< Torati 1 >

1 Haya ni maneno ambayo Musa aliyasema kwa Israeli wote ng'ambo ya jangwa la Yordani, katika tambarare ya mto wa Yordani juu ya Suph, katikati mwa Paran, Topheli, Laban, Hazeroth, na Di Zahab.
These ben the wordis whiche Moyses spak to al Israel ouer Jordan, in the wildirnesse of the feeld, ayens the reed see, bitwix Pharan and Tophel and Laban and Asseroth, where is ful myche gold,
2 Ni safari ya siku kumi na moja toka Horabu kupitia njia ya mlima wa Seir kwenda Kadeshi Barnea.
by enleuene daies fro Oreb bi the weie of the hil of Seir, til to Cades Barne.
3 Ilitokea kwenye mwaka wa nne, mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, Musa alizungumza kwa watu wa Israeli, kuambia yote yale Yahwe aliyomwamuru kuhusu wao.
In the fortithe yeer, in the enleuenth monethe, in the firste dai of the monethe, Moises spak to the sones of Israel alle thingis whiche the Lord commandide to hym that he schulde seie to hem,
4 Hii ilikuwa baada ya Yahwe kumvamia Sihoni mfalme wa Amoria, ambaye aliishi huko Heshboni, na Ogi mfalme wa Bashani, ambaye aliishi huko Ashtarothi ya Edrei.
after that he smoot Seon, kyng of Ammorreis, that dwellide in Esebon, and Og, the kyng of Basan, that dwelide in Asseroth and in Edray, ouer Jordan, in the lond of Moab.
5 Ng'ambo ya Yordani, katika nchi ya Moabu, Musa alianza kutangaza maelekezo haya, akisema,
And Moyses bigan to declare the lawe, and to seie,
6 “Yahwe Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, akisema, umeishi vya kutosha katika milima ya nchi hii.
Oure Lord God spak to vs in Oreb, and seide, It suffisith to you that ye han dwellid in this hil;
7 Geuka na uanze safari yako, na uende kwenye nchi ya milima ya Amorites, na kwenye maeneo yote karibu na tambarare ya mto Yordani, katika nchi ya milima, na nyanda za chini, huko Negev, na pwani - nchi ya Wakanani na huko Lebanoni mbali ya mto mkuu wa Euphratesi.
turne ye ayen, and come ye to the hil of Amorreis, and to othere placis that ben next it; to places of feeldis, and of hillis, and to lowere places ayens the south, and bisidis the brenke of the see, to the lond of Cananeys, and of Liban, `til to the greet flood Eufrates.
8 Tazama, nimetenga nchi kwa ajili yako, nenda ndani na umiliki nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kuwapa na uzao wao baada yao.
Lo, `he seith, Y haue youe to you; entre ye, and `welde ye `that lond on which the Lord swoor to youre fadrys, Abraham, Ysaac, and Jacob, that he schulde yyue it to hem, and to her seed after hem.
9 Nilisema nawe kwa wakati huo, nikisema, siwezi nikakubeba peke yangu,
And Y seide to you in that time, Y may not aloone susteyne you, for youre Lord God hath multiplied you,
10 Yahwe Mungu wako amekuzidisha, na tazama, leo umekuwa umati wa nyota angani.
and ye ben ful many to dai, as the sterris of heuene;
11 Yahwe aweza, Mungu wa baba zako, kukufanya wewe mara elfu moja zaidi ya ulivyo, na kukubariki, kama alivyokuahidi!
the Lord God of youre fadris adde to this noumbre many thousyndis, and blesse you, as he spak.
12 Lakini inawezekanaje mimi peke yangu kubeba shehena zako, mizigo yako, na migogoro yako?
Y may not aloone susteyne youre causis, and birthun, and stryues; yyue ye of you men wise `in dyuyn thingis,
13 Chukua wanaume wa hekima, wanaume waelewa, na wanaume walio na sifa nzuri toka kila kabila, nitawafaya kuwa vichwa juu yenu.
and witti `in mennus thingis worthi to be don, whose conuersacioun is preued in youre lynagis, that Y sette hem princes to you.
14 Mlinijibu na kusema, 'Jambo ulilolisema ni zuri kwetu kufanya.'
Thanne ye answeriden to me, The thing is good which thou wolt do.
15 Kwa hiyo nilichukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wa hekima, na wanaume wenye sifa nzuri, na nikawafanya kuwa vichwa juu yenu, jemedari kwa elfu, jemedari kwa hamsini, jemedari kwa kumi, na maakida, kabila kwa kabila.
And Y took of youre lynagis men wise and noble, `in vertues and kyn; and Y ordeynede hem princis, tribunes, and centuryouns, and quynquagenaries, and denys, whiche schulden teche you all thingis.
16 Niliwaamuru waamuzi wenu kwa wakati huo, kusema, 'Zikiliza mabishano kati ya ndugu zenu, na muhukumu ya haki kati ya ndugu na ndugu zake, na mgeni aliye pamoja naye.
