< Danieli 6 >
1 Ilimpendeza Dario kuchagua juu ya ufalme magavana wa majimbo 120 ambao wangetawala juu ya ufalme wote.
Il plut à Darius d'établir sur le royaume cent vingt gouverneurs locaux, qui devaient être répartis dans tout le royaume;
2 Juu yao kulikuwa na watawala wakuu watatu, na Daniel alikuwa mmoja wao. Hawa watawala waliwekwa ili waweze kuwasimamia magavana wa majimbo, ili kwamba mfalme asipate hasara.
et sur eux trois présidents, dont Daniel faisait partie, afin que ces gouverneurs locaux leur rendent compte et que le roi ne subisse aucune perte.
3 Danieli alipambanuliwa juu ya watawala wakuu na juu ya magavana wa majimbo kwasababu alikuwa na roho isiyo ya kawaida. Mfalme alikuwa akipanga kumweka juu ya ufalme wote.
Ce Daniel se distingua des présidents et des gouverneurs locaux, parce qu'il avait un esprit excellent, et le roi pensa à l'établir sur tout le royaume.
4 Basi watawala wakuu wengine na magavana wa majimbo walitafuta makosa katika kazi ambazo Danieli alizifanya kwa ufalme, lakini hawakuweza kuona ufisadi au kushindwa katika majukumu yake kwasababu alikuwa mwaminifu. Hakuna kosa au uzembe uliopatikana ndani yake.
Alors les présidents et les gouverneurs locaux cherchèrent à trouver une occasion contre Daniel en ce qui concerne le royaume; mais ils ne purent trouver ni occasion ni faute, parce qu'il était fidèle. Ils ne trouvèrent ni erreur ni faute en lui.
5 Kisha watu hawa wakasema, “Hatukuweza kupata sababu yoyote ya kumshitaki huyu Danieli isipokuwa tukitafuta kitu fulani dhidi yake kuhusiana na sheria za Mungu wake.'”
Alors ces hommes dirent: « Nous ne trouverons aucune occasion contre ce Daniel, à moins que nous ne la trouvions contre lui au sujet de la loi de son Dieu. »
6 Ndipo watawala hawa na magavana walileta mpango mbele ya mfalme. Walimwambia, “Mfalme Dario, uishi milele!
Alors ces présidents et ces gouverneurs locaux s'assemblèrent auprès du roi, et lui dirent ceci: « Roi Darius, vis éternellement!
7 Watawala wote wakuu wa ufalme, magavana wa mikoa, na magavana wa majimbo, washauri, na magavana wameshauriana kwa pamoja na kuamua kuwa wewe, mfalme, unapaswa kupitisha amri na kuitekeleza, ili kwamba mtu yeyote anayefanya dua kwa mungu yeyote au mtu kwa siku thelathini, isipokuwa wewe mfalme, mtu huyo lazima atupwe katika tundu la simba.
Tous les présidents du royaume, les députés et les gouverneurs locaux, les conseillers et les gouverneurs, se sont consultés pour établir une loi royale et un décret fort, selon lequel quiconque demandera une requête à un dieu ou à un homme pendant trente jours, sauf à toi, ô roi, sera jeté dans la fosse aux lions.
8 Sasa mfalme, litoe agizo na utie saini nyaraka ili kwamba isije ikabadilika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi, hivyo haiweze ikabatilishwa.
Maintenant, ô roi, établis le décret et signe l'écrit, afin qu'il ne soit pas modifié, selon la loi des Mèdes et des Perses, qui ne change pas. »
9 Basi, mfalme Dario alitia saini nyaraka kwa kuifanya amri kuwa sheria.
Le roi Darius signa donc l'écrit et le décret.
10 Danieli alipojua kuwa nyaraka imekwisha kusainiwa kuwa sheria, alienda ndani ya nyumba yake (madirisha yake katika chumba cha juu yalikuwa wazi kuelekea Yerusalemu), na alipiga magoti yake, kama alivyokuwa akifanya mara tatu kwa siku, na aliomba na kushukuru mbele ya Mungu wake, kama alivyofanya hapo kabla.
