< Danieli 8 >

1 Katika mwaka wa tatu wa utawala wa mfalme Belshaza, mimi Danieli niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata).
In the third year of the reign of King Belshazzar, a vision appeared to me, to me, Daniel, after that which appeared to me at the first.
2 Nilipokuwa nikiangalia katika ndoto, niliona kwamba nilikuwa katika mji wa Shushani wenye ngome katika jimbo la Elamu. Niliona katika ndoto kuwa nilikuwa karibu na mfereji wa Ulai.
And I saw in a vision, and when I saw, I was in Shushan, in the palace, which is in the province of Elam; and I saw in a vision, and was by the river Ulai.
3 Nilitazama juu na nikaona mbele yangu kondoo dume lenye mapembe mawili, limesimama pembeni mwa mfereji. Pembe moja lilikuwa refu kuliko jingine, lakini pembe ndefu ilikuwa inakua pole pole kuliko ile fupi na pembe fupi ilirefuka na kuizidi nyingine.
And I lifted up my eyes and saw, and behold, there stood before the river a ram, which had two horns; and the two horns were high, and one was higher than the other; and the higher came up last.
4 Niliona kondoo mme akiishambulia magharibi, kisha kaskazini, na baadaye kusini; hakuna mnyama mwingine aliyeweza kusimama mbele yake. Hakuna yeyote aliyeweza kumwokoa yeyote katika mkono wake. Alifanya chochote kile alichokitaka, na alikuwa mtu mkubwa sana.
I saw the ram pushing westward and northward and southward, and no beast could stand before him, and none could deliver out of his hand; but he did according to his will and became great.
5 Na nilipokuwa natafakari juu ya haya, niliona beberu akitoka magharibi, na kuvuka katika uso wa dunia yote, akikimbia kwa kasi kana kwamba hakuonekana kama aligusa ardhini. Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake.
And I gave heed, and behold, a he-goat came from the west, over the face of the whole earth, without touching the ground; and the goat had a conspicuous horn between his eyes.
6 Alienda mpaka kwa kondoo aliyekuwa na pembe mbili, nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji na mbuzi alikimbia kumwelekea kondoo dume kwa hasira kali.
And he came to the ram which had two horns, which I had seen standing before the river, and ran against him in the fury of his power.
7 Niliiona mbuzi ikija karibu na kondoo. Mbuzi alikuwa na hasira na kondoo, alimpiga kondoo na alizivunja pembe zake mbili. Kondoo hakuwa na nguvu za kusimama mbele zake. Mbuzi alimgonga kondoo akaanguka chini na akamkanyaga. Hapakuwa na yeyote wa kumwokoa kutoka katika nguvu zake.
And I saw him come close to the ram, and he was enraged against him, and smote the ram, and broke in pieces his two horns; and there was no power in the ram to stand before him; and he cast him down to the ground, and stamped upon him; and none could deliver the ram out of his hand.
8 Ndipo mbuzi alikua akawa mkubwa, lakini alipokuwa na nguvu, pembe kubwa ilivunjwa, na katika sehemu yake zilichipuka na kukua pembe nne kubwa zilizochomoza kuelekea pepo nne za mbingu.
And the he-goat became exceedingly great; but when he became strong the great horn was broken, and instead of it grew up four conspicuous ones toward the four winds of heaven.
9 Kutoka katika pembe moja ilichipuka pembe nyingine, ilikuwa ndogo hapo awali, lakini baadaye ilikuwa pembe kubwa upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri.
And out of one of them came forth a little horn, which became exceedingly great toward the south, and toward the east, and toward the beautiful land.
10 Pembe ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita dhidi ya jeshi la mbinguni. Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani, na zilikanyagwa.
And it exalted itself even to the host of heaven, and some of the host and of the stars it cast down to the ground, and stamped upon them.
11 Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama kamanda wa jeshi la kimungu. Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye, na sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi.
Yea, he magnified himself even to the Prince of the host, and the daily sacrifice did he take away from him, and the place of his sanctuary was cast down.
12 Kwasababu ya uasi, pembe ya mbuzi ilipewa jeshi, na sadaka za kuteketezwa zitasitishwa. Pembe itautupa ukweli chini ardhini, na itafanikiwa katika kila jambo ilifanyalo.
And a host was placed over the daily sacrifice with impiety, and it cast down truth to the ground, and it accomplished its purpose and prospered.
13 Kisha nilimsikia mtakatifu mmoja akiongea na mtakatifu mwingine akamjibu, “Mambo haya yatadumu kwa muda gani, maono haya ya sadaka ya kuteketezwa, dhambi ile iletayo uharibifu, ukabidhiajia wa sehemu takatifu, na jeshi la mbinguni kukanyagwa?