And Y comaundide to hem, and seide, Here ye hem, and deme ye that that is iust, whether he be a citeseyn, whether a pilgrym.
17 Hamtaonesha upendeleo kwa yeyote katika mgogoro, mtasikia madogo na makubwa pia. Hamtaogopa uso wa mtu, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Migogoro iliyo migumu kwenu, mtaniletea mimi, na mimi nitaisikiliza.
No difference schal be of persones; ye schulen here so a litil man, `that is, pore, as a greet man, nether ye schulen take the persoone of ony man, for it is the doom of God. That if ony thing semeth hard to you, telle ye to me, and Y schal here.
18 Niliwaamuru kwa wakati huo mambo yote mtakayofanya.
And Y comaundide alle thingis whiche ye ouyten to do.
19 Tulisafiri toka Horebu na kwenda kupitia jangwa lile kubwa lote na lenye kutisha lile mliloliona, katika njia yetu kuelekea nchi ya milima huko Amorites, kama Yahwe Mungu wetu alivyotuamuru sisi, na tukaja Kadeshi ya Barnea.
Forsothe we yeden forth fro Oreb, and passiden bi a feerdful deseert, and grettiste wildirnesse, which ye sien, bi the weye of the hil of Ammorrey, as oure Lord God comaundide to vs. And whanne we hadden come in to Cades Barne,
20 Niliwambia, mmekuja kwenye nchi ya milima ya Amorites, ambayo Yahwe Mungu wetu anatupa sisi.
Y seide to you, Ye ben comen to the hil of Ammorrey, which youre Lord God schal yyue to you;
21 Tazama, Yahwe Mungu wenu amekwisha weka nchi mbele yenu; nenda juu, muimiliki, kama Yahwe, Mungu wa baba zenu, amekwisha zungumza nanyi, msiogope wala kukata tamaa.
se thou the lond which thi Lord God schal yyue to thee; `stie thou, and welde it, as oure Lord God spak to thi fadris; `nyle thou drede, nether `drede thou in herte ony thing.
22 Kila moja wenu alikuja kwangu na kusema, 'Basi tutume watu mbele yetu, ili kwamba waweze kupepeleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea sisi neno kuhusiana na njia ya wapi tuvamie, na kuhusiana na miji tutakayoingia.
And alle ye neiyiden to me, and ye seiden, Sende we men, that schulen biholde the lond, and telle to vs bi what weye we owen stie, and to whiche citees we owen to go.
23 Shauri hilo lilinibariki mimi, 'Nilichukua watu kumi na mbili kutoka kwenu, mtu moja kwa kila kabila.
And whanne the word pleside to me, Y sente of you twelue men, of ech lynage oon.
24 Waligeuka na kwenda juu ya nchi ya milima, kufika kwenye bonde la Eshcol na kufanya upepelezi wa kina.
And whanne thei hadden go, and hadden stied in to the hilli places, thei camen `til to the valei of Clustre; and whanne thei hadden biholde the lond,
25 Walichukua baadhi ya mazao ya ardhi mikononi mwao na kuleta kwetu, Pia walileta neno na kusema, 'Ni nchi nzuri ambayo Yahweh Mungu wetu anatupa sisi'
thei token of the fruytis therof, to schewe the plentee, and brouyten `to vs, and seiden, The lond is good which oure Lord God schal yyue to vs.
26 Bado mlikataa kushambulia, lakini mliasi dhidi ya amri ya Yahwe Mungu wenu.
And ye `nolden stie, but ye weren vnbileueful to the word of oure Lord God.
27 Mlilalamika katika mahema yenu na kusema, “Ni kwa sababu Yahwe alituchukia sisi kwa kuwa ametutoa katika nchi ya Misri, kuteweka katika mikono ya Amorites kutuangamiza.
And ye grutchiden in youre tabernaclis, and ye seiden, The Lord hatith vs, and herfor he ledde vs out of the lond of Egipt, that he schulde bitake vs in the hond of Ammorey, and schulde do awei vs.
28 Tuende wapi sasa? Ndugu zetu wamefanya mioyo yetu kuyeyuka, kusema, Hao watu ni wakubwa na warefu zaidi yetu, miji yao ni mikubwa na imeimarishwa kwenda mbinguni; zaidi ya yote, tumewaona wana wa Anakim huko”
Whidur schulen we stie? the messangeris maden aferd oure herte, and seiden, A grettiste multitude is, and largere in stature than we; the citees ben greete, and wallid `til to the heuene; we sien there the sones of Enachym, that is, giauntis.
29 Kisha nikasema nao, msitishwe wala msiwaogope.
And Y seide to you, `Nyle ye drede `with ynne, nether `drede withoutforth; the Lord God hym silf,
30 Yahwe Mungu wenu, ambaye aenda mbele yenu, atawapigania, kama yote aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu,
which is youre ledere, schal fiyte for you, as he dide in Egipt, while alle men sien.