Lorsque Daniel sut que l'écriture était signée, il entra dans sa maison (les fenêtres de sa chambre étaient maintenant ouvertes vers Jérusalem) et il se mit à genoux trois fois par jour, et pria, et rendit grâce devant son Dieu, comme il le faisait auparavant.
11 Kisha watu hawa walikuwa wameunda hila kwa pamoja walimwona Danieli akiomba na kutafuta msaada kutoka kwa Mungu.
Alors ces hommes s'assemblèrent et trouvèrent Daniel en train de prier et de supplier son Dieu.
12 Ndipo walipomwendea mfalme na kuongea naye kuhusiana na amri yake: “Je haukuweka amri kwamba mtu yeyote akayefanya maombi kwa mungu mwingine au kwa binadamu ndani ya siku thelathini zijazo, isipokuwa kwako wewe, mfalme, lazima mtu huyo atupwe katika tundu la simba? Mfalme akajibu, “Jambo hili ni la hakika, kama ilivyoelekezwa katika sheria za Wamedi na Waajemi; ambazo haziwezi zikabatilishwa.”
Alors ils s'approchèrent et parlèrent devant le roi au sujet du décret du roi: « N'as-tu pas signé un décret selon lequel tout homme qui, dans les trente jours, adressera une requête à un dieu ou à un homme, sauf à toi, ô roi, sera jeté dans la fosse aux lions? ». Le roi répondit: « Cette chose est vraie, selon la loi des Mèdes et des Perses, qui ne change pas. »
13 Kisha wakamjibu mfalme, “Mtu yule Daniel, ambaye ni mmoja wa watu wa mateka kutoka Yuda, hakutii wewe, mfalme wala maagizo yako uliyoyasaini. Yeye humwomba Mungu wake mara tatu kwa siku.”
Alors ils prirent la parole et dirent devant le roi: « Ce Daniel, qui est d'entre les enfants de la captivité de Juda, ne te respecte pas, ô roi, ni le décret que tu as signé, mais il fait sa demande trois fois par jour. »
14 Mfalme aliposikia haya, alisikitishwa sana, alitumia akili jinsi ya kumwokoa kutoka katika utawala huu. Alisumbuka sana mpaka wakati wa kuzama kwa jua akijaribu kumwokoa Danieli.
Alors le roi, en entendant ces paroles, fut très mécontent, et il jeta son dévolu sur Daniel pour le délivrer; et il travailla jusqu'au coucher du soleil pour le secourir.
15 Kisha watu hawa waliokuwa wamepanga njama walikusanyika kwa pamoja na mfalme, na wakamwambia, “Ujue mfalme kwamba ni sheria ya Wamedi na Waajemi kwamba hakuna amri au sanamu ambayo mfalme anaipitisha yaweza kubadilishwa.”
Alors ces hommes s'assemblèrent auprès du roi et lui dirent: « Sache, ô roi, que c'est une loi des Mèdes et des Perses, qu'aucun décret ni aucune loi que le roi établit ne peut être modifié. »
16 Ndipo mfalme alitoa agizo, na walimleta ndani Danieli, na kisha wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako, ambaye unamtumikia daima, na akuokoe.''
Alors le roi ordonna qu'on amène Daniel et qu'on le jette dans la fosse aux lions. Le roi prit la parole et dit à Daniel: « Ton Dieu que tu sers sans cesse, il te délivrera. »
17 Jiwe lililetwa katika mlango wa tundu, na mfalme alilitia muhuri wa pete yake mwenyewe na pamoja na muhuri wa wakuu wake ili kwamba chochote kisiweze kubadilishwa kuhusiana na Danieli.
On apporta une pierre qu'on posa sur l'ouverture de la fosse, et le roi la scella de son propre sceau et du sceau de ses grands, afin que rien ne fût changé au sujet de Daniel.
18 Basi mfalme alienda kwenye ikulu yake na usiku ule alikuwa na mfungo. Hakuna starehe yoyote iliyoletwa mbele yake, nao usingizi ulimkimbia.
