< Danieli 7 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza mfalme wa Babelli, Danieli alikuwa na ndoto na maono katika akili zake wakati alipokuwa amelala kitandani kwake. Kisha akayaandika yale aliyoyaona katika ndoto. Aliandika matukio ya muhimu sana:
Uti första årena Belsazars, Konungens i Babel, hade Daniel en dröm och syn på sin säng; och han skref den samma drömmen, och författade honom alltså:
2 Danieli alieleza, “Usiku katika ndoto zangu niliona pepo nne za mbinguni zilikuwa zinaitikisa bahari kuu.
Jag, Daniel, såg en syn om nattene, och si, de fyra väder under himmelen stormade emot hvartannat på stora hafvena.
3 Wanyama wakubwa wanne, kila mmoja alikuwa tofauti na mwenzake, walitoka katika bahari.
Och fyra stor djur stego upp utu hafvet, ju det ena annorlunda än det andra;
4 Mnyama wa kwanza alikuwa kama simba, lakini alikuwa na mabawa ya tai. Nilipokuwa natazama, mabawa yake yalikuwa yamepasuka na alikuwa ameinuliwa katika ardhi na alikuwa amesimama kwa miguu miwili kama mtu. Na alipewa akili za kibinadamu.
Det första såsom ett lejon, och hade vingar såsom en örn; jag såg till, intilldess att vingarne vordo thy afryckte, och det vardt tagit bort af jordene, och det stod på sina fötter såsom en menniska; och thy vardt ett menniskligit hjerta gifvet.
5 Na kulikuwa na mnyama wa pili, alikuwa kama dubu, na alikuwa ameinama, alikuwa na mbavu tatu katikati ya meno yake katika mdomo wake. Aliambiwa, 'Inuka na umeze watu wangi.'
Och si, det andra djuret dernäst var likt enom björn, och stod på den ena sidone, och hade i sinom mun, ibland sina tänder, tre stora långa tänder; och man sade till det: Statt upp, och ät mycket kött.
6 Baada ya hili, niliangalia tena. Kulikuwa na mnyama mwingine ambaye alionekana kama chui. Mgongoni mwake alikuwa na mabawa manne kama mabawa ya ndege, na alikuwa na vichwa vinne. Alipewa mamlaka ya kutawala.
Efter detta såg jag, och si, ett annat djur, likt enom parde, det hade fyra vingar, såsom en fogel, på sin rygg; och det samma djuret hade fyra hufvud, och thy vardt magt gifven.
7 Baada haya, niliona usiku katika ndoto yangu mnyama wa nne, mwenye kuogofya, na kutisha na mwenye nguvu. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; aliteketeza, na kuvunja vunja katika vipande, na kusaga saga katika miguuni pake kile kilichosalia. Alikuwa ni wa tofauti na wanyama wengine, na alikuwa na pembe kumi.
Efter detta såg jag i denna synene om nattena, och si, det fjerde djuret var grufveligit och förskräckligit, och mägta starkt, och hade stora jerntänder; åt omkring sig, och förkrossade, och hvad qvart var, trampade det med sina fötter. Det var ock mycket annars än de förra, och hade tio horn.
8 Na wakati nilipokuwa natafakari juu ya pembe, nilitazama na niliona pembe nyingine ndogo ilichipuka katikati ya pembe zingine. Mizizi ya pembe tatu kati ya pembe za mwanzo iling'olewa. Niliona katika pembe hii macho kama macho ya mtu na mdomo ambao ulikuwa ukijivuna kwa mambo makubwa.
Då jag nu skådade hornen, si, då gick der ut ibland dem ett annat litet horn, för hvilko de tre främsta hornen afstött vordo; och si, det samma hornet hade ögon såsom menniskoögon, och en mun, den stor ting talade.
9 Na nilipotazama, viti vya enzi vilikuwa vimewekwa, na Mtu wa siku za kale alikaa sehemu yake. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theruji, na nywele zake katika kichwa chake zilikuwa safi kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa na miali ya moto, na magurudumu yake yalikuwa yanawaka moto.
Sådant såg jag, tilldess stolar framsatte vordo, och den gamle satte sig, hvilkens kläde var snöhvitt, och håret på hans hufvud såsom ren ull; hans stol var alltsammans eldslåge, och hans hjul brunno af eld.
10 Mto wa moto ulitiririka kutoka mbele yake, na mamilioni ya watu walimtumikia, na wengine mia moja milioni walikuwa wamesimama mbele yake. Na mahakama iliitishwa, na vitabu vilifunguliwa.
Och af honom utgick en lång eldstrimma: Tusende sinom tusend tjente honom, och tio sinom hundrade tusend stodo för honom. Domen vardt hållen, och böckerna vordo upplåtna.
11 Niliendelea kuangalia kwasababu ya maneno ya kiburi yaliyosemwa na pembe. Nilitazama wakati mnyama anauliwa, na mwili wake uliharibiwa, na ulitolewa kwa ajili ya kuchomwa moto.
Jag såg till, för de stora ords skull, som det hornet talade; jag såg till, intilldess djuret dräpit vardt, och dess kropp förgicks, och i eld kastad vardt;
12 Na kwa wale wanyama wanne waliosalia, mamlaka yao yalitwaliwa mbali, lakini maisha yao yaliendelezea kwa kipindi fulani cha muda.
Och de andra djurs välde också ute var; ty dem var en tid och stund bestämd, huru länge hvartdera vara skulle.
13 Katika maono yangu usiku ule, nilimwona mtu mmoja anakuja katika mawingu ya mbinguni alikuwa kama mwana wa mtu; alikuja kwa Mzee wa Siku na aliletwa mbele zake.
Jag såg i denna synene om nattene; och si, en kom i himmelens sky, såsom ens menniskos Son, allt intill den gamla, och han vardt framhafd för honom.
14 Naye alipewa mamlaka ya kiutawala na utukufu na mamlaka ya kifalme ili kwamba watu wote, na mataifa na lugha ziweze kumtumikia yeye. Mamlaka yake ya kutawala ni mamlaka ya milele ambayo hayatapita, na ufalme wake ni ule ambao hautaangamizwa.
Honom gaf han våld, äro och rike, att all land, och folk, och tungomål, skulle tjena honom: Hans välde är evigt, det icke förgås, och hans rike hafver ingen ända.
15 Na kwangu mimi, Danieli, roho yangu ilihuzunishwa ndani yangu, na maono niliyoyaona katika akili zangu yalinisumbua.
Jag, Daniel, förskräckte mig derföre, och sådana syn förfärade mig.
16 Nilimsogelea mmoja wa hawa walikuwa wamesimama hapo na nikamwomba anioneshe maana ya mambo haya.
Och jag gick till en af dem som der stodo, och bad honom, att han skulle gifva mig en viss undervisning om allt detta; och han talade med mig, och tedde mig hvad det betydde:
17 Hawa wanyama nne wakubwa ni wafalme wanne ambao watatoa katika nchi.
Dessa fyra stora djur äro fyra rike, som på jordena komma skola;
18 Lakini watu watakatifu wa Mungu aliyejuu wataupokea ufalme na wataumiliki milele na milele.'
Men dens Högstas helige skola intaga riket och skola besitta det i evig tid.
19 Ndipo nilipotaka kujua zaidi juu ya mnyama wa nne, ambaye alikuwa tofauti sana na wengine na alikuwa wa kutisha pamoja na meno yake ya chuma na makucha ya shaba; alimeza, na alivunja vipande vipande, na alisaga saga kwa miguu yake kile kilichokuwa kimesalia.
Sedan hade jag gerna vetat en viss undervisning om det fjerde djuret, hvilket platt annars var, än all de andra, ganska grufveligit; det jerntänder och kopparklor hade, det omkring sig åt, och förkrossade, och det qvart var med sina fötter trampade;
20 Nilitaka kujua juu ya pembe kumi katika kichwa chake, na kuhusu pembe nyingine iliyochomoza, na ambayo mbele yake pembe zingine tatu zilianguka chini. Nilitaka kujua kuhusu pembe yenye macho na kuhusu mdomo uliokuwa unajisifu kwa mambo makubwa na ambayo ilionekana kuwa ni kubwa kuliko zingine.
Och om de tio horn på dess hufvud, och om det andra som uppväxte, för hvilko tre afföllo; och om det samma hornet som ögon hade, och en mun, som stor ting talade, och större var än de der bredvid voro.
21 Na nilipotazama, pembe hii iliinua vita dhidi ya watu watakatifu na ilikuwa inawawashinda mpaka pale
Och jag såg det samma hornet strida emot de heliga, och det behöll segren emot dem;
22 Mzee wa Siku alipokuja, na watu watakatifu wa Mungu Aliye Juu Sana. Ndipo wakati ulipowadia ambapo watu watakatifu waliupokea ufalme.
Tilldess den gamle kom, och höll dom för dens Högstas heligom, och tiden kom, att de helige intogo riket.
23 Hiki ndicho mtu yule alichokisema, 'Kwa habari ya mnyama wanne, utakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia ambao utakuwa tofauti na falme zingine zote. Utaimeza dunia yote, na utaikanyaga yote chini na kuivunja vunja vipande vipande.
Han sade alltså: Det fjerde djuret skall vara det fjerde riket på jordene, hvilket mägtigare skall vara än all rike; det skall uppäta, förtrampa och förkrossa all land.
24 Na kuhusu pembe kumi, kutoka katika ufalme huu, wafalme kumi watainuka, na mwingine atainuka baada yao. Atakuwa wa tofauti na wale waliomtangulia, na atawashinda wale wafalme watatu.
De tio horn betyda tio Konungar, som i de rikena uppkomma skola; efter dem skall en annan uppkomma, han skall vara mägtigare än någor af de förra, och skall undertrycka tre Konungar.
25 Atazungumza maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu sana na atawatesa watu watakatifu wa Mungu Aliye Juu. Atajaribu kuzibadili sikukuu na sheria. Mambo haya atapewa mikononi mwake kwa mwaka mmoja, miaka miwili na nusu mwaka.
Han skall försmäda den Högsta, och för störa dens Högstas heliga; och skall taga sig före att förvandla tider och lag; men de skola varda gifne uti hans hand i en tid, och några tider, och en half tid.
26 Lakini kikao cha mahakama kitaitishwa, na watazichukua nguvu zake za kifalme ili mwisho aweza kuharibiwa na kuteketezwa.
Derefter skall domen hållen varda; så skall då hans välde borttaget varda, så att han skall i grund förderfvad och förgjord varda.
27 Ufalme na utawala, ukubwa wa falme chini ya mbingu yote, watapewa watu walio wa watu watakatifu wa Yeye Aliye juu Sana. Ufalme wake ni ufalme wa milele, na falme zingine zote zitamtumikia na kumtii yeye.'
Men riket, magten och väldet under hela himmelen skall varda gifvit dens Högstas heligo folke, hvilkes rike evigt är; och allt välde skall tjena honom, och lyda honom.
28 Na huu ndio mwisho wa mambo. Na kuhusu mimi, Danieli, mawazo yangu yanihuzunisha sana mimi na mwonekano wa uso wangu ulibadilika. Lakini mambo haya niliyahifadhi mimi mwenyewe.”
Det var änden på talet. Men jag, Daniel, vardt svårliga bedröfvad i mina tankar, och mitt ansigte förvandlade sig uppå mig; dock behöll jag talet i mitt hjerta.

< Danieli 7 >