31 na pia katika jangwa, ambapo mmekwisha muona Yahwe Mungu wenu jinsi alivyowabeba, kama mtu abebavyo mtoto wake, kokote mlikoenda mpaka kufika hapa.'
And ye sien in the wildirnesse, thi Lord God bar thee, as a man is wont to bere his litil sone, in al the weie bi which ye yeden til ye camen to this place.
32 Bado licha ya neno hili hakumwamini Yahwe Mungu wenu,
And sotheli nether so ye bileueden to youre Lord God, that yede bifor you in the weie,
33 aliyeenda mbele yenu kwenye njia kutafuta eneo kwa ajili yenu kuweka kambi, katika moto kwa usiku, katika mawingu kwa mchana.
and mesuride the place in which ye ouyten to sette tentis, and schewide in nyyt the weie to you bi fier, and in dai bi a piler of cloude.
34 Yahwe alisikia sauti ya maneno yenu na alikasirika; aliapa na kusema,
And whanne the Lord hadde herd the vois of youre wordis, he was wrooth,
35 Hakika hakuna mmoja ya hawa watu wa kizazi hiki kiovu wataona nchi nzuri ambayo niliapa kuwapa babu zao,
and swoor, and seide, Noon of the men of this werste generacioun schal se the good lond, which Y bihiyte vndur an ooth to youre fadris,
36 kasoro Kalebu mwana wa Jephuneeh; yeye ataiona. Yeye nitampa nchi ambayo amekwisha kuikanyanga, na watoto wake, kwa sababu alimfuata Yahwe kwa ukamilifu.'
outakun Caleph, the sone of Jephone; for he schal se it, and Y schal yyue to hym the lond on which he trad, and to hise sones, for he suede the Lord.
37 Pia Yahweh alinikasirikia mimi kwa sababu yenu, kusema, 'Wewe pia hautaingia huko,
Nether the indignacioun ayens the puple is wondirful, sithen the Lord was wrooth also to me for you, and seide,
38 Yoshua mwana wa Nuh, ambaye amesimama mbele yako, yeye ataingia, mtie moyo, kwani yeye atawaongoza Israeli kuimiliki.
Nether thou schalt entre thidur, but Josue, the sone of Nun, thi mynystre, he schal entre for thee; excyte and strengthe thou him, and he schal departe the lond bi lot to Israel.
39 Zaidi ya yote, watoto wenu wadogo, ambao mlisema watakuwa waathirika, ambao leo hawana elimu ya uzuri au ubaya-wataenda ndani huko. Wao nitawapa nchi hiyo, na wataimiliki.
Youre litle children, of whiche ye seiden, that thei schulden be led prisoneris, and the sones that kunnen not to dai the diuersite of good and of yuel, thei schulen entre; and Y schal yyue to hem the lond, and thei schulen welde it.
40 Lakini ninyi, geuka na muuanza safari kwenda jangwani kwa kuambaa njia ya bahari ya mianzi'.
Sotheli turne ye ayen, and go ye in to the wildirnesse, bi the weie of the Reed See.
41 Kisha mlinijibu na kusema kwangu, 'Tumetenda dhambi dhidi ya Yahwe, tutaenda juu na kupigana, tutafuata yote ambayo Yahwe Mungu wetu ametuamuru sisi kufanya'. Kila mtu miongoni mwenu aliweka silaha za vita, na mlikuwa tayari kuvamia nchi ya milima.
And ye answeriden to me, We synneden to the Lord; we schulen stie, and we schulen fiyte, as oure Lord God comaundide. And whanne ye weren arayed with armeris, and yeden `into the hil, the Lord seide to me,
42 Yahwe alisema nami, 'Waambie, msivamie na kupigana, kwa kuwa sitakuwa pamoja nanyi, na mtashindwa na adui zenu'.
Seie thou to hem, `Nyle ye stye, nether fiyte ye, for Y am not with you, lest ye fallen bifor youre enemyes.
43 Nilizungumza nanyi kwa njia hii, lakini hamkunisikiliza, Mliasi dhidi ya amri ya Yahwe, mlikuwa wenye kiburi na mlivamia nchi ya milima.
Y spak, and ye herden not; but ye `weren aduersaries to the comaundement of the Lord, and bolnden with prijde, and stieden in to the hil.
44 Lakini Amorites, ambayo waliishi katika nchi hiyo ya milima, walitoka dhidi yenu na kuwafukuza kama nyuki, na kuwapiga chini huko Seir, mbali kama Hormah.
Therfor Ammorrey yede out, that dwellide in the hillis, and he cam ayens you, and pursuede you, as bees ben wont to pursue, and killide fro Seir til Horma. And whanne ye turneden ayen,
45 Mlirudi na kulia mbele ya Yahwe; lakini Yahwe hakusikiliza sauti zenu, wala hakuwa makini kwenu.
and wepten bifor the Lord, he herde not you, nether wolde asente to youre vois;
46 Kwa hiyo mlibaki Kadeshi siku nyingi, siku zote mlibaki huko.
therfor ye saten in Cades Barne bi myche tyme.

< Torati 1 >