Le roi se rendit ensuite dans son palais, et passa la nuit à jeûner. On ne lui apporta aucun instrument de musique, et le sommeil le quitta.
19 Kisha katika mapambazuko mfalme aliamka na kwa haraka alienda kwenye tundu la simba.
Le roi se leva de grand matin, et se rendit en hâte à la fosse aux lions.
20 Na alipokaribia kwenye tundu, alimwita Danieli kwa sauti ya huzuni, akimwambia Danieli, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je Mungu wako ambaye anamtumkia daima ameweza kukuokoa kutoka katika simba?
Lorsqu'il s'approcha de la fosse, Daniel cria d'une voix troublée. Le roi prit la parole et dit à Daniel: « Daniel, serviteur du Dieu vivant, ton Dieu, que tu sers continuellement, est-il capable de te délivrer des lions? »
21 Ndipo Danieli akamwambia mfalme, “Mfalme, uishi milele!
Alors Daniel dit au roi: « O roi, vis éternellement!
22 Mungu wangu amemtuma mjumbe na amevifunga vinywa vya simba, na hazijaweza kunidhuru. Kwa kuwa sikuwa na hatia yoyote mbele yake na pia mbele yako, ewe mfalme, na sijakufanyia jambo lolote la kukudhuru.”
Mon Dieu a envoyé son ange et a fermé la gueule des lions, et ils ne m'ont pas fait de mal, parce que l'innocence a été trouvée en moi devant lui; et aussi devant toi, ô roi, je n'ai fait aucun mal. »
23 Basi mfalme alikuwa na furaha sana. Alitoa agizo kwamba wanatakiwa wamtoe Danieli nje ya tundu. Hivyo Danieli aliondolewa kutoka katika tundu. Hakuna dhara lolote lililoonekana kwake, kwa kuwa alikuwa amemtumainia Mungu wake.
Le roi se réjouit et ordonna qu'on fasse sortir Daniel de la fosse. On fit donc sortir Daniel de la fosse, et on ne lui trouva aucun mal, car il avait mis sa confiance en son Dieu.
24 Mfalme alitoa agizo, waletwe wale watu waliomshitaki Danieli na kisha akawatupa wao katika tundu la simba - wao, na watoto wao, na wake zao. Kabla hawajafika sakafuni, simba waliwararua na kuvunjavunja mifupa yao vipande vipande.
Le roi donna cet ordre. On amena les hommes qui avaient accusé Daniel et on les jeta dans la fosse aux lions, eux, leurs enfants et leurs femmes; les lions les déchiquetèrent et brisèrent tous leurs os avant qu'ils n'arrivent au fond de la fosse.
25 Kisha mfalme Dario aliandika ujumbe kwa watu wote, mataifa na lugha ambazo ziliishi katika dunia yote: “Amani na iongezeke kwenu.
Alors le roi Darius écrivit à tous les peuples, nations et langues qui habitent sur toute la terre: « Que la paix vous soit multipliée.
26 Ninaagiza kwamba katika utawala wote wa ufalme wangu watu watetemeka na kumcha mbele ya Mungu wa Danieli, kwa kuwa ni Mungu aliye hai na huishi milele, na ufalme wake hauwezi kuharibiwa; utawala wake utakuwepo hadi mwisho.
« Je décrète que dans toute la domination de mon royaume, les hommes tremblent et craignent devant le Dieu de Daniel. « Car il est le Dieu vivant, et inébranlable pour toujours. Son royaume est celui qui ne sera pas détruit. Sa domination s'étendra jusqu'à la fin.
27 Yeye anatuhifadhi salama na kutuokoa, na anafanya ishara na maajabu mbinguni na duniani; amemhifadhi Danieli salama dhidi ya uwezo wa simba.”
Il délivre et sauve. Il accomplit des signes et des prodiges dans le ciel et sur la terre, qui a délivré Daniel de la puissance des lions. »
28 Na hivyo basi, Danieli alifanikiwa katika utawala wa Dario na katika utawala wa Koreshi Mwajemi.
Ce Daniel prospéra donc sous le règne de Darius et sous le règne de Cyrus le Perse.