< Danieli 8 >
1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
In year three of [the] reign of Belshazzar the king a vision it appeared to me I Daniel after the [one] which it appeared to me at the beginning.
2 Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
And I saw in the vision and it was when saw I and I [was] in Susa the citadel which [is] in Elam the province and I saw in the vision and I I was at [the] canal of Ulai.
3 Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
And I lifted up eyes my and I saw and there! - a ram one [was] standing before the canal and [belonged] to it two horns and the two horns [were] high and the one [was] high more than the second and the high [one] [was] growing up at the last.
4 Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
I saw the ram thrusting west-ward and north-ward and south-ward and any living creatures not they stood before it and there not [was one] delivering from hand its and it did according to pleasure its and it magnified itself.
5 Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
And I - I was observing and there! [the] he-goat of the goats [was] coming from the west over [the] surface of all the earth and not [it was] touching the earth and the he-goat a horn of conspicuousness [was] between eyes its.
6 Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
And it came to the ram [the] possessor of the two horns which I had seen standing before the canal and it ran against it in [the] rage of strength its.
7 Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
And I saw it approaching - beside the ram and it was enraged against it and it struck the ram and it broke [the] two horns its and not it was strength in the ram to stand before it and it threw it [the] ground towards and it trampled it and not anyone was delivering the ram from hand its.
8 Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
And [the] he-goat of the goats it magnified itself up to muchness and just as became mighty it it was broken the horn great and they grew up conspicuousness four in place its to [the] four [the] winds of the heavens.
9 Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
And from the one of them it came out a horn one from a small [thing] and it became great excess to the south and to the east and to the beauty.
10 Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
And it became great to [the] host of the heavens and it made fall [the] ground towards some of the host and some of the stars and it trampled them.
11 Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
And to [the] commander of the host it magnified itself and from him (it was removed *Q(K)*) the perpetual [offering] and it was thrown down [the] place of sanctuary his.
12 Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
And an army it will be set over the perpetual [offering] in transgression and it will throw down truth [the] ground towards and it will act and it will succeed.
13 Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
And I heard! one holy [one] speaking and he said one holy [one] to the certain [one] who was speaking until when? [will be] the vision the perpetual [offering] and the transgression desolate to give over and [the] sanctuary and an army trampling.
14 Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
And he said to me until evening morning two thousand and three hundreds and it will be put right [the] sanctuary.
15 Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
And it was when saw I I Daniel the vision and I sought! understanding and there! [was] standing to before me like [the] appearance of a man.
16 Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
And I heard [the] voice of a person between Ulai and he called and he said O Gabriel explain to this [one] the vision.
17 Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
And he came beside standing place my and when came he I was terrified and I fell! on face my and he said to me understand O son of humankind that [is] for [the] time of [the] end the vision.
18 Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
And when spoke he with me I was dazed on face my [the] ground towards and he touched me and he made stand me on standing place my.
19 Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
And he said here I [am] making known to you [that] which it will be at [the] end of the indignation for [it is] for [the] appointed time of [the] end.
20 Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
The ram which you saw [the] possessor of the two horns [is] [the] kings of Media and Persia.
21 Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
And the he-goat hairy [is] [the] king of Greece and the horn great which [is] between eyes its it [is] the king first.
22 Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
And the broken [horn] and they arose four [horns] in place its four kingdoms from a nation they will arise and not with power its.
23 Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
And at [the] end of reign their when are completed the rebels he will arise a king strong of face and understanding of intrigue.
24 Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
And it will be mighty power his and not by own power his and wonders he will destroy and he will succeed and he will act and he will destroy mighty [ones] and a people of holy [ones].
25 Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
And on insight his and he will make successful deceit by hand his and in heart his he will magnify himself and in prosperity he will destroy many [people] and on a prince of princes he will stand and by not a hand he will be broken.
26 Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
And [the] vision of the evening and the morning which it has been told [is] truth it and you keep secret the vision for [it is] for days many.
27 Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.
And I Daniel I was done [in] and I was sick days and I arose and I did [the] work of the king and I was appalled on the vision and there not [was one] giving understanding.