And I heard a holy one speak; and another holy one said to the one that had spoken, To how long a time extendeth the vision concerning the daily sacrifice, and the impiety of the destroyer, to give both the sanctuary and the host to be trodden under foot?
14 Aliniambia, “Itadumu kwa jioni na asubuhi zipatazo 2, 300. Baada ya hapo, mahali patakatifu patawekwa sawa.”
And he said to me, To two thousand and three hundred evenings and mornings; then shall the sanctuary be cleansed.
15 Wakati mimi Danieli, nilipoona maono, nilijaribu kuyaelewa. na hapo mbele yangu alisimama yule aliyeoneakana kama mtu.
And it came to pass, that when I Daniel saw the vision, I sought for the meaning; and behold, there stood one before me having the appearance of a man.
16 Niliisikia sauti ya mtu ikiita katikati ya kingo za mfereji wa Ulai. Alisema, “Gabrieli, msaidie mtu huyu kuelewa maono.”
And I heard a man's voice between the banks of Ulai, which called and said, Gabriel, make this man to understand the vision.
17 Basi alikuja karibu na mahali niliposimama. Na alipokuja, niliogopa na nilisujudia hadi chini. Aliniambia,”Fahamu, mwana wa mtu, kwamba maono ni kwa ajili ya wakati wa mwisho.”
And he came near where I stood; and when he came, I was afraid, and fell upon my face, and he said to me, Understand, O son of man! for this vision relateth to the time of the end.
18 Alipokuwa anaongea na mimi, nilipata usiingizi mzito nikiwa nimelala kifudifudi. Kisha alinishika na kunisimamisha.
But when he spake to me, I sank senseless upon my face to the ground; but he touched me, and lifted me up where I had stood.
19 Akaniambia, “Tazama, nitakuonyesha kile kitachotokea baadaye katika kipindi cha ghadhabu, kwasababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho uliopangwa.
And he said, Behold, I make known to thee what shall be in the latter time of the indignation; for [[the vision relateth]] to the time of the end.
20 Na kuhusu kondoo mme uliyemwona, yule mwenye pembe mbili - ni wafalme wawili wa Umedi na Uajemi.
The ram which thou sawest, having two horns, denoteth the kings of Media and Persia.
21 Mbuzi dume ni mfalme wa Ugiriki. Pembe kubwa katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.
And the rough goat is the king of Greece; and the great horn between his eyes is the first king.
22 Na kuhusu pembe iliyovunjika, ambayo katika nafasi yake pembe zingine nne zilichipuka - hizi ni falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake, lakini hazitakuwa na nguvu kubwa.
And as that was broken, and four arose in its place, four kingdoms shall arise out of the nation, but not with his power.
23 Katika siku zijazo za falme hizo, wakati ambapo wahalifu watakuwa wamefikia kikomo chao, mfalme mwenye uso katili, na yeye mwenye akili sana, atainuka.
And toward the end of their reign, when the transgressors have filled up the measure of their iniquities, a king shall arise of a fierce countenance, and cunning in artifices.
24 Nguvu zake zitakuwa kubwa, lakini si kwa nguvu zake mwenyewe. Atakuwa wa kustaajabisha kwa kile atakachokuwa anakiharibu; atafanya na kufanikiwa. Atawaangamiza watu wenye nguvu, watu miongoni wa watakatifu.
And his power shall become mighty, but not by his own strength; and wonderfully will he destroy, and prosper, and accomplish his purposes, and he will destroy many, even the people of the holy ones.
25 Ataufanya udanganyifu usitawi chini ya mkono wake kwasababu ya ujanja wake. Atawaangamiza watu wengi bila kutegemea. Atainuka pia hata kinyume cha Mfalme wa wafalme, na atavunjwa, lakini si kwa mkono wowote wa binadamu.
And through his cunning will he cause fraud to prosper in his hand, and he will magnify himself in his heart, and he will destroy many in the midst of security, and against the Prince of princes will he stand up; but he shall be broken without hand.
26 Maono kuhusu jioni na asubuhi ulizoambiwa ni ya kweli. Lakini uyafunge maono haya, kwa kuwa yanahusu siku nyingi za wakati ujao.
And the vision of the evening and the morning, which was told thee, is true; but do thou seal up the vision, for it relates to many days.
27 Ndipo mimi, Danieli nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa. Kisha nikainuka na nikaenda kufanya kazi za mfalme. Lakini nilikuwa nimetishwa sana na maono, na hapakuwa na mtu yeyote aliyeweza kuyaelewa.
And I Daniel fainted, and was sick some days; then I rose up and did the king's business; and I was astonished at the vision, but no one explained it.

< Danieli 8 >