< Danieli 8 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
La troisième année du règne du roi Belschatsar, une vision m'apparut, à moi, Daniel, après celle qui m'était apparue la première fois.
2 Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
Je vis la vision. Or, lorsque j'ai eu la vision, j'étais dans la citadelle de Suse, qui est dans la province d'Élam. Je vis dans la vision, et je me trouvais près du fleuve d'Ulai.
3 Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
Alors je levai les yeux et je regardai, et voici, un bélier qui avait deux cornes se tenait devant le fleuve. Les deux cornes étaient hautes, mais l'une était plus haute que l'autre, et la plus haute montait la dernière.
4 Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
Je vis le bélier qui poussait vers l'ouest, vers le nord et vers le sud. Aucun animal ne pouvait se dresser devant lui. Il n'y avait personne qui pût délivrer de sa main, mais il faisait ce qu'il voulait, et il se glorifiait.
5 Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
Comme je considérais, voici qu'un bouc vint de l'ouest sur la surface de toute la terre, et ne toucha pas le sol. Le bouc avait une corne remarquable entre les yeux.
6 Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
Il s'approcha du bélier aux deux cornes, que je voyais debout devant le fleuve, et se précipita sur lui dans la fureur de sa puissance.
7 Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
Je l'ai vu s'approcher du bélier, et il s'est mis en colère contre lui; il a frappé le bélier et lui a brisé les deux cornes. Le bélier n'avait pas la force de se tenir devant lui, mais il le jeta à terre et le piétina. Il n'y avait personne qui pût délivrer le bélier de sa main.
8 Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
Le bouc s'éleva à un haut degré d'orgueil. Quand il fut fort, la grande corne se brisa, et à sa place s'élevèrent quatre grandes cornes vers les quatre vents du ciel.
9 Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
De l'une d'elles sortit une petite corne, qui devint extrêmement grande, vers le midi, vers l'orient, et vers le pays glorieux.
10 Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
Elle s'éleva jusqu'à l'armée du ciel; elle jeta à terre une partie de l'armée et des étoiles, et les foula aux pieds.
11 Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
Elle s'éleva jusqu'au chef de l'armée; elle lui enleva l'holocauste perpétuel, et le lieu de son sanctuaire fut renversé.
12 Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
L'armée lui fut livrée, ainsi que l'holocauste perpétuel, par la désobéissance. Il a jeté la vérité par terre, et il a fait sa volonté et a prospéré.
13 Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
Alors j'entendis un saint qui parlait; et un autre saint dit à celui qui parlait: « Jusqu'à quand durera la vision concernant l'holocauste perpétuel, et la désobéissance qui désole, pour que le sanctuaire et l'armée soient foulés aux pieds? »
14 Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
Il me dit: « Jusqu'à deux mille trois cents soirs et matins. Alors le sanctuaire sera purifié. »
15 Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
Lorsque moi, Daniel, j'eus vu la vision, je cherchai à la comprendre. Et voici que se tenait devant moi quelqu'un qui avait l'apparence d'un homme.
16 Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
Entre les rives de l'Oulaï, j'entendis la voix d'un homme qui appelait et disait: « Gabriel, fais comprendre la vision à cet homme. »
17 Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
Il s'approcha donc de l'endroit où je me tenais; quand il arriva, j'eus peur et je tombai sur ma face; mais il me dit: « Comprends, fils d'homme, car la vision appartient au temps de la fin. »
18 Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
Comme il me parlait, je tombai dans un profond sommeil, le visage contre terre, mais il me toucha et me redressa.
19 Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
Il dit: « Voici, je vais te faire connaître ce qui arrivera au dernier moment de la colère, car cela appartient au temps fixé de la fin.
20 Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
Le bélier que tu as vu, qui avait deux cornes, ce sont les rois de Médie et de Perse.
21 Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
Le bouc rude, c'est le roi de Grèce. La grande corne qui est entre ses yeux, c'est le premier roi.
22 Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
Quant à ce qui a été brisé, à la place où quatre se sont levés, quatre royaumes se lèveront de la nation, mais non avec sa puissance.
23 Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
« Au dernier temps de leur règne, quand les transgresseurs seront au comble, se lèvera un roi à la face farouche, et qui comprendra des énigmes.
24 Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
Sa puissance sera grande, mais non par sa propre force. Il fera des ravages et prospérera dans ce qu'il fera. Il détruira les puissants et le peuple saint.
25 Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
Par sa politique, il fera prospérer la tromperie dans sa main. Il se glorifiera dans son cœur, et il détruira beaucoup de gens dans leur sécurité. Il se dressera aussi contre le prince des princes, mais il sera brisé sans mains humaines.
26 Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
« La vision des soirs et des matins qui a été racontée est vraie; mais scellez la vision, car elle concerne de nombreux jours à venir. »
27 Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.
Moi, Daniel, je me suis évanoui et j'ai été malade pendant quelques jours. Puis je me suis levé et j'ai fait les affaires du roi. Je m'interrogeais sur la vision, mais personne ne la comprenait.