< Danieli 7 >

1 Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza mfalme wa Babelli, Danieli alikuwa na ndoto na maono katika akili zake wakati alipokuwa amelala kitandani kwake. Kisha akayaandika yale aliyoyaona katika ndoto. Aliandika matukio ya muhimu sana:
In the first year of Belshazzar king of Babylonia, Daniel had a dream and visions in his mind while lying on his bed. Then he wrote down what he had seen in the dream. He wrote down the most important events:
2 Danieli alieleza, “Usiku katika ndoto zangu niliona pepo nne za mbinguni zilikuwa zinaitikisa bahari kuu.
Daniel explained, “In my vision at night I saw that the four winds of heaven were stirring up the great sea.
3 Wanyama wakubwa wanne, kila mmoja alikuwa tofauti na mwenzake, walitoka katika bahari.
Four large animals, each one different from the other, came up out of the sea.
4 Mnyama wa kwanza alikuwa kama simba, lakini alikuwa na mabawa ya tai. Nilipokuwa natazama, mabawa yake yalikuwa yamepasuka na alikuwa ameinuliwa katika ardhi na alikuwa amesimama kwa miguu miwili kama mtu. Na alipewa akili za kibinadamu.
The first was like a lion but had eagle's wings. As I was looking, its wings were torn off and it was lifted from the ground and made to stand on two feet, like a man. The mind of a man was given to it.
5 Na kulikuwa na mnyama wa pili, alikuwa kama dubu, na alikuwa ameinama, alikuwa na mbavu tatu katikati ya meno yake katika mdomo wake. Aliambiwa, 'Inuka na umeze watu wangi.'
Then there was a second animal, like a bear, and it was bending over; it had three ribs between its teeth in its mouth. It was told, 'Get up and devour many people.'
6 Baada ya hili, niliangalia tena. Kulikuwa na mnyama mwingine ambaye alionekana kama chui. Mgongoni mwake alikuwa na mabawa manne kama mabawa ya ndege, na alikuwa na vichwa vinne. Alipewa mamlaka ya kutawala.
After this I looked again. There was another animal, one that looked like a leopard. On its back it had four wings like bird wings, and it had four heads. It was given authority to rule.
7 Baada haya, niliona usiku katika ndoto yangu mnyama wa nne, mwenye kuogofya, na kutisha na mwenye nguvu. Alikuwa na meno makubwa ya chuma; aliteketeza, na kuvunja vunja katika vipande, na kusaga saga katika miguuni pake kile kilichosalia. Alikuwa ni wa tofauti na wanyama wengine, na alikuwa na pembe kumi.
After this I saw in the visions of the night a fourth animal, terrifying, frightening, and very strong. It had large iron teeth; it devoured, broke in pieces, and trampled underfoot what was left. It was different from the other animals, and it had ten horns.
8 Na wakati nilipokuwa natafakari juu ya pembe, nilitazama na niliona pembe nyingine ndogo ilichipuka katikati ya pembe zingine. Mizizi ya pembe tatu kati ya pembe za mwanzo iling'olewa. Niliona katika pembe hii macho kama macho ya mtu na mdomo ambao ulikuwa ukijivuna kwa mambo makubwa.
While I was considering the horns, I looked and saw another horn grow up among them, a little horn. Three of the first horns were wrenched out by the roots. I saw in this horn eyes like the eyes of a man and a mouth that was boasting about great things.
9 Na nilipotazama, viti vya enzi vilikuwa vimewekwa, na Mtu wa siku za kale alikaa sehemu yake. Mavazi yake yalikuwa meupe kama theruji, na nywele zake katika kichwa chake zilikuwa safi kama sufu. Kiti chake cha enzi kilikuwa na miali ya moto, na magurudumu yake yalikuwa yanawaka moto.
As I looked, thrones were set in place, and the Ancient of Days took his seat. His clothing was as white as snow, and the hair of his head was like pure wool. His throne was flames of fire, and its wheels were burning fire.
10 Mto wa moto ulitiririka kutoka mbele yake, na mamilioni ya watu walimtumikia, na wengine mia moja milioni walikuwa wamesimama mbele yake. Na mahakama iliitishwa, na vitabu vilifunguliwa.
A river of fire flowed out from before him; millions served him, and one hundred million were standing before him. The court was in session, and the books were opened.
11 Niliendelea kuangalia kwasababu ya maneno ya kiburi yaliyosemwa na pembe. Nilitazama wakati mnyama anauliwa, na mwili wake uliharibiwa, na ulitolewa kwa ajili ya kuchomwa moto.
I continued to look because of the boastful words spoken by the horn. I watched while the animal was killed, and its body was destroyed, and it was given over to be burned up.
12 Na kwa wale wanyama wanne waliosalia, mamlaka yao yalitwaliwa mbali, lakini maisha yao yaliendelezea kwa kipindi fulani cha muda.
As for the rest of the four animals, their authority to rule was taken away, but their lives were prolonged for a period of time.
13 Katika maono yangu usiku ule, nilimwona mtu mmoja anakuja katika mawingu ya mbinguni alikuwa kama mwana wa mtu; alikuja kwa Mzee wa Siku na aliletwa mbele zake.
In my visions that night, I saw one coming with the clouds of heaven like a son of man; he came to the Ancient of Days and was presented before him.
