first, and come up unto Me into the mount; and make thee an ark of wood.
2 Nitaandika kwenye mbao maneno ambayo yalikuwa kwenye mbao za kwanza ulizozivunja, na utaziweka ndani ya sanduku.
And I will write on the tables the words that were on the first tables which thou didst break, and thou shalt put them in the ark.'
3 Basi nilitengeneza sanduku la mbao za mikaratusi, na nikachonga mbao mbili za mawe kwa zile za kwanza, na nikaenda juu ya mlima, nikiwa na mbao mbili mkononi mwangu.
So I made an ark of acacia-wood, and hewed two tables of stone like unto the first, and went up into the mount, having the two tables in my hand.
4 Aliandika kwenye mbao, kama maandishi ya kwanza, amri kumi ambazo Yahwe amesema nanyi kwenye mlima kutoka katikati mwa moto katika siku ya kusanyiko; ndipo Yahwe alilinipa mimi.
And He wrote on the tables according to the first writing, the ten words, which the LORD spoke unto you in the mount out of the midst of the fire in the day of the assembly; and the LORD gave them unto me.
5 Niligeuka na kushuka chini kutoka mlimani, na kuweka mbao ndani ya sanduku nililokuwa nimetengeneza; hapo zilikaa, kama Yahwe alivyoniamuru.”
And I turned and came down from the mount, and put the tables in the ark which I had made; and there they are, as the LORD commanded me. —
6 (Watu wa Israeli walisafiri kutoka Beerothi ya Bene Jaakan kwenda Moserathi. Huko Aaroni alikufa, na huko alizikwa; Eleazar, mwana wake, alitumika katika ofisi ya ukuhani kwenye nafasi yake.
And the children of Israel journeyed from Beeroth-benejaakan to Moserah; there Aaron died, and there he was buried; and Eleazar his son ministered in the priest's office in his stead.
7 Kutokea huko walisafiri kwenda Gudgodah, na kutoka Gudgodah kwenda Jotbathah, nchi yenye mikondo ya maji.
From thence they journeyed unto Gudgod; and from Gudgod to Jotbah, a land of brooks of water. —
8 Kwa wakati huo Yahwe alichagua kabila la Lawi kubeba sanduku la agano la Yahwe, kusimama mbele ya Yahwe kumtumikia na kubariki watu kwa jina lake, kama ilivyo leo.
At that time the LORD separated the tribe of Levi, to bear the ark of the covenant of the LORD, to stand before the LORD to minister unto Him, and to bless in His name, unto this day.
9 Kwa hiyo Lawi hawana sehemu wala urithi wa nchi pamoja na ndugu zake; Yahwe ni urithi wao, kama Yahwe Mungu wenu alizungumza naye)
Wherefore Levi hath no portion nor inheritance with his brethren; the LORD is his inheritance, according as the LORD thy God spoke unto him. —
10 “Nilibaki kwenye mlima kama ilivyokuwa mara ya kwanza, siku arobaini na usiku arobaini. Yahwe alinisikiliza wakati huo pia; Yahwe hakutaka kukuangamiza.
Now I stayed in the mount, as at the first time, forty days and forty nights; and the LORD hearkened unto me that time also; the LORD would not destroy thee.
11 Yahwe alisema nami, “Inuka, nenda mbele ya watu uwaongoze katika safari yao; wataingia na kumiliki nchi ambayo niliapa kwa mababu zao kuwapa.'
And the LORD said unto me: 'Arise, go before the people, causing them to set forward, that they may go in and possess the land, which I swore unto their fathers to give unto them.'
12 Sasa, Israeli, Yahwe Mungu wenu ataka nini kwenu, isipokuwa hofu ya Yahwe Mungu wenu, kutembea katika njia zake zote, kumpenda yeye, na kumwabudu Yahwe Mungu wenu kwa moyo wenu wote na roho yenu yote.
And now, Israel, what doth the LORD thy God require of thee, but to fear the LORD thy God, to walk in all His ways, and to love Him, and to serve the LORD thy God with all thy heart and with all thy soul;
13 Kuzishika amri za Yahwe, na maagizo ambayo ninawaamuru ninyi leo kwa ajili ya uzuri wenu?
to keep for thy good the commandments of the LORD, and His statutes, which I command thee this day?
14 Tazama, kwa Yahwe Mungu wenu mbingu ni zake na mbingu za mbingu, dunia, vyote vilivyomo.
Behold, unto the LORD thy God belongeth the heaven, and the heaven of heavens, the earth, with all that therein is.
15 Yahwe peke alichukua furaha kwa baba zenu ili kwamba awapende, na aliwachagua ninyi, wazao wao, baada yao, zaidi kuliko ya watu wengine wowote, kama afanyavyo leo.
Only the LORD had a delight in thy fathers to love them, and He chose their seed after them, even you, above all peoples, as it is this day.
16 Kwa hiyo basi wataili govi la mioyo yao, na msiwe wakaidi tena.
Circumcise therefore the foreskin of your heart, and be no more stiffnecked.
17 Kwa kuwa Yahwe Mungu wenu, ni Mungu wa miungu na Bwana wa bwana, Mungu mkuu, mwenye nguvu na wakutisha, ambaye hapendelei yeyote na hapokei rushwa-
For the LORD your God, He is God of gods, and Lord of lords, the great God, the mighty, and the awful, who regardeth not persons, nor taketh reward.
18 Hutekeleza haki kwa yatima na wajane, na huonesha upendo kwa mgeni kwa kumpa chakula na mavazi.
He doth execute justice for the fatherless and widow, and loveth the stranger, in giving him food and raiment.
19 Kwa hiyo basi mpende mgeni; kwa kuwa mlikuwa wageni kutoka nchi ya Misri.
Love ye therefore the stranger; for ye were strangers in the land of Egypt.
20 Mtamche Yahwe Mungu wenu yeye mtamwabudu. Mtashikamana kwake, na kwa jina lake mtaapa.
Thou shalt fear the LORD thy God; Him shalt thou serve; and to Him shalt thou cleave, and by His name shalt thou swear.
21 Yeye ni sifa yenu, ni Mungu wenu, ambaye amefanya kwa ajili yenu haya mambo makuu na kutisha, ambayo macho yenu yameyaona.
He is thy glory, and He is thy God, that hath done for thee these great and tremendous things, which thine eyes have seen.
22 Baba zako walienda Misri kama watu sabini; sasa Yahwe Mungu wako amekufanya wewe kuwa wengi kama nyota za mbinguni.
Thy fathers went down into Egypt with threescore and ten persons; and now the LORD thy God hath made thee as the stars of heaven for multitude.