< Danieli 1 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja Yerusalemu na kuuzunguka mji ili kuzuia mahitaji yake yote.
In the third year of the reign of Jehoiakim king of Judah, came Nebuchadnezzar king of Babylon to Jerusalem, and laid siege against it;
2 Bwana alimpa Nebukadneza ushindi dhidi ya Yehoyakimu mfalme wa Yuda, na alimpatia vitu vitakatifu kutoka nyumba ya Mungu. Alivipeleka vitu hivyo mpaka katika nchi ya Babeli, kwa nyumba ya mungu wake, na aliviweka vitu vitakatifu katika hazina ya mungu wake.
and the Lord gave into his hand Jehoiakim king of Judah, and a part of the vessels of the house of God, and he brought them into the land of Shinar, into the house of his gods, —and, the vessels, brought he into the treasure-house of his gods.
3 Mfalme akamwambia Ashipenazi, afisa wake mkuu, awalete baadhi ya watu wa Israeli, wa familia ya kifalme na za kiungwana -
Then did the king give word to Ashpenaz, the chief of his eunuchs, —that he should bring in, of the sons of Israel, even of the seed royal, and of the nobles,
4 vijana wasio na hila, wenye mwonekano wa kuvutia, wenye ujuzi katika hekima yote, wenye kujawa na ufahamu na weledi, na wenye sifa za kutumika katika ikulu ya mfalme. Alitakiwa kuwafundisha maandiko na lugha ya Babeli.
youths in whom was no blemish, but comely of countenance, and skilful in all wisdom, and possessed of knowledge, and able to impart instruction, and who had vigour in them, to stand in the palace of the king, —and that they should be taught the learning and the tongue of the Chaldeans.
5 Mfalme aliwatengea kwa ajili yao fungu kutoka katika chakula chake kizuri kwa kila siku na katika divai aliyokunywa. Vijana hawa walitakiwa kufunzwa kwa miaka mitatu, na baada ya hapo, wangeweza kumtumikia mfalme.
And the king appointed them the provision of each day upon its day, out of the delicacies of the king and out of the wine which he drank, and so to let them grow three years, —and, at the end thereof, that they should stand before the king.
6 Miongoni mwao walikuwa ni Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria, baadhi ya watu wa Yuda.
Now there were, among them, out of the sons of Judah, Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah;
7 Afisa mkuu aliwapa majina: Danieli alimwita Belteshaza, Hanania alimwita Shadraka, Mishaeli alimwita Meshaki, na Azaria alimwita Abedinego.
and the ruler of the eunuchs gave them names, —yea he gave to Daniel the name of Belteshazzar, and to Hananiah of Shadrach, and to Mishael of Meshach, and to Azariah of Abed-nego.
8 Lakini Danieli alinuia katika akili yake kuwa asingejitia ujanisi mwenyewe kwa chakula kizuri cha mfalme wala kwa divai ambayo alikunywa.
But Daniel laid it upon his heart, that he would not defile himself with the delicacies of the king, nor with the wine which he drank, —therefore sought he of the ruler of the eunuchs, that he might not defile himself.
9 Basi, aliomba ruhusa kutoka kwa afisa mkuu ili kwamba asije akajitia uchafu yeye mwenyewe. Hivyo, Mungu alimpa Danieli kibali na huruma kupitia katika heshima ambayo afisa mkuu alikuwa nayo kwake.
But, although God had brought Daniel into lovingkindness and tender compassion, before the ruler of the eunuchs,
10 Afisa mkuu alimwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme. Ameagiza aina ya chakula na vinywaji mnavyotakiwa kutumia. Kwa nini awaone ninyi mkiwa mnaonekana vibaya kuliko vijana wengine wa umri wenu? Mfalme aweza kukitwaa kichwa changu kwa sababu yenu.
yet said the ruler of the eunuchs unto Daniel, I do fear my lord the king, who hath appointed your food and your drink, —for why should he see your faces more sad than those of the youths of your own age? so should ye bring me under the penalty of mine own head unto the king.
11 Kisha Daniel akamwambia msimamizi ambaye afisa mkuu alikuwa amemweka juu ya Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria.
Then said Daniel, unto the overseer whom the ruler of the eunuchs had appointed over Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah:
12 Alisema, “Tafadhari tujaribuni, sisi watumishi wako kwa siku kumi. Tupatieni tu mboga mboga za kula na maji ya kunywa.
I pray thee—prove thy servants, ten days, —and let them give us vegetable food, that we may eat, and water that we may drink:
13 Kisha ulinganishe mwonekano wetu na mwonekano wa vijana wanaokula vyakula vya mfalme, na mtutendee, sisi watu wako kulingana na kile unachokiona.”'
then let our countenances be looked upon before thee, and the countenances of the youths who have been eating the delicacies of the king, —and, as thou shalt see, deal thou with thy servants.
14 Hivyo msimamizi alikubaliana naye kufanya hivi, na aliwajaribu kwa siku kumi.
So then he hearkened unto them, according to this word, —and proved them ten days;
15 Katika mwisho wa siku kumi mwonekano wao ulikuwa ni wenye afya nzuri kuliko wa wale vijana waliokula vyakula vya kifalme.
and, at the end of ten days, their countenances appeared more comely, and fatter in flesh, —than any of the youths who had been eating the delicacies of the king.
16 Basi, msimamizi aliliondoa fungu lao la chakula na vivywaji vyao na walipewa mboga mboga tu.
Thus it came about that the overseer continued taking away their delicacies, and the wine appointed them to drink, —and kept on giving them vegetable food.
17 Na kuhusu vijana hawa nne Mungu aliwapa uelewa na ufahamu katika maandiko yote na hekima, na Danieli aliweza kupambanua aina zote za maono na ndoto.
And, as for these four youths, God, gave them, knowledge and skill, in all learning and wisdom, —and, Daniel, had discernment, in all visions and dreams.
18 Katika mwisho wa muda uliokuwa umepangwa na mfalme kuwaleta ndani, afisa mkuu aliwaleta mbele ya Nebukadneza.
Now, at the end of the days after which the king had given word to bring them in, then did the ruler of the eunuchs bring them in, before Nebuchadnezzar.
19 Mfalme aliongea nao, na miongoni mwa kundi lote hapo hapakuwa na wa kuwalinganisha na akina Danieli, Hanania, Mishaeli, na Azaria. Walisimama mbele ya mfalme, wakiwa tayari kumtumikia.
So then the king, spake with them, and there was not found, from among them all, one like unto Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah, —therefore stood they before the king;
20 Katika kila swali la hekima na ufahamu ambalo mfalme aliwauliza, aliwakuta wakiwa na uwezo mara kumi kuliko waganga wote na wale waliojidai kusema na wafu, waliokuwa katika ufalme wake wote.
and, in any matter of wisdom and discernment as to which the king, enquired of them, he found them ten times better than all the sacred scribes—the magicians, who were in all his realm.
21 Danieli alikuwa hapo mpaka mwaka wa kwanza wa Mfalme Koreshi.
Now Daniel continued, until the first year of Cyrus the king.