14 Naye alipewa mamlaka ya kiutawala na utukufu na mamlaka ya kifalme ili kwamba watu wote, na mataifa na lugha ziweze kumtumikia yeye. Mamlaka yake ya kutawala ni mamlaka ya milele ambayo hayatapita, na ufalme wake ni ule ambao hautaangamizwa.
Authority to rule and glory and royal power were given to him so that all the peoples, nations, and languages should serve him. His authority to rule is an everlasting authority that will not pass away, and his kingdom is one that will never be destroyed.
15 Na kwangu mimi, Danieli, roho yangu ilihuzunishwa ndani yangu, na maono niliyoyaona katika akili zangu yalinisumbua.
As for me, Daniel, my spirit was grieved inside of me, and the visions I saw in my mind troubled me.
16 Nilimsogelea mmoja wa hawa walikuwa wamesimama hapo na nikamwomba anioneshe maana ya mambo haya.
I approached one of them standing there and asked him to show me the meaning of these things.
17 Hawa wanyama nne wakubwa ni wafalme wanne ambao watatoa katika nchi.
'These large animals, four in number, are four kings that will arise from the earth.
18 Lakini watu watakatifu wa Mungu aliyejuu wataupokea ufalme na wataumiliki milele na milele.'
But the holy people of the Most High will receive the kingdom, and they will possess it forever and ever.'
19 Ndipo nilipotaka kujua zaidi juu ya mnyama wa nne, ambaye alikuwa tofauti sana na wengine na alikuwa wa kutisha pamoja na meno yake ya chuma na makucha ya shaba; alimeza, na alivunja vipande vipande, na alisaga saga kwa miguu yake kile kilichokuwa kimesalia.
Then I wanted to know more about the fourth animal—it was so different from the others and very horrifying with its iron teeth and bronze claws; it devoured, broke into pieces, and trampled on what was left with its feet.
20 Nilitaka kujua juu ya pembe kumi katika kichwa chake, na kuhusu pembe nyingine iliyochomoza, na ambayo mbele yake pembe zingine tatu zilianguka chini. Nilitaka kujua kuhusu pembe yenye macho na kuhusu mdomo uliokuwa unajisifu kwa mambo makubwa na ambayo ilionekana kuwa ni kubwa kuliko zingine.
I wanted to know about the ten horns on its head, and about the other horn that grew up, and before which the three horns fell down. I wanted to know about the horn that had eyes and about the mouth that boasted about great things and that seemed greater than its companions.
21 Na nilipotazama, pembe hii iliinua vita dhidi ya watu watakatifu na ilikuwa inawawashinda mpaka pale
As I looked, this horn waged war against the holy people and was defeating them
22 Mzee wa Siku alipokuja, na watu watakatifu wa Mungu Aliye Juu Sana. Ndipo wakati ulipowadia ambapo watu watakatifu waliupokea ufalme.
until the Ancient of Days came, and justice was given to the holy people of the Most High. Then the time came when the holy people received the kingdom.
23 Hiki ndicho mtu yule alichokisema, 'Kwa habari ya mnyama wanne, utakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia ambao utakuwa tofauti na falme zingine zote. Utaimeza dunia yote, na utaikanyaga yote chini na kuivunja vunja vipande vipande.
This is what that person said, 'As for the fourth animal, it will be a fourth kingdom on earth that will be different from all the other kingdoms. It will devour the whole earth, and it will trample it down and break it into pieces.
24 Na kuhusu pembe kumi, kutoka katika ufalme huu, wafalme kumi watainuka, na mwingine atainuka baada yao. Atakuwa wa tofauti na wale waliomtangulia, na atawashinda wale wafalme watatu.
As for the ten horns, out of this kingdom ten kings will arise, and another will arise after them. He will be different from the previous ones, and he will conquer the three kings.
25 Atazungumza maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu sana na atawatesa watu watakatifu wa Mungu Aliye Juu. Atajaribu kuzibadili sikukuu na sheria. Mambo haya atapewa mikononi mwake kwa mwaka mmoja, miaka miwili na nusu mwaka.
He will speak words against the Most High and will oppress the holy people of the Most High God. He will try to change the festivals and the law. These things will be given into his hand for one year, two years, and half a year.
26 Lakini kikao cha mahakama kitaitishwa, na watazichukua nguvu zake za kifalme ili mwisho aweza kuharibiwa na kuteketezwa.
But the court will be in session, and they will take his royal power away to be consumed and destroyed at the end.
27 Ufalme na utawala, ukubwa wa falme chini ya mbingu yote, watapewa watu walio wa watu watakatifu wa Yeye Aliye juu Sana. Ufalme wake ni ufalme wa milele, na falme zingine zote zitamtumikia na kumtii yeye.'
The kingdom and the dominion, and the greatness of the kingdoms under the whole heaven, will be given to the people who belong to the holy people of the Most High. His kingdom is an everlasting kingdom, and all other kingdoms will serve and obey him.'
28 Na huu ndio mwisho wa mambo. Na kuhusu mimi, Danieli, mawazo yangu yanihuzunisha sana mimi na mwonekano wa uso wangu ulibadilika. Lakini mambo haya niliyahifadhi mimi mwenyewe.”
Here is the end of the matter. As for me, Daniel, my thoughts greatly alarmed me and my face changed in appearance. But I kept these things to myself.”

< Danieli